Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 uku. 7
  • Programu mpya ya kusanyiko la pekee la siku moja

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu mpya ya kusanyiko la pekee la siku moja
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Komaza Nguvu Zako za Ufahamu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Programu ya Mkusanyiko wa Pekee wa Siku Moja ya 2010
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Programu Ya Kusanyiko La Pekee La Siku Moja Lijalo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 uku. 7

Programu mpya ya kusanyiko la pekee la siku moja

“Iweni Watu Wazima Katika Nguvu za Kuelewa” ndicho kitakuwa kichwa cha programu ya kusanyiko la pekee la siku moja kuanzia Septemba 2000. (1 Kor. 14:20) Kwa nini litakuwa jambo la lazima kwetu kuhudhuria? Tunaishi katika ulimwengu wenye kujaa uovu. Ili kushindana na hilo, tunapaswa kukuza nguvu zetu za kuelewa kiroho ili tuweze kushinda ubaya kwa wema. Ni hivyo kusanyiko la pekee la siku moja litatusaidia kufanya.

Katika kipindi cha kufungua cha mkusanyiko, mwangalizi wa mzunguko atazungumzia “Misaada ili Kuwa Watu Wazima Katika Kuelewa Biblia.” Atatuonyesha jinsi ya kuwa wenye kuimarika katika imani ya Kikristo. Msemaji mgeni atakazia jinsi matumizi ya kweli ya kanuni za Biblia yalivyo ya lazima katika kukuza ufahamu wenye akili; atazungumzia kichwa “Linda Hali ya Kiroho kwa Kuzoeza Nguvu Zako za Ufahamu.”

Vijana pia wanapaswa kukuza nguvu za kuelewa. Hilo litazungumziwa katika sehemu “Kwa Nini Kuwa Watoto Wachanga Sana Kuhusu Uovu” na “Vijana Ambao Hupata Uelewevu Sasa.” Wasikilize vijana wakieleza yale wanayofanya ili kujitia nguvu kiroho kusudi waweze kuzuia tamaa yoyote ya kutaka kujua utendaji mwovu wa ulimwengu na kuepuka matata.

Tunawezaje kupata furaha kubwa zaidi katika maisha? Msemaji mgeni ataeleza hilo katika hotuba ya mwisho “Faidikeni kwa Kutumikisha Kanuni za Biblia kwa Uelewevu.” Atatoa mifano ili kuonyesha kwamba kutumikisha Neno la Mungu kunatusaidia kukabiliana na matatizo, kuchukua maamuzi, na kufaidika kwelikweli kutokana na yale ambayo Yehova anatufundisha.

Wale wanaotaka kubatizwa katika maji ili kuonyesha wakfu wao kwa Mungu wanapaswa kumjulisha mwangalizi-msimamizi mapema zaidi iwezekanavyo. Tia alama kwenye kalenda yako wakati tu tarehe ya kusanyiko la pekee la siku moja itakapotangazwa, na uchukue mipango kamili ili kufaidika na programu hii nzuri sana. Usikose sehemu yoyote ya kusanyiko la pekee la siku moja! Hiyo itakutia nguvu ili kuvumilia mfumo huu mbovu na kubaki mwaminifu kwa Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine