Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/96 uku. 1
  • Je! Vikumbusha Vya Yehova Vyatuamsha Kiroho?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je! Vikumbusha Vya Yehova Vyatuamsha Kiroho?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Vikumbusho vya Yehova Ni Vyenye Kutegemeka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Je! hatukusikia hilo hapo mbele?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Furahia Vikumbusho Vya Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Je, Ninahubiri Vyakutosha?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 1/96 uku. 1

Je! Vikumbusha Vya Yehova Vyatuamsha Kiroho?

1 Katika kumsifu Yehova, Mtunga-Zaburi mmoja alisema: ‘Vikumbusha vyako ndivyo nihangaikiavyo.’ (Zab. 119:​99, NW) Neno la Kiebrania la “vikumbusha” hutoa wazo la kwamba Yehova hutukumbusha yanayosemwa na sheria zake, kanuni zake, masharti yake na amri zake. Tukiziitikia, zitatuamsha kiroho na kutufanya tuwe na furaha.​—Zab. 119:2.

2 Tukiwa kati ya watu wa Yehova, tunapokea kwa ukawaida mashauri; tumekwisha tayari kusikia mengi yayo. Ingawa twathamini vitia moyo kama hivyo, tunayo maelekeo ya kuvisahau. (Yk. 1:25) Yehova hututolea kwa uvumilivu vikumbusha vyenye kujaa upendo. Mtume Petro alitujulisha mojawapo wavyo katika kusudi la ‘kuamsha uwezo wetu mwangavu wa kufikiri kwamba tukumbuke amri za Bwana.’​—2 Pet. 3:​1, 2.

3 Twakumbushwa kwa kurudia-rudia umaana wa kujifunza kibinafsi na kuhudhuria mikutano. Sababu ni kwamba utendaji huo mbalimbali ni wa muhimu kwa hali yetu ya kiroho.​—1 Tim. 4:​15; Ebr. 10:​24, 25.

4 Kwa wengine, tatizo kubwa zaidi ni kutimiza wajibu wao wa Kikristo wa kuhubiri. Hilo lahitaji jitihada, azimio na uvumilivu. Ingawa hilo lataka mengi kwa upande wetu, jambo la kuwa ‘miguu yetu ikiwa imevishwa vifaa vya habari njema’ litatusaidia ‘kusimama imara.’​—Efe. 6:​14, 15.

5 Utumishi wetu haupaswi kuchochewa tu na kujua kwetu kiakili matakwa ya Yehova. Mtume Paulo atukumbusha kwamba ni moyo unaotoa uchocheo tunaohitaji ili “kukiri hata kupata wokovu.” (Rum. 10:10) Ikiwa tunayo imani yenye nguvu na kwamba moyo wetu unaelekea vikumbusha vya Yehova, tutasukumwa kusema na kulisifu jina lake.​—Zab. 119:36; Mt. 12:34.

6 Tunapotumika kwa bidii katika kutimiza matendo mema, tunatazamia bila shaka kupatia ndani shangwe. (Mhu. 2:10) Paulo hufafanua shangwe kuwa tunda la roho ya Yehova, na tungepaswa kuendelea kutafuta kukomaa katika kuionyesha sifa hiyo. (Gal. 5:22) Petro aliongeza kwamba “jitihada yote” itathawabishwa na huduma yenye matokeo, jambo linalotokeza shangwe.​—2 Pet. 1:​5-8.

7  Ikiwa tunakabiliwa na magumu, tukumbuke msimamo imara wa mitume, waliosema: “Hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.” (Mdo. 4:20) Twatiwa nguvu tunapokumbuka kwamba ‘kwa kufanya hivyo tutajiokoa nafsi yetu na wale watusikiao.’​—1 Tim. 4:16.

8 Hatukasiriki au kuudhika kwa sababu tunapokea mara kwa mara vikumbusha. Badala yake, twatambua kwelikweli thamani bora yavyo. (Zab. 119:129) Katika wakati huu mgumu, twashukuru kwamba Yehova anaendelea kututolea vikumbusha vinavyokusudiwa kutuamsha kiroho na kutuchochea kuwa wenye bidii kwa ajili ya matendo mema.​—2 Pet. 1:​12, 13.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine