Programu Ya Kusanyiko Lipya La Mzunguko
1 Kuanzia Septemba, kichwa cha habari cha makusanyiko ya mzunguko kitakuwa “Tusikilize na Tujifunze Kutumikisha Neno la Mungu.” Kichwa hicho chenye kutegemea Kumbukumbu 31:12, 13 kinafaa vizuri sana kwa programu, ambayo inakazia mafundisho tunayopaswa kujifunza na kutumikisha.
2 Hata ikiwa watu walio wengi leo wanasikiliza kwa makini matamko ya uongo yanayoongozwa vibaya na roho waovu, ni jambo la muhimu kwamba kila mmoja wetu asikilize Neno la Mungu na kujifunza kulitumikisha. (Lk. 11:28; 1 Tim. 4:1) Ni pamoja na mradi huo kwamba habari mbalimbali za kusanyiko la mzunguko zilitayarishwa kwa namna ya kuwatia moyo na kuwasaidia wahubiri, familia, wazee na mapainia. Siku ya Posho kutatolewa mfululizo wa hotuba katika sehemu nne yenye kichwa cha habari “Tuyashinde Matatizo Yetu kwa Kusikiliza kwa Makini Neno la Mungu.” Na Siku ya Yenga asubuhi, nyingine yenye kichwa “Maandiko Yanatia Nidhamu Katika Haki.” Kwa ujumla programu itakuwa na vitia-moyo vya kiroho ambavyo wewe na familia yako hampaswi kukosa.
3 Siku ya Posho na Siku ya Yenga yatatolewa, yakikaziwa na maonyesho, madokezo yenye kutenda kazi kwa ajili ya mahubiri. Huko utasikia pia mahojiano na mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo na yenye kuelimisha. Hivyo, kwa kuwako na kwa kusikiliza pamoja na kusudi la kutumikisha yale unayojifunza, utakuwa mwenye uwezo wa kutii amri za Neno la Mungu.
4 Ubatizo wa wale waliojiweka wakfu hivi karibuni kwa Mungu utakuwa wakati wa muhimu wa kusanyiko la mzunguko. Wale wanaotaka kubatizwa wangepaswa kusema juu ya nia yao ya kubatizwa kwa mwangalizi-msimamizi, kusudi achukua mipango ili kwamba wazee wazungumze nao.
5 Hotuba ya watu wote ya mfululizo huo wa makusanyiko itakuwa yenye kichwa “Kwa Nini Kujiacha Kuongozwa na Biblia?” Alika watu wanaoonyesha kupendezwa. Kwa kutazamia vitia-moyo na msaada ambao wewe na familia yako mtapata huko, jitayarisheni kuhudhuria kwenye vipindi vyote.