Tutumie Broshua Mbalimbali Katika Mahubiri
1 Wanadamu wenzetu wanapendezwa na kila aina ya habari. Tutakapokwenda kuhubiri mnamo Januari, tuchukue broshua nyingi ili kutumia ile itakayowapendeza wakaaji wa eneo letu. Tujaribu hivyo moja kati ya utoaji huu mbalimbali:
2 Kwa toleo la broshua “Serikali Itakayoleta Paradiso,” tuulize:
◼ “Kwa maoni yako, ulimwengu ungefanana namna gani ikiwa Mungu peke yake ndiye aliyekuwa kiongozi? [Tuache mtu ajibu.] Kwamba Mungu achukue mamlaka duniani, hilo ndilo hasa tunaloomba tunapotamka Baba Yetu, sala ambayo Yesu Kristo alitufundisha. [Tufungue broshua kwenye ukurasa wa 3 na tusome fungu la 1, linalotaja Mathayo 6:10.] Ikiwa unatamani kuishi katika ulimwengu kama huu, ungepaswa kusoma broshua hii.” Kisha tuitolee.
3 Dokezo ili kutolea broshua “Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa”:
◼ “Je! unaamini kwamba siku fulani hakuna mtu atakayelia mpendwa aliyechukuliwa na kifo? [Tuache mtu ajibu.] Broshua hii iliyoandikwa vizuri imefariji mamilioni ya watu, kwani inafasiria kwamba siku hiyo ni karibu na kwamba ni ahadi hakika ya Biblia. [Tufungue broshua kwenye ukurasa wa 5 na tusome fungu la 5, hasa 1 Wakorintho 15:21, 22. Kisha tuonyeshe picha ya ukurasa wa 30.] Hapa mchoraji alionyesha vizuri shangwe ambayo tutaweza kuwa nayo kwa kuwakaribisha wapendwa wetu waliokufa watakapofufuliwa. Lakini tamasha hii yenye furaha itatendeka wapi? Utavumbua jibu la Biblia katika broshua hii.” Ikiwa mtu anakubali toleo letu, tuongeze: “Ningependa kurudi tena ili kuzungumzia kwa undani habari hii pamoja nawe.”
4 Labda tunapenda kutolea broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” kwa kutolea moja kwa moja funzo la Biblia:
◼ “Watu wengi wanajiuliza maulizo juu ya Biblia. Na huenda tayari umekwisha kujiuliza mojawapo yayo. [Tufungue broshua kwenye ukurasa wa 30.] Wengi wanasimamia kwa hili la mwisho: ‘Jinsi gani unaweza kujitayarisha kuishi milele katika Paradiso?’ ” Ikiwa tunatoa maelezo ya mafungu 57 na 58 kwenye kurasa 29 na 30 na tunasoma Ufunuo 21:3, 4, tunatia hivyo msingi wa funzo la Biblia. Tumalizie kwa kutolea broshua na kupanga ziara ya kurudia ili kuchunguza maulizo mengine.
5 Au tutajaribu utoaji huu mwepesi wa broshua “Jina la Mungu Litakaloendelea Milele”:
◼ “Mojawapo ya mambo ya kwanza kwanza niliyojifunza katika Biblia lilikuwa jina la Mungu. Je! wewe walijua? [Tuache mtu ajibu.] Ningependa kukuonyesha lenyewe. Linapatikana kwa mfano katika Zaburi 83:18. [Tusome andiko.] Broshua hii huonyesha jinsi jina la Mungu, Yehova, lipatikanavyo katika lugha nyingi tofauti. [Tuonyeshe sanduku kwenye ukurasa 8.] Ikiwa unapenda kujua zaidi juu ya Yehova na makusudi yake, soma hivyo broshua hii.” Tumtolee msikilizaji wetu broshua.
6 Tukiwa na broshua hizo bora mbalimbali, hakika tumetayarishwa vema ili ‘kuwahubiri wanyenyekevu habari njema.’—Isa. 61:1.