Jinsi ya Kuhubiri kwa Matokeo Barabarani
1. Ni katika njia gani moja tunaweza kumwiga Yesu?
1 Katika utumishi wake duniani, Yesu hakusita kuzungumza na watu aliokutana nao kwenye barabara na kwenye nafasi zingine za watu wote. (Luka 9:57-61; Yoh. 4:7) Alipenda watu wengi zaidi iwezekanavyo wasikie ujumbe wa maana aliokuwa nao. Leo, kuhubiri barabarana ni njia nzuri zaidi inayosaidia watu wapate hekima yenye kutoka kwa Mungu. (Met. 1:20) Tutapata matokeo mazuri zaidi ikiwa tunachukua hatua ya kukaribia watu na kutumia utambuzi.
2. Kwa nini ni lazima kukaribia watu tunapohubiri barabarani?
2 Karibia Watu: Kwa kawaida ni vizuri kukaribia watu kuliko kusimama ao kukaa mahali pamoja ili kungojea watu wanaopita njiani watukaribie. Onyesha sura ya kicheko, uwatazame watu usoni, na uzungumze nao kwa utulivu na kwa njia ya kirafiki. Ikiwa unatumika na wahubiri wengine, mara nyingi ni vizuri kila mmoja awakaribie watu yeye mwenyewe. Pia, utahitaji kujikaza ili kupata namna ya kurudilia tena mutu aliyependezwa ili kuzungumza naye. Ikiwa inafaa, mwishoni mwa mazungumzo, unaweza kumuuliza mutu kwa upole jinsi munavyoweza kuonana tena. Wahubiri fulani wanafanya mahubiri yao ya barabarani kwa ukawaida nafasi ileile, na hilo linawawezesha kuzungumza mara kwa mara na watu walewale na kuwasaidia wapendezwe zaidi.
3. Namna gani tunaweza kutumia utambuzi tunapohubiri barabarani?
3 Tumia Utambuzi: Inaomba kutumia utambuzi ili kujua mahali utasimama kwenye barabara na mutu unayepaswa kukaribia ili kuzungumza naye. Si lazima kuhubiria kila mutu anayepita njiani ao barabarani. Uwe mtazamaji mzuri. Kwa mfano, ikiwa mutu ni mwenye kuwa haraka, inaweza kuwa vizuri kumwacha apite zake. Unapohubiri mbele ya duka (magasin) fulani, uwe mwangalifu ili usimufanye msimamizi wa duka awe na wasiwasi kupita kiasi. Mara nyingi ni vizuri kuhubiria watu wanapoondoka katika duka kuliko kuwahubiria wanapoingia. Karibia watu ili kuzungumza nao kwa njia ambayo haitawaogopesha ao kuwashitusha. Pia, tumia utambuzi unapotolea watu vichapo. Ikiwa mutu hapendezwi sana na ujumbe wetu, unaweza kumtolea trakti kuliko kumtolea magazeti.
4. Kwa nini mahubiri ya barabarani ni njia ya kuhubiri yenye matokeo na yenye kufurahisha?
4 Kuhubiri barabarani kunatuwezesha kueneza mbegu nyingi za ukweli katika muda mfupi. (Mhu. 11:6) Watu fulani tunaokutana nao wanaweza kuwa wale ambao hatukute nyumbani tunapohubiri nyumba kwa nyumba. Kwa nini usifanye mipango ili kushiriki katika mahubiri ya barabarani, njia ya kuhubiri yenye matokeo mazuri na yenye kufurahisha?