Programu ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja Lijalo
“Tufanye Mambo Yote kwa Ajili ya Habari Njema,” hicho ndicho kitakachokuwa kichwa cha kusanyiko la pekee la siku moja linalofanyika tangu mwezi huu wa Septemba. (1 Kor. 9:23) Habari njema ya Ufalme ni habari ya muhimu zaidi ambayo husikilizwa kwa sasa. Kusanyiko litatusaidia kuwa wenye kutambua pendeleo pekee tunalo la kuwa wachukuaji wa habari hii ya ajabu. Zaidi ya hilo, litatutolea uhodari ili kuendelea kutangaza habari njema, bila kuacha.—Mdo. 5:42.
Programu itatuonyesha jinsi ya kutumia kikamilifu mazoezi yetu ya kitheokrasi ili kufanya mengi zaidi katika huduma. Tutawasikiliza Wakristo fulani waliofanya mabadiliko ili kuongeza utumishi wao, kwa mfano vijana ambao walijitoa kwa ajili ya maendeleo ya habari njema.—Ona Wafilipi 2:22.
Hotuba kuu, ambayo msemaji mwalikwa atatoa, itakazia ulazima wa kudumu kuwa sisi “twafaa kukabidhiwa habari njema.” (1 Thess. 2:4, TUM) Tutaona kwamba ili kulinda pendeleo la kutangaza habari njema, imetupasa kuendelea kutimiza matakwa na kanuni za Mungu iwe katika mafikiri kama vile katika mwenendo. Yatakayokaziwa ni pia baraka zinazotokana na hali hiyo.
Tusikose programu hiyo ya pekee. Watu ambao walijitoa wakfu kwa Yehova hivi karibuni na ambao wanatamani kubatizwa wakati wa kusanyiko hilo wangepaswa kumjulisha tangu sasa mwangalizi-msimamizi. Tuwaalike wale wote tunaojifunza nao Biblia. Tumruhusu Yehova kututia nguvu ili kufanya mambo yote kwa ajili ya habari njema na kumaliza hivi kazi kubwa hii kabla ya Harmagedoni.