Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/09 uku. 1
  • Programu ya Mkusanyiko wa Pekee wa Siku Moja ya 2010

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu ya Mkusanyiko wa Pekee wa Siku Moja ya 2010
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Mpango Mpya Kuhusu Kujikumbusha Programu za Mikusanyiko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Neno la Mungu Lina Nguvu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Programu mpya ya kusanyiko la pekee la siku moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2009
km 8/09 uku. 1

Programu ya Mkusanyiko wa Pekee wa Siku Moja ya 2010

1. (a) Mikusanyiko ya pekee ya miaka iliyopita ilikuwa na vichwa gani vinavyotegemea Biblia? (b) Je, kuna mambo fulani yaliyokusaidia katika mahubiri ambayo yalizungumziwa kwenye mikusanyiko ya pekee ya siku moja ya miaka iliyopita?

1“Mhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi,” “Msimame Imara Kama Kundi Moja,” “Muendelee Kutoa Ushahidi juu ya Kweli,” na “Sisi Ni Udongo na Yehova Ni Mfinyanzi Wetu.” (Flp. 1:9, 10, 27; Yoh. 18:37; Isa. 64:8) Hizo ni habari fulani tu kati ya zile zilizozungumziwa kwenye mikusanyiko ya pekee ya siku moja ya miaka iliyopita. Je, wewe ni mwenye kungojea kwa hamu mkusanyiko wa pekee wa siku moja wa mwaka wa utumishi wa 2010? Utakuwa na kichwa: “Wakati Uliobaki Umepungua,” na utategemea andiko la 1 Wakorintho 7:29.

2. Munaweza kufanya nini ili kuamsha hamu yenu kuhusu mkusanyiko wa pekee?

2 Munapotangaziwa tarehe ya mkusanyiko wa pekee katika kutaniko lenu, munaweza kuanza kuzungumzia kwa uchangamfu programu ya mkusanyiko huo. Wazazi fulani wanasaidia watoto wao wangojee kwa hamu mkusanyiko kwa kuandika tarehe ya mkusanyiko kwenye kalenda ya familia pamoja na vifaa ambavyo kila mutu anahitaji kuchukua watakapokwenda kwenye mkusanyiko, na kuanza kuhesabu siku mpaka tarehe ya mkusanyiko. Munapofanya Ibada ya Familia ya mangaribi, munaweza kurudilia mambo muliyoandika wakati wa mikusanyiko ya pekee ya miaka iliyopita. Pia, munaweza kutayarisha mioyo yenu kwa kuchunguza ukurasa wa 13-16 wa kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ili kusaidia kila mshiriki wa familia ‘akazie uangalifu jinsi anavyosikiliza.’—Luka 8:18.

3. Namna gani tunaweza kufaidika kabisa na mkusanyiko?

3 Tumia Mambo Unayojifunza: Mara nyingi kisha mkusanyiko tunasikia ndugu wakisema: “Ilikuwa programu nzuri kabisa!” Maneno hayo yanafaa kabisa, kwa kuwa mikusanyiko ni moja kati ya mipango ya Yehova yenye kutajirisha. (Met. 10:22) Ili mkusanyiko ukusaidie kuzaa matunda, unapaswa kufikiri sana juu ya habari zinazotolewa na kuzichunga moyoni. (Luka 8:15) Munaporudi nyumbani, mzungumze kuhusu programu mukiwa familia ao pamoja na wale mulio nao katika gari. Kila mutu anaweza kuzungumzia miradi anayoweza kujiwekea ambayo itamsaidia katika mahubiri. Kwa kufanya hivyo, mutafaidika kabisa na mambo yatakayotolewa kwenye mkusanyiko huo miaka mingi baadaye.—Yak. 1:25.

4. Kwa nini mkusanyiko huo utakuwa wa pekee kwetu?

4 Kwa kawaida, tunafurahi tunapopokea zawadi inayoweza kutusaidia. Je, tunangojea kwa hamu yale ambayo Yehova anatutayarishia kwenye mkusanyiko wetu wa pekee wa siku moja? Tuko hakika kwamba mkusanyiko huu utatusaidia katika kila hali. Tunaweza kutazamia baba wetu wa mbinguni Yehova atutolee zawadi inayofaa kwa kututia moyo na kutuzoeza ili kutimiza kazi yake.—2 Tim. 4:2; Yak. 1:17.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine