Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Pekee wa Siku Moja
Wakiwa wenye kutiwa nguvu na roho takatifu, Wakristo wa kwanza walijikaza sana ili kuhubiri habari njema mahali pote. (Mdo. 1:8; Kol. 1:23) Programu ya mkusanyiko wa pekee wa siku moja ya mwaka wa utumishi wa 2007, wenye kichwa: “Shughulika Sana na Lile Neno,” itatusaidia tufuate mfano wao bora—Mdo. 18:5.
Kuhusu Neno la Mungu, Mfalme Daudi alisema hivi: “Kikumbusho cha Yehova ni chenye kutegemeka, humfanya asiye na uzoefu awe na hekima.” (Zab. 19:7) Programu yenye kutayarishwa kwa uangalifu kwa ajili ya mkusanyiko wa pekee wa siku moja ya mwaka wa 2007 itakazia ulazima wa kutumia Maandiko ili “kunyoosha mambo” na itatutia moyo kutumia Neno la Mungu ili kuhubiri na kufundisha tukiwa wenye kutambua uharaka wa wakati (2 Tim. 3:16, 17) Programu hiyo mpya itaonyesha namna gani tunaweza kuepuka mitego na namna tunaweza kupata faida sisi wenyewe kwa kutumia kanuni za Biblia katika maisha yetu ya kila siku. Itatusaidia pia kutumia Neno la Mungu ili kusaidia vijana na wapya waweze kufanya maendeleo ya kiroho.
Fanya nguvu ili uhuzurie programu hiyo mwanzo mpaka mwisho, na usikilize kwa uangalifu. Andika mambo ya lazima; mambo unayoweza kutumia kipekee. Onyesha kwamba unafurahia mafundisho na vikumbusho vinavyotolewa kwa kusikiliza kwa uangalifu na kwa kuazimia kutumia maishani mambo unayojifunza.
Programu hiyo ya mkusanyiko wa pekee wa siku moja itatusaidia tusamini sana Neno la Mungu, itatukumbusha tuendelee kuhubiri habari njema ya Ufalme kwa bidii, na itatuonyesha jinsi ya kusaidia wengine wafanye hivyohivyo. Kwa hiyo, azimia ili usikose hata kidogo mwongozo wowote wa kiroho na mafundisho ambayo Yehova anatutolea katika njia hii!—Isa. 30:20b, 21.