Programu Ya Kusanyiko La Pekee La Siku Moja Lijalo
Makusanyiko ya pekee ya siku moja yalianza kupangwa katika 1987. Mikusanyiko hiyo ya siku moja hujenga watumishi wa Yehova na watu wenye nia tayari wanaohudhuria. Kuanzia Septemba 1998, programu mpya itatolewa kwenye kusanyiko la pekee la siku moja. Mtafaidika kiroho na zile hotuba tisa, mahojiano mengi na mambo yaliyoonwa.
“Tuwe Wenye Kuthamini Meza ya Yehova,” ndicho kitakuwa kichwa cha kusanyiko hilo. (Isa. 65:14; 1 Kor. 10:21) Hilo litatia nguvu azimio letu la kuweka ibada ya Yehova pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu. (Zab. 27:4) Mwangalizi wa mzunguko atatoa sehemu yenye kichwa: “Kuchunguza Mielekeo ya Moyo Wetu,” ambayo itazungumzia msimamo wetu kuhusiana na kuhudhuria mikutano. Msemaji mwenye kuzuru atatoa hotuba yenye kichwa “Tunzeni Hali Yenu ya Kiroho kwa Kula Kwenye Meza ya Yehova.” Vitia-moyo vyenye kutumika vitatolewa vilevile kwa vijana walio washiriki wa tengenezo la Yehova ili wabaki thabiti katika kumtumikia Mungu. Hotuba kubwa ya msemaji mwenye kuzuru, yenye kichwa “Waliotiwa Nguvu Kiroho Ili Kutoa Ushahidi Wenye Ujasiri,” itatuonyesha namna mipango inayofanywa katika kutaniko inavyotusaidia kutoa ushahidi kuhusu Ufalme kwa ujasiri. Ni nani asiyetaka kufaidika na programu hiyo?
Watu waliojiweka wakfu kwa Mungu juzijuzi na ambao watamani kubatizwa wanapaswa kumjulisha mwangalizi-msimamizi kunapokuwa uwezekano. Huku tukiingia katika mwaka wa 12 wa makusanyiko ya pekee ya siku moja, tunasadiki kwamba kila mmoja atakayehudhuria atatoka akiwa mwenye kukomaa kiroho kwa ajili ya kazi yenye kuwa mbele.