Mikutano Ya Utumishi Ya Januari
Juma Toka Januari 1
Wimbo 194
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yafaayo ya Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 17: “Fululizeni Kulinda.” Kwa maulizo ya majibu.
Dak. 18: “Tutumie Broshua Mbalimbali Katika Mahubiri.” Mazungumzo juu ya utoaji mbalimbali uliodokezwa. Toa maelezo mafupi juu ya sehemu zenye kupendeza za broshua. Maonyesho mafupi mawili au matatu yanayoonyesha jinsi ya kuzitolea.
Wimbo 213 na sala ya mwisho.
Juma Toka Januari 8
Wimbo 110
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Hali ya akaunti.
Dak. 10: “Je! Vikumbusha vya Yehova Vyatuamsha Kiroho?” Kwa maulizo na majibu.
Dak. 20: Je! Wewe ni Tayari Kupambana na Tatizo la Kiganga Ambalo Lingeijaribu Imani Yako? Hotuba yenye shauku inayotolewa na mzee mwenye ujuzi. Kwa kutumia mawazo ya mafungu 1 mpaka 3 ya nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 1994, saidia wasikilizaji kutambua thamani yenye kulinda ya hati “Attestation”. Fanyisha ugawaji wa kadi nyipya kwa wahubiri wenye kubatizwa kwa kutoa mchango mdogo, kisha chunguza barua ya Septemba 15, 1995 iliyo na maagizo juu ya namna ya kuzijaza. Ambia ndugu KUTOJAZA kadi hizo jioni hiyo lakini kwenda nazo nyumbani kwao, kuchunguza ulizo kupitia sala, kisha kuzijaza. Lakini HAWATATIA SAHIHI kadi hizo wakati ule. Watazileta zikiwa zenye kujazwa wakati wa Funzo la Kitabu lijalo ambako wazee watazisainisha, watazishuhudisha na mashahidi na kutia hati tarehe. Kiongozi wa Funzo la Kitabu atatumia orodha ya karibuni zaidi ya majina ya wahubiri wote ili kuwa hakika kwamba hakuna mtu katika kikundi chake aliyesahauliwa. (Wazazi wenye kubatizwa wanaweza kusaidiwa kujaza Kadi za Utambulishi za watoto wao.) Wale watakaokosa Funzo la Kitabu hilo wataweza kupata sikuzote msaada wa viongozi vya Funzo la Kitabu na wazee wakati wa mkutano wa utumishi ufuatao, mpaka pale wahubiri wote wenye kubatizwa wataweza kujaza na kutia sahihi vizuri kadi zao. Wazee watafanya orodha ya wale wasio kuwapo na watajaribu kukamilisha hati zote mara tu iwezekanavyo.
Wimbo 154 na sala ya mwisho.
Juma Toka Januari 15
Wimbo 192
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 20: “Turudi Kumwona Kila Mtu Aliyekubali Broshua.” Ndugu anayegawiwa sehemu hii ya mkutano anazungumza pamoja na wahubiri watatu juu ya ulazima wa kurudilia wote wale walioonyesha kupendezwa au kukubali vichapo. Wanachunguza utoaji mbalimbali unaopendekezwa na wanajizoeza pamoja ili kuutumia.
Dak. 15: Tuongoze Funzo la Biblia Nyumbani. Hotuba inayotolewa na mzee anayeongoza mafunzo ya Biblia yenye kuzaa matunda. Tia wahubiri moyo kufanya bidii zaidi ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Rudilia madokezo fulani ya kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, kurasa 89-91. Unaweza kueleza kwa kifupi mambo fulani yaliyoonwa yaliyotukia katika kutaniko.
Wimbo 164 na sala ya mwisho.
Juma Toka Januari 22
Wimbo 126
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Chunguza kisanduku “Programu ya Kusanyiko la Mzunguko 1995-1996.”
Dak. 15: Tutokeze Nafasi za Kutoa Ushahidi. Wengi kati yetu husafiri ili kwenda kusanyikoni au mapumzikoni, jambo linalotutolea nafasi bora za kutoa ushahidi kwa namna ya vivihivi. Kwa msingi wa kitabu Kiongozi cha Shule, kurasa 80-82, mafungu 11-16, sema jinsi inavyowezekana kuanzisha mazungumzo na mtu tusiyejua. Onyesha kwamba kujitayarisha kunawezesha kupata matokeo bora. Maonyesho matatu mafupi yakionyesha wahubiri watatu tofauti, mmoja akianzisha mazungumzo pamoja na mfanya-kazi wa bomba la mafuta ya motokaa kwenye stesheni (au msaidizi-dreva), mwingine pamoja na msafiri katika usafirishaji wa watu wote na wa tatu pamoja na mtu anayengoja kwenye dirisha la hazina ya duka kubwa. Kumbusha wahubiri kwamba ni jambo la maana kuandika juu ya wale walioonyesha kupendezwa na kufanya programu ili mtu fulani awatembelee wakati ujao.
Dak. 20: Majirani Watafiri Nini? Hotuba na onyesho kutokana na Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1974, kurasa 425-7 (Kifaransa). Hotuba inafasiria kwa nini majirani zetu wasio Mashahidi wanajaribu mara nyingi kuwa na uvutano juu yetu. (Chunguza ukurasa 425 na fungu la kwanza la ukurasa 426.) Kisha onyesho moja linaonyesha wenzi wa ndoa wenye ujuzi wakizungumza pamoja na familia moja yenye kupendezwa hivi karibuni na kweli na ambayo majirani wanapinga funzo layo la Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova wanajaribu kuogopesha. (Kuchunguza mawazo makuu yanayopatikana katika sehemu inayobaki ya makala hiyo.) Kazia sababu ambazo kwa nini familia hiyo yenye kupendezwa karibuni haipaswi kuvunjika moyo au kuacha.
Wimbo 169 na sala ya mwisho.
Juma Toka Januari 29
Wimbo 136
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Tuwe Wenye Kujenga.” Mazungumzo na hotuba inayotolewa na mzee.
Dak. 20: Vichapo Tutakavyotolea Mnamo Februari. Kumbusha ni broshua gani za kurasa 32 ambazo zaweza kutumiwa. Alika wahubiri fulani waeleze mambo yaliyoonwa yaliyotukia mnamo Januari wakati wa kutolea broshua. Onyesho: Mhubiri mmoja anaanzisha funzo la Biblia kwa kutumia broshua Je! Kweli Mungu Anatujali?; anauliza ulizo linalotokezwa katika fungu la 1 la sehemu ya 1; anauliza msikilizaji yale anayofikiri juu ya mafungu 2-4; anasema kwamba broshua inaonyesha kwamba Mungu anatujali na kwamba itawezekana kuishi pasipo mateso katika ulimwengu mpya; anapendekeza kurudi ili kuzungumza kwa uzito zaidi.
Wimbo 179 na sala ya mwisho.