‘Mapenzi ya Mungu Yatendeke’
1. Mkusanyiko wa pekee wa siku moja wa mwaka wa utumishi wa 2012 una kichwa gani, na kwa nini kichwa hicho cha habari kinafaa?
1 Ikiwa tuliumbwa ni sababu ya mapenzi ya Yehova. (Ufu. 4:11) Kwa hiyo, maisha yetu hayawezi kuwa na kusudi ikiwa hatujifunze na kufanya mapenzi ya Mungu. Si rahisi kufanya mapenzi ya Mungu kwa kuwa tunapaswa kupiganisha mwelekeo wetu wa ndani wa kufanya “mambo yanayopendwa na mwili na fikira” ao wa kufanya “mapenzi ya mataifa.” (Efe. 2:3; 1 Pet. 4:3; 2 Pet. 2:10) Ikiwa Mungu hatusaidie, tunaweza ‘kushikwa tukiwa hai [na Ibilisi] kwa ajili ya mapenzi ya huyo.’ (2 Tim. 2:26) Mkusanyiko wetu wa pekee wa siku moja wa mwaka wa utumishi wa 2012 utasaidia kila mmoja wetu kuishi kulingana na ombi la tatu la sala ambayo Yesu alifundisha wanafunzi wake. (Mt. 6:9, 10) Kichwa cha mkusanyiko huo ni: ‘Mapenzi Yako Yatendeke.’
2. Ni maulizo gani yatakayojibiwa wakati wa programu?
2 Maulizo Ambayo Yatajibiwa: Unapofuata programu, tafuta majibu ya maulizo haya: Zaidi ya kusikia Neno la Mungu, jambo lingine la maana la kufanya ni nini? Namna gani tunaweza kujua kila mara yale ambayo Mungu anapenda tufanye? Kwa nini ni lazima tuwe tayari kuwahubiria watu wa namna zote? Namna gani unaweza kuwa na maisha yenye baraka nyingi na yenye kutosheleza? Ninyi vijana, ni jambo gani munalopaswa kumuhakikishia Yehova? Kufanya mapenzi ya Mungu kunaleta baraka gani? Kwa nini ni jambo la haraka kuwajenga wengine na kuwatia moyo?
3. Namna gani tunaweza kufaidika kabisa na mkusanyiko huu wa pekee wa siku moja?
3 Fanya yote uwezayo ili uhuzurie mkusanyiko huo na utakapofika azimia kufuata programu kwa uangalifu. Bila shaka msemaji aliyetumwa na Betheli ao mwangalizi mwenye kusafiri atakuwa kwenye mkusanyiko kama msemaji mgeni. Mbele na kisha programu, usisite kuzungumza naye na muke wake ikiwa ni mwenye kuoa. Munaporudi nyumbani, musiwe ‘wasikiaji wasahaulifu’ lakini murudilie programu katika familia ao kipekee na mufikirie yale munayoweza kufanya zaidi ili kuishi kulingana na mapenzi ya Mungu.—Yak. 1:25.
4. Kwa nini ni jambo la maana kutia mapenzi ya Mungu pa nafasi ya kwanza?
4 Hivi karibuni wale wanaofuatia tamaa zao na kukataa kuongozwa na mapenzi ya Yehova wataharibiwa. (1 Yoh. 2:17) Kwa hiyo sisi ni wenye shukrani kwa Yehova kwa kuwa ametayarisha programu hii kwa wakati unaofaa ili kutusaidia tutie mapenzi ya Mungu pa nafasi ya kwanza!