Tutafute Wale Wanaostahili
1 Maagizo ya Yesu kuhusu kazi ya kuhubiri yanaweza kuonekana kuwa jambo gumu. Alisema: “Katika jiji lote lile au kijiji chochote kile mtakapoingia, tafuteni ni nani humo anayestahili.” (Mt. 10:11) Kwa kuwa watu leo wanapitisha nyumbani wakati mdogo zaidi na zaidi, tunawezaje kufanya utafiti huo kwa matokeo?
2 Fikiria Eneo Lako: Anza kwa kufikiria eneo lako. Watu wanaelekea zaidi kuwa nyumbani wakati gani? Wanaweza kupatikana wapi mchana? Je, kuna siku fulani ya juma au wakati fulani wa mchana ambapo wanaweza kuitikia zaidi ziara? Kupatanisha huduma yako na kawaida na hali za watu katika eneo lako kunaweza kukusaidia upate matokeo bora zaidi.—1 Kor. 9:23, 26.
3 Wahubiri wengi wamepata mafanikio saa za mapema jioni. Wenye nyumba fulani wanatulia zaidi na wanaelekea zaidi kusikiliza wakati huo. Kutoa ushahidi kwa njia ya simu jioni kunaweza kuonekana kuwa kwenye matokeo. Kuhubiri katika eneo la biashara na kutoa ushahidi katika maeneo ya watu wote ni njia za kufikishia pia watu habari njema.
4 Mnamo mwezi wa utendaji wa pekee, kutaniko moja lilifanya mipango ya kutoa ushahidi mwishoni mwa mchana Siku ya Posho na Siku ya Yenga na kutoa ushahidi jioni Siku ya Tatu na Siku ya Tano. Walipanga pia kutoa ushahidi kwa njia ya simu na kuhubiri katika eneo la biashara. Mipango hiyo ilitokeza bidii nyingi kwa ajili ya huduma hivi kwamba kutaniko liliamua kuiendeleza.
5 Tufanye Ziara za Kurudia kwa Bidii: Ikiwa ni vigumu katika eneo lenu kupata watu nyumbani unaporudi kuwaona, jaribu mwishoni mwa kila ziara—kutia ndani ziara ya kwanza—kufanya mpango kamili wa kurudi tena. Kisha, hakikisha kwamba unatimiza mpango huo. (Mt. 5:37) Ikiwa inafaa, unaweza kuomba namba ya simu ya mwenye nyumba. Hilo pia linaweza kukusaidia uwasiliane naye tena.
6 Bila shaka, jitihada zetu zenye bidii za kutafuta wale wanaostahili na kufuatia kupendezwa tunakopata zitabarikiwa na Yehova.—Met. 21:5.