Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/05 uku. 7
  • Tuendelee Kujengana

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuendelee Kujengana
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Fanya Mema na Ushiriki Pamoja na Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Tutiane Moyo Tunapokuwa Katika Kazi ya Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Tuendelee “Kujengana”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Msaada Unaopatikana kwa Utayari
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 9/05 uku. 7

Tuendelee Kujengana

1 Mtume Paulo alifanya yote aliyoweza ili kuimarisha waamini wenzake. (Mdo. 14:19-22) Sisi pia, tunahangaika wakati ndugu zetu wanapambana na hali ngumu, na tunataka kuwasaidia. Biblia inaonyesha kwamba sote, na si wazee tu, tunapaswa kupendezwa na wengine. (Rom. 15:1, 2) Fikiria mambo mawili ambayo katika hayo tunaweza kutumia onyo hili lenye upendo: “Endeleeni kufarijiana na kujengana.”—1 Tes. 5:11.

2 Kutambua Mahitaji ya Wengine: Neno la Mungu linaripoti kwamba Dorkasi “alizidi katika matendo mema na zawadi za rehema.” (Mdo. 9:36, 39) Alitambua wale waliokuwa katika uhitaji na alifanya yote aliyoweza ili kuwasaidia. Ni mfano mzuri kabisa kwetu. Unaweza kupata habari kwamba mtu mzee-mzee anahitaji msaada ili kwenda kwenye mkutano. Au kunaweza kuwa painia ambaye hana mtu yeyote wa kufanya kazi pamoja naye siku ya juma kisha mchana-kati. Ukitambua kwamba kuna uhitaji kama huo na ukitoa msaada unaofaa, fikiri jinsi jambo hilo linavyoweza kumtia moyo mtu yule aliye katika uhitaji!

3 Mazungumzo ya Kiroho: Tunaweza pia kuwajenga wengine kupitia usemi wetu. (Efe. 4:29) Mzee mmoja mwenye uzoefu alitambua: “Ukipenda kuwa mtu mwenye kutia moyo, zungumzia mambo ya kiroho. Ili kuanzisha mazungumzo yenye kujenga, unaweza kutumia ulizo rahisi, kama vile, ‘Ulijifunza kweli namna gani?’” Katika kutaniko onyesha vijana kwamba unapendezwa kweli nao. Onyesha pia kwamba unapendezwa na wale wanaovunjika moyo na wale wanaosikia haya. (Met. 12:25) Usiruhusu kuzungumzia viburudisho vya ulimwengu kukuzuie kufanya mazungumzo ya kiroho pamoja na waamini wenzako.—Rom. 1:11, 12.

4 Kwa hiyo, ni mambo gani unayoweza kusema ili kujenga wengine? Katika usomaji wako wa Biblia na funzo lako la kibinafsi, je, ulipata hivi karibuni kanuni ambayo imeimarisha uthamini wako kwa Yehova? Je, ulichochewa na jambo fulani ulilosikia katika hotuba ya watu wote au kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi? Au je, moyo wako uliguswa na jambo lililoonwa lenye kutia imani nguvu? Ikiwa unathamini mambo hayo ya kiroho, sikuzote utakuwa na jambo la kutia moyo la kushiriki na wengine.—Met. 2:1; Luka 6:45.

5 Kwa kutoa msaada unaofaa na kufanya matumizi yenye hekima ya ulimi wetu, na tuendelee kujengana.—Met. 12:18.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine