Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/08 uku. 1
  • Tutiane Moyo Tunapokuwa Katika Kazi ya Kuhubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tutiane Moyo Tunapokuwa Katika Kazi ya Kuhubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tusaidiane Vizuri Tunapohubiri Pamoja
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Saidia Yule Unayehubiri Naye
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Uendelee Kuwa na Bidii Katika Kazi ya Kuhubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Muendelee Kutiana Moyo Kila Siku
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 3/08 uku. 1

Tutiane Moyo Tunapokuwa Katika Kazi ya Kuhubiri

1 Sisi wote tunafurahia kutiwa moyo na “neno linalosemwa wakati unaofaa.” (Met. 25:11) Tunapohubiri pamoja na wengine, namna gani tunaweza kufanya mazungumzo yetu yawatie moyo?

2 Mazungumzo Yenye Kutia Moyo: Ni jambo lenye kutia moyo sana kuzungumzia mambo ya kiroho tunapohubiri pamoja na ndugu na dada zetu! (Zab. 37:30) Tunaweza kuzungumza kuhusu utoaji wetu ao kueleza mambo yenye kutia moyo ambayo tulijionea hivi karibuni katika kazi ya kuhubiri. (Mdo. 15:3) Tunaweza kuelezea wengine jambo lenye kupendeza ambalo tulipata katika usomaji wetu wa Biblia, katika magazeti mapya ao katika mikutano ya kutaniko. Tunaweza kuzungumzia mambo yaliyoelezwa katika hotuba ya watu wote ambayo tulisikiliza hivi karibuni kwenye Jumba la Ufalme.

3 Tunaweza kujisikia kuwa wenye kuvunjika moyo ikiwa msikilizaji wetu alitokeza kizuia-mazungumzo ambacho hatukuweza kushinda. Tukiisha kuachana na mtu, ni jambo lenye faida kwetu kuchukua dakika chache ili kuzungumza na mhubiri mwenzetu kuhusu jinsi ambavyo tunaweza kushinda kizuia-mazungumzo kama hicho wakati ujao, labda kwa kuchunguza kitabu Kutoa Sababu. Na ikiwa tulifurahia jambo fulani kuhusu utoaji wa mhubiri mwenzetu, tunaweza kumtia moyo kupitia neno la shukrani lenye kutoka moyoni mwetu.

4 Chukua Hatua ya Kutia Wengine Moyo: Je, kuna watu fulani katika kikundi chetu cha funzo la kitabu ambao hatukuhubiri nao hivi karibuni? Kuwaalika watusindikize katika mahubiri kunaweza kutokeza “ubadilishanaji wa kitia-moyo.” (Rom. 1:12) Mapainia wasaidizi na wa kawaida wanafurahi sana wanapopata mtu wa kutumika nao, zaidi sana wakati wa asubuhi mapema na magaribi, wakati ambapo ni wahubiri wachache tu wanaoenda katika kazi ya kuhubiri. Tunaweza kuwaunga mkono mapainia kwa kuwa tayari kuhubiri pamoja nao. Je, kuna mhubiri aliye mzaifu kimwili ambaye afya yake inazuia yale ambayo anaweza kufanya katika utumishi? Kufanya mpango ili mhubiri huyo atusindikize, labda kwenye funzo la Biblia, kunaweza kuwa jambo lenye kusaidia.—Met. 27:17.

5 Mara nyingi, tunaposhukuru wengine na kuwaambia maneno yenye kuonyesha kwamba tunapendezwa nao, hilo linawatia moyo hata katika mambo madogo. Tukumbuke jambo hilo tunapohubiri pamoja na wengine, kwa kuwa tunataka ‘kuendelea . . . kujengana.’—1 The. 5:11.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine