‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’
1. Namna gani mkusanyiko wa pekee wa siku moja ulikusaidia wewe na wengine?
1 Kisha kuhuzuria mkusanyiko wetu wa pekee wa siku moja, mara nyingi tunasema, “Hayo ndiyo tuliyohitaji!” Mwangalizi mmoja wa mzunguko alieleza kwamba, kisha kusikiliza programu, wahubiri fulani katika mzunguko wake walionyesha nia yao ya kuongeza saa wanazofanya katika mahubiri. Mwangalizi mmoja mwenye kusafiri alisema: “Ilitusaidia kujua waziwazi mahali tulipo katika kipindi cha wakati na kuchunguza upya maamuzi tunayofanya maishani.” Mwengine alisema: “Wahubiri wengi walisema kwamba hilo liliwasaidia wakumbuke waziwazi kwamba wanapasa kukaza akili juu ya kazi iliyo ya maana sana, yaani kazi ya kuhubiri.” Namna gani mkusanyiko wa pekee wa siku moja ulikusaidia?
2. Tutakuwa na programu gani katika mwaka wa utumishi unaokuja?
2 Programu ya mkusanyiko wa pekee wa siku moja ya mwaka wa utumishi ujao litakuwa ndilo jambo tunalohitaji. Kichwa cha mkusanyiko huo ni ‘Mkimbilie Yehova,’ kilichukuliwa kutoka katika andiko la Zaburi 118:8, 9. Habari fulani zitakazozungumziwa ni kama vile: “Yehova Ni Kimbilio Wakati wa Taabu—Namna Gani?,” “Saidia Wengine Wakimbilie Chini ya Mabawa ya Yehova,” “Mwige Yehova kwa Kuwatolea Wengine Mahali pa Kukimbilia,” “Vijana, Mumtegemee Yehova!” na “Paradiso Yetu ya Kiroho—Mahali pa Kukimbilia Ambapo Yehova Ametutolea.”
3. Namna gani tunaweza kufaidika kabisa na programu?
3 Jinsi ya Kufaidika na Programu: Tarehe ya mkusanyiko itakapotangazwa, chukua mipango ili kuhuzuria, na ualike watu unaojifunza nao Biblia ili wahuzurie pamoja nawe. Ili ‘tuzae matunda kwa uvumilivu,’ tunapaswa kuchunga akilini mambo tunayosikia. (Luka 8:15) Kwa hiyo, fuata programu kwa uangalifu, na uandike mambo machache na mafundisho ambayo unapenda kutumia katika maisha na katika kazi ya kuhubiri. Kisha mkusanyiko, muchukue wakati katika familia ili kuzungumzia programu, na jinsi familia yenu inavyoweza kutumia mafundisho hayo.
4. Kwa nini tunapaswa kungojea kwa hamu mkusanyiko wa pekee wa siku moja unaokuja?
4 Kama chakula chenye harufu nzuri na chenye kujenga, mkusanyiko wa pekee wa siku moja wa mwaka huu umetayarishwa kwa upendo na ufikirio mwingi. Yehova na awabariki munapojikaza kuhuzuria na kufaidika na ‘chakula hicho kwa wakati unaofaa,’ ambacho kimetayarishwa ili kulisha kiroho wahudumu Wakristo.—Mt. 24:45.