Programu Ya Kusanyiko La Mzungumko 1995-1996
1 Programu ya kusanyiko la mzunguko iliyoanza mnamo Septemba 1995 ina kichwa: “Kesheni, Simameni Imara, Mkawe Hodari.” Hayo ni maneno ya kutia moyo ya mtume Paulo kwa Wakristo wa karne ya kwanza, yanayoripotiwa katika 1 Wakorintho 16:13.
2 Kwa wale ambao bado hawajalihudhuria, kusanyiko litaonyesha kwanza kwamba tunahitaji sikuzote kujichunguza kiroho. Ili kuazimia kubaki imara thabiti kwa kusudi la kufanya yaliyo haki katika “siku [hizi] za mwisho”, ni jambo la lazima tuchunguze kwa unyofu wote uhusiano wetu pamoja na Yehova na pamoja na tengenezo lake. (2 Tim. 3:1) Tutakumbushwa kwamba Yehova anathamini jitihada zetu. Tunahitaji kufundishwa kuonyesha zaidi sifa za Kikristo na kulinda mwenendo ulio kielelezo kizuri.
3 Mkazo utawekwa pia juu ya umaana wa kushiriki kwa bidii katika kazi inayohusu kufanya wanafunzi, huku tukifikiria kufanya maendeleo ya kiroho na kuchukua madaraka. Madokezo yenye kutenda kazi yanayoonyesha jinsi, tukiwa mtu mmoja-mmoja na katika familia, tunaweza kufuata programu ya kawaida ya mlo wa kiroho yatatolewa katika hotuba mbalimbali, maonyesho na mazungumzo.
4 Siku ya Posho, wale wanaotimiza matakwa yanayoombwa ili kubatizwa wataweza kufanya tangazo la peupe la wakfu wao kwa Yehova kwa kubatizwa. Kwa upande mwingine, sote tutataka kuwapo Siku ya Yenga ili kusikiliza hotuba ya watu wote yenye kichwa: “Wewe Una Msimamo Gani Pamoja na Mungu?”
5 Programu itamalizika kwa vitia-moyo vya kubaki imara katika imani, huku tukishughulikiana katika roho ya upendo na amani. Kusanyiko la mzunguko ni mojawapo ya nafasi za pekee ambazo Yehova anatutolea za sisi ‘kuhimizana katika upendo na kazi nzuri.’ (Ebr. 10:24, 25) Tufanye mipango ili tuwepo siku hizo mbili.