Turudi Kumwona Kila Mtu Aliyekubali Broshua
1 Mtume Paulo aliwapongeza Wafilipi kwa sababu ‘waliamsha fikira zao kwa ajili yake.’ (Flp. 4:10) Ikiwa tunafuata kielelezo chao katika mahubiri, ‘tutaamsha fikira zetu’ kwa ajili ya wale tunaohubiri na tutajisikia wenye kuchochewa kuwarudilia tena.
2 Ikiwa tuliacha broshua “Serikali Itakayoleta Paradiso,” tungeweza kwa mfano kusema hivi:
◼ “Nilifikiria mazungumzo tuliyokuwa nayo siku ile, na maandiko mawili ya Biblia yalinijia akilini. Ningependa kukuonyesha yenyewe. Unakumbuka labda: Tulizungumza juu ya utawala ambao Mungu angeendesha duniani. Katika Biblia, Yehova Mungu anaahidi kwamba hilo litatimia. [Tusome Danieli 2:44.] Je! unafikiri kwamba hilo lawezekana? [Tuache mtu ajibu.] Sikiliza yale Mungu anasema kuhusu uwezo wake wa kutimiza ahadi zake. [Tusome Isaya 55:11.] Je! andiko hilo halingepaswa kututia moyo kuweka tumaini letu katika Ufalme wa Mungu? Lakini sasa, ni wakati gani Mungu atakapotimiza ahadi zake?” Tuseme kwamba tutajibu ulizo hilo wakati wa ziara yetu ijayo.
3 Ikiwa tunamtembelea mtu aliyekubali broshua “Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa,” tungeweza kujaribu utangulizi huu:
◼ “Kwa kuwa siku ile tulizungumza juu ya kifo cha mpendwa, nilifanya jitihada ya pekee ili kurudi kukuona tena.” Tuonyeshe picha ya ukurasa 30 kwa kusema: “Unakumbuka tamasha hii ya furaha, ya watu wakifufuliwa na kuunganishwa na wapendwa wao? Nilikuuliza swali ikiwa ulijua ni wapi jambo hili litatendeka, mbinguni au duniani. Labda ulipata, kwenye ukurasa 26 wa broshua hii, jibu la Biblia.” Tuzungumzie mambo makuu ya mafungu 3 mpaka 5, na tuonyeshe Yohana 5:21, 28, 29. Wakati ukituruhusu, tusome mojawapo ya maandiko yanayotajwa kwenye ukurasa 26.
4 Je! tumeanza kujifunza broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”? Wakati wa ziara ijayo, tungeweza kufanya hivi:
◼ Turejee tena kwenye ukurasa 30 na tutokeze ulizo hili: “Biblia ni kitabu chenye kutokeza katika njia gani?” Tufungue broshua kwenye kurasa 3 na 4 na turudilie tena mafungu 1 mpaka 4, na pia picha ya jalada. Tusome andiko moja au mawili yanayotajwa katika kielezi-chini cha fungu la 4. Tuseme kwamba Biblia ndicho kitabu pekee ambacho hutoa tumaini ajabu kama hilo. Tuchukue mipango kwa ajili ya ziara ifuatayo. Baada ya ziara ya tatu, ikiwa tunafikiri kwamba funzo litaendelea, tutaweza kuliripoti kama funzo lipya.
5 Tungeweza kurudilia mazungumzo juu ya broshua “Jina la Mungu Litakaloendelea Milele” kwa njia hii:
◼ “Wakati uliopita, nilikuonyesha jina la Mungu katika Biblia. Kujua jina la Yehova na kulitumia ni sehemu muhimu ya ibada yetu.” Tufungue broshua kwenye ukurasa 31, tuchunguze mawazo ya maana ya mafungu manne ya mwisho-mwisho, na tumsomee mwenye nyumba Yohana 17:3 na Mika 4:5. Tumwambie kwamba tunamtolea funzo la Biblia litakalomwezesha kujifunza kwamba jina la Mungu litatakaswa na kwamba wanadamu watapata shangwe ya kuishi kwenye dunia iliyo paradiso.
6 Tuamshe hivyo fikira zetu kwa ajili ya wale tuliokutana nao. Tunapaswa kuwatembelea kwa uvumilivu na kujitayarisha ili kuwatolea mawazo yenye kutia moyo. Hivyo, tutakuwa hakika Wakristo ‘wazaao matunda’ katika kazi ya kufanya wanafunzi wapya.—Mt. 13:23.