Tuwe Wenye Kujenga
1 Tukiwa wenye kuishi ‘Nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo’, sisi sote twahitaji vitia-moyo. (2 Tim. 3:1, NW) Akitambua tayari uhitaji huo kwa wakati wake, Paulo aliangalia sana kufanya ushirika wake pamoja na ndugu zake kuwa nafasi ya ‘badilishano la vitia-moyo.’ Aliwasihi ndugu zake ‘wafuate mambo . . . ya kujengana.’ (Rum. 1:11, 12; 14:19) Jitihada hizo zilifanikiwa ‘kufanya imara nafsi za wanafunzi, na kuwatia moyo wakae katika imani.’ (Mdo. 14:22) Tunahitaji sana aina hiyo ya kitia-moyo leo.
2 Maneno yetu yanaweza kujenga wengine na, yakitumiwa vizuri, yanaweza kuwa “kama machungwa katika vyano vya fedha.” (Mit. 25:11) Kwa kushiriki katika mikutano, ‘tunatiana moyo.’ (Ebr. 10:25, NW) Ulimi wetu unatumiwa vizuri ikiwa tunaeleza mambo yaliyoonwa katika mahubiri, kupongeza wengine au kuzungumzia mambo ya kiroho. Matumizi hayo yenye kufaa ya ulimi ni ‘mema kwa ajili ya kujenga kama vile kuwezavyo kuwa na uhitaji, ili huo upate kuwagawia wasikiaji lililo la kupendeleka.’—Efe. 4:29, NW.
3 Tuzungumze Mambo Yenye Kujenga: Katika Wafilipi 4:8, Paulo alitoa mashauri yenye kutenda kazi yanayoonyesha jinsi ya kufanya matumizi yafaayo ya usemi: kutoa uangalifu wetu kwa yote yaliyo kweli na yanayostahili kuhangaikiwa kwa uzito, ya uadilifu, safi, yenye kupendeka, yanayosemwa vizuri, yenye wema-adili na yenye kustahili sifa. Tunaweza kuwa hakika kwamba yale tunayosema ni kweli na yenye kujenga ikiwa hayo hutokana na Neno la Mungu. (Yn. 17:17) Wakfu wetu kwa Mungu, yale tunayojifunza wakati wa mikutano ya kutaniko, bidii tunayofanya katika huduma na mambo mengine kama hayo yanastahili kuhangaikiwa kwa uzito. Mazungumzo kuhusu viwango na kanuni za Neno la Mungu yatatusaidia hakika ‘kutuhekimisha hata tupate wokovu.’ (2 Tim. 3:15) Tuonyeshe shukrani yetu kwa ajili ya mwenendo safi wa wale walio washiriki wa tengenezo safi la Yehova. Tusifu matendo yenye kupendeza ya fadhili ya ndugu zetu. (Yn. 13:34, 35) Kati ya mambo yenye kusemwa vizuri hutia ndani sifa zifaazo za Kikristo ambazo ni imani, shangwe, amani, na uvumilivu, sifa tunazoona kwa ndugu zetu. Kuzungumza juu ya mambo hayo yenye wema-adili na yenye kustahili sifa ni ‘mema yenye kujenga’ wengine.—Rum. 15:2.
4 Ni jambo lenye kuvunja moyo kupambana kila siku na mikazo ya ulimwengu. Ni jambo lenye kupendeza kama nini kutoyafikiria mambo yote hayo ili kuonja upendo wa kindugu! Wakati wenye thamani ambao tunapitisha pamoja ni hazina ambayo tunapaswa kuthamini. Ikiwa sikuzote sisi ni wenye kutia moyo na wenye kujenga, hakika wengine wataweza kusema juu yetu: ‘Wameniburudisha roho yangu.’—1 Kor. 16:18.