Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja
Kichwa cha programu ya kusanyiko la pekee la siku moja kwa ajili ya mwaka mpya wa utumishi kina msingi mzuri wa Kimaandiko: “Jitiisheni Wenyewe kwa Mungu—Mpingeni Ibilisi.” (Yak. 4:7) Huo ni mwongozo wenye kufaa wakati huu mgumu! Kutii kwetu amri za Mungu kunafanya tukabiliane moja kwa moja na Shetani. Programu hii itatufundisha jinsi ya kusimama imara dhidi ya mipango miovu ya Ibilisi yenye kuharibu imani. Ni nini mambo fulani-fulani ya thamani tutakayopokea kwenye kusanyiko hilo?
Mwangalizi wa mzunguko ataonyesha jinsi “Kuonyesha Ujitiisho wa Kimungu Tukiwa Washiriki wa Familia” kunavyoimarisha familia ili kupinga mikazo ya ulimwengu. Hotuba ya kwanza ya msemaji-mgeni siku hiyo, “Mambo Ambayo Kupinga Ibilisi Kunamaanisha,” itaeleza kwa nini na jinsi tunavyohitaji kutenda kwa nguvu ili kupinga makusudi ya Shetani ya kuharibu hali yetu ya kiroho. Hotuba mbili zimetayarishwa hasa kwa ajili ya vijana, ambao wanapaswa pia kuwa wepesi kuelewa mbinu za Ibilisi. Wakristo wengi ambao sasa ni watu wazima walikataa kufuata tamaa za ulimwengu wakati walipokuwa vijana. Tutafurahi kusikia mengine ya mambo yao yaliyoonwa.
Ujitiisho kwa mamlaka unaombwa kwa wale wote wanaofanyiza jamii. Kwa hiyo, hotuba ya mwisho ya msemaji-mgeni itakazia sehemu nne ambazo katika hizo ujitiisho wetu wa kimungu unapaswa kuwa wazi: (1) kwa serikali, (2) katika kutaniko, (3) katika shughuli za kimwili, na (4) katika familia. Ni programu yenye kutumika kama nini!
Wale wanaotaka kubatizwa siku hiyo ya kusanyiko la pekee wanahitaji kujulisha mwangalizi-msimamizi mapema zaidi iwezekanavyo. Sisi sote tunapaswa kutia alama tarehe hiyo kwenye kalenda zetu na kuchukua mipango ili kuhudhuria programu yote ya kusanyiko. Baraka tunazopokea zitakuwa za milele kadiri tunavyojitiisha kwa Yehova milele.