Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/97 uku. 7
  • Programu Ya Kusanyiko La Mzunguko Lijalo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu Ya Kusanyiko La Mzunguko Lijalo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Programu Ya Kusanyiko Lipya La Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Programu Ya Kusanyiko La Mzunguko Lijalo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Programu mpya ya mkusanyiko wa mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • ‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 8/97 uku. 7

Programu Ya Kusanyiko La Mzunguko Lijalo

“Tulinde Kila Mara Akilini Siku ya Yehova,” hicho ndicho kichwa cha habari cha kusanyiko la mzunguko lijalo ambalo kipindi kitaanza mnamo Septemba. (2 Pt. 3:12) Lilitayarishwa ili kutusukuma kutenda. Hivi karibuni, hukumu za Yehova zitaanguka juu ya wakaaji wa dunia. Nani ataokoka kwa “siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote”? Ni peke yao wale wanaobaki macho kiroho na walio na maisha tajiri katika “matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji-kimungu.”​—Ufu. 16:14; 2 Pt. 3:11.

Ili kuokoka katika siku ya Yehova, ni jambo la muhimu kubatizwa. (1 Pt. 3:21) Wahubiri wanaotamani kufanya hivyo kwenye kusanyiko hilo wangepaswa kumjulisha mwangalizi-msimamizi, ambaye atachukua mipango ya lazima.

Hotuba mfululizo iliyo na sehemu nne, yenye kichwa “Aina ya Watu Tunapaswa Kuwa,” itaonyesha waziwazi jinsi ya kutenda ili kulinda kila mara akilini kuwapo kwa siku ya Yehova. Hotuba ya watu wote, ambayo itakuwa na kichwa cha habari “Tenda Kihekima Siku ya Yehova Inapokaribia,” itafasiria kile kinachomaanisha ‘kutafuta Yehova, haki na unyenyekevu’ ili kuwa kati ya waokokaji.​—Zef. 2:3.

Kusanyiko la mzunguko litamalizika kwa hotuba mbili zenye kutia moyo zitakazotolewa na waangalizi wasafiri na zenye vichwa vya habari “Je! Maisha Yako Yanategemea Ukweli?” na “Tupange Mambo Yetu Tukilinda Akilini Siku ya Yehova.” Hotuba hizo zitatoa nafasi ya kufikiri juu ya maisha yetu na kufanya mabadiliko yatakayohitajiwa. Unabii mbalimbali wa Biblia na matukio ya ulimwengu yanaonyesha wazi kwamba siku ya Yehova ni karibu. Programu ya kusanyiko hilo itatuchochea ‘kutunza akili zetu, na kuwa wenye kulinda.’ (1 Pt. 5:8) Tuchukue mipango kamili ili kuudhuria.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine