Saidia Yule Unayehubiri Naye
1. Tunapohubiri na wengine, namna gani tunaweza kumuiga mutume Paulo?
1 Mutume Paulo aliona wakati aliopitisha na wahubiri wenzake kuwa nafasi za “ubadilishanaji wa kitia moyo.” (Rom. 1:12) Unapohubiri na ndugu ao dada, je, unatumia nafasi hiyo ili kumutia moyo na kumusaidia? Kuliko kunyamaza, ni muzuri umuelezee namna ulifikia kuwa na ufundi katika mahubiri.
2. Sababu gani ni lazima tumusaidie yule tunayehubiri naye ili ashinde woga, na namna gani tunaweza kumusaidia?
2 Umusaidie Ashinde Woga: Wahubiri wengi wana woga ao wasiwasi; hilo linaweza kuonekana kupitia sura ao sauti yao. Tukiwapongeza kwa moyo wote, tunaweza kuwasaidia washinde tatizo hilo. Ni njia gani zingine tunazoweza kutumia ili kuwasaidia? Mwangalizi mumoja mwenye kusafiri anamuambia waziwazi ndugu ao dada anayehubiri naye kwamba yeye pia anaogopa wakati fulani, na anasali mara nyingi ili Yehova amusaidie. Ndugu mwengine alisema kwamba anazoea kuonyesha sura ya kicheko ili kushinda woga. Anasema tena kwamba, wakati mwingine ni lazima kusali ili Yehova atusaidie tuonyeshe sura ya kicheko. Unazoea kufanya nini ili kushinda woga katika mahubiri? Umuelezee yule unayehubiri naye.
3. Tunaweza kumuelezea mambo gani yule tunayehubiri naye ili kumusaidia awe na ufundi zaidi?
3 Umuonyeshe Njia Unazotumia: Unajua maneno ao maulizo mepesi ya utangulizi, pengine yanayohusu tukio ao hali fulani ya kwenu, ambayo yanakusaidia kuanzisha mazungumuzo kwa ufundi? Huduma Yetu ya Ufalme ina mapendekezo kuhusu namna ya kuanzisha mazungumuzo; je, una mawazo fulani ambayo unazoea kuongeza kwenye mapendekezo ambayo yanakusaidia upate matokeo mazuri? Umuelezee yule unayehubiri naye. (Met. 27:17) Munapojielekeza kwenye funzo fulani, unaweza kumuelezea yule unayehubiri naye kusudi lako kuelekea funzo hilo na namna umepanga kutimiza kusudi hilo. Kisha kuongoza funzo, unaweza kumuelezea sababu gani ulikazia jambo fulani ao andiko fulani, ao sababu gani ulitumia njia fulani ya kufundisha kulingana na mahitaji ya mwanafunzi.
4. Sababu gani tuwasaidie wahubiri wenzetu?
4 Wahubiri wa wakati wa mitume hawakuwasaidia tu watu wengine. Waliona pia kwamba ni jambo la maana kutia moyo na kujenga waabudu wenzao. (Mdo. 11:23; 15:32) Mutume Paulo alimuzoeza kijana Timotheo na kisha alimutia moyo awaelezee wengine mambo aliyojifunza. (2 Tim. 2:2) Ikiwa tunakumbuka kuwatendea waabudu wenzetu mema tunapokuwa katika mahubiri, tunaongeza furaha yao na tunawasaidia kuwa na ufundi, na pia, tunamufurahisha Baba yetu wa mbinguni.—Ebr. 13:15, 16.