Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI 01/03/10
Soma Kutoka 20:15. Kisha sema: “Hata ikiwa watu wengi wanaheshimu amri hii, wengine wanafikiri kwamba kuiba na namna nyingine za kukosa uaminifu zinaweza kukubaliwa ikiwa mutu anapatikana katika hali ngumu sana. Wewe unafikiri nini? [Acha mutu ajibu.] Habari hii inazungumzia faida za kuwa siku zote mutu mwenye kutumainika.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 12.
Amkeni! Mwezi wa 3
“Watu wengi wanaheshimu Biblia lakini wanafikiri kwamba sehemu kubwa yake inatumika kwa kadiri ndogo katika ulimwengu wa leo. Wewe unafikiri nini? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Waroma 15:4.] Habari hii inaonyesha kwa nini hata sehemu ya agano la kale ingali yenye kufaa wakati wa leo.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 28.
MNARA WA MLINZI 01/04/10
“Wanapoulizwa ni mutu gani anayejulikana sana katika historia, wengi wanasema ni Yesu. Je, hayo ndiyo maoni yako? [Acha mutu ajibu.] Watu wana maoni yenye kupingana kuhusu Yesu. Ona kwa nini tunapaswa kujifunza kweli kumhusu. [Soma Yohana 17:3.] Gazeti hili la pekee la Mnara wa Mlinzi linaonyesha hasa yale ambayo Biblia inazungumzia kuhusu Yesu na mafundisho yake.”
Amkeni! Mwezi wa 4
“Inaoneka kwamba hatuna wakati wa kutosha ili kutimiza mambo yote ambayo tungetaka kufanya. Je, unakubaliana na hilo? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wameona shauri hili kuwa lenye kusaidia. [Soma Wafilipi 1:10.] Gazeti hili linatoa mapendekezo yenye kufaa ili kutusaidia kutumia wakati wetu vizuri.”