Je! Umejaribu Mahubiri Ya Jioni?
1 Kazi yetu inapokuwa yenye kuzaa matunda, tunakuwa wenye kufurahia kuifanya. Kinyume na hilo, tunapokuwa hatuoni matokeo yoyote ya waziwazi, inakuwa yenye kuchosha na haituletei kamwe uradhi. Kazi ya maana ni yenye kudhawabisha na ni baraka. (Ona Muhubiri 3:10-13.) Tunaweza kutumikisha kanuni hiyo kuhusu kazi yetu ya kuhubiri. Tunajua hilo kutokana na ujuzi wa siku nyingi, tunapohubiri mlango kwa mlango na kwamba tunafikia kuanzisha mazungumzo juu ya Biblia, tunarudi nyumbani kwetu wenye kuburudishwa kiroho. Tunahisi hakika kwamba tulitimiza jambo fulani.
2 Katika mahali pengi, watu wengi hawapatikani nyumbani kwao tunapopita mapema mchana. Makutaniko fulani yalishindana na tatizo hilo kwa kuchukua mipango ili kuhubiri jioni, na yalipata matokeo mazuri. Mahali petu tutaweza kuhubiri na kusimamisha usiku unapoingia. Wahubiri wanaripoti kwamba kwa kupita baadaye mchana wanakuta watu zaidi makwao na, kwa ujumla, watu hao ni wenye starehe zaidi na waliyo tayari zaidi kusikiliza ujumbe wa Ufalme. Je! umejaribu mahubiri ya jioni katika eneo lenu?—Ona Marko 1:32-34.
3 Wazee Wanapanga Mahubiri ya Jioni: Katika makutaniko mengi, mikutano kwa ajili ya mahubiri inayopangwa mwisho wa kisha-mchana au mwanzoni mwa jioni inategemezwa vizuri. Tunaweza kufikiria wahubiri vijana wanaotoka shuleni kisha-mchana na watu wazima wanaomaliza kazi zao nyuma kidogo mchana. Kwa wahubiri fulani wasio na uwezekano wa kuhubiri mwishoni mwa juma, mahubiri ya jioni muda wa juma ni suluhisho lenye kutenda kazi linalowawezesha kushiriki kwa ukawaida katika mahubiri.
4 Mahubiri ya jioni yanaweza kufanywa kwa namna mbalimbali. Tunaweza kwenda nyumba kwa nyumba na kutolea magazeti au kitabu kinachokusudiwa muda wa mwezi. Pia ni wakati bora wa kuwatembelea watu ambao hawakuwako nyumbani kwao wakati wahubiri wengine walipopita mapema mchana au muda wa juma. Labda kuna pia mahali pengine ambapo panajitokeza vizuri kwa ajili ya ushuhuda wa barabarani, ambako tunaweza kukutana na watu wanaorudi kazini. Wengi wanaona kwamba jioni ni wakati bora kabisa ili kuwarudilia wale walioonyesha kupendezwa.
5 Tujionyeshe Kuwa Waangalifu na Wenye Akili: Kutoka wakati usiku umekwisha kuingia kunaweza kuwa kwenye hatari katika mitaa fulani ya miji yetu. Lingekuwa jambo la hekima kutembea tukiwa wawili au katika kikundi. Tunapenda kusema hapa juu ya vikundi vingi vya wahubiri wawili wawili wakiwa wenye kuhubiri pamoja katika barabara moja. Tukumbuke hili, ndugu: Kwa ujumla, haifai kutia wahubiri watatu watatu au wane mara moja, ili kuhubiri pamoja. (Ona Marko 6:7; Luka 10:1.) Tunaweza kuhubiri ama wenyewe, ama wawili wawili. Ingekuwa vizuri kuchagua barabara zenye kuangaziwa vizuri na kwenda tu katika mitaa ambamo tupo hakika vya kutosha kwamba hatutapatwa na hatari yoyote. Tunapogonga kwenye mlango, tujiweke nafasi kwa jinsi tuonekane na tujitambulishe waziwazi. Tujionyeshe kuwa wenye utambuzi. Kwa ujumla, ni vizuri kusimamisha utendaji wetu mwanzoni mwa jioni, badala ya kufanya ziara za kurudia nyuma wakati watu wengine wanapojitayarisha labda kulala.
6 Majira ya jua na pia jioni ambako hakuna mvua ni yenye kufaa hasa kwa mahubiri ya jioni. Yehova atabariki hakika bidii yetu ili kumtolea “utumishi mtakatifu mchana na usiku.”— Ufu. 7:15.