Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea watu katika Mwezi wa 2: Je, Kuna Muumba Anayekujali?, Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Mwezi wa 3: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mujikaze sana ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mwezi wa 4 na wa 5: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Munaporudilia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale waliohuzuria Ukumbusho ao matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawajiunge sana na kutaniko, mujikaze kuanzisha mafunzo ya Biblia kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote kwa ajili ya kipindi cha Ukumbusho mwaka wa 2011 itakuwa na kichwa “Je, Kanuni za Biblia Zinaweza Kutusaidia Kupambana na Matatizo ya Siku Zetu?”
◼ Hakuna mkutano wowote utakaofanywa siku ya Ukumbusho, yaani Siku ya Yenga tarehe 17 mwezi wa 4, isipokuwa tu mkutano kwa ajili ya mahubiri. Makutaniko ambayo kwa kawaida yanafanya mikutano ya kutaniko siku hiyo, yanaweza kuifanya siku ingine ya juma. Mahali ambapo makutaniko mengi yanatumia Jumba la Ufalme lile lile, na haitawezekana kubadili programu ya mikutano, basi wanaweza kuondoa mikutano. Kwa hiyo, familia zinatiwa moyo kuchunguza habari ya Funzo la Mnara wa Mlinzi wakati wa Ibada yao ya Familia ya mangaribi.