Programu Ya Kusanyiko La Mzunguko Lijalo
“Shikeni Amri za Mungu Mkaishi,” ndicho kichwa cha kusanyiko la mzunguko lijalo, ambalo litaanza kufanywa mnamo Septemba. (Mez. 4:4) Kusanyiko hilo litatukumbusha sababu zinazofanya kutii amri za Mungu kusiwe jambo lenye uzito. Litatuonyesha vilevile katika njia gani kutimiza mapenzi ya Mungu hutokeza burudisho na furaha ya kweli, na pia tumaini la wakati ujao.—Mt. 11:28-30; Yn. 13:17.
Watu ambao, kulingana na amri ya Kristo, wanataka kubatizwa kwenye kusanyiko hilo wanapaswa kujulisha hilo kwa mwangalizi-msimamizi, ambaye atachukua mipango inayohitajika.—Mt. 28:19, 20.
Wakati wa hotuba-mfululizo, tutaona hali zenye kufaa ambazo katika hizo tutaweza kuonyesha upendo wetu kwa Mungu na kwa ndugu zetu. (Yn. 13:34, 35; 1 Yn. 5:3) Tutachunguza vilevile mashauri yenye kuhimiza yanayotokana na Zaburi 19 na 119. Ingawa yametolewa miaka maelfu iliyopita, tutaona kwamba mashauri hayo ni yenye mafaa kwetu leo.
Hotuba ya watu wote atakayoitoa mwangalizi wa wilaya ni yenye kichwa “Ogopeni Mungu na Shikeni Amri Zake.” (à vérifier) (Mhu. 12:13) Katika hotuba yake ya mwisho, mwangalizi wa mzunguko ataonyesha vijana kwamba wanaweza kupata faida zote za maisha yao tangu sasa na kuwa na tumaini katika wakati ujao wa milele. Kwa kumaliza kusanyiko, mwangalizi wa wilaya atataja faida nyingi zinazopatikana kwa kuishi kulingana na “sheria ya kifalme” ya upendo. (Yk. 2:8) Basi, tusikose kusanyiko hilo!