Programu mpya ya mkusanyiko wa mzunguko
Ni faida gani zenye kutumika unazozipata sasa kwa kutembea na Yehova? Unawezaje kuzuia kishawishi cha kuruhusu ufuatiaji usio wa kitheokrasi usonge faida za Ufalme kutoka kwenye nafasi ya kwanza katika maisha yako? (Mt. 6:33) Je! unaona vigumu kupambanua kati ya lililo jema na lililo baya katika ulimwengu unaofanya lililo baya lionekane kuwa jema? (Ebr. 5:14) Mambo hayo yatazungumziwa kwenye mkusanyiko wa mzunguko “Faidikeni Sasa kwa Kutembea Katika Njia za Mungu,” kuanzia Septemba 1999.—Zab. 128:1.
Jambo jipya Siku ya Posho ya mkusanyiko huo wa mzunguko litakuwa kule kuonyesha Mkutano wa Utumishi wa kielelezo. Mwangalizi wenu wa mzunguko atajulisha makutaniko kuhusu mambo yanayopangwa kusudi wote waweze kuja wakiwa wamejitayarisha ili kufurahia programu kikamili.
Sehemu yenye kichwa “Mapainia—Fulizeni Kuangalia Jinsi Mnavyotembea” itatuonyesha jinsi ya kuonyesha hekima na usawaziko wa akili ili kununua wakati unaofaa kwa ajili ya huduma ya painia. (Efe. 5:15-17) Habari “Jihadharini na Njia Zinazoonekana Tu Kuwa Sawa” itatufundisha jinsi ya kuwa hakika na lile linalokubaliwa na Mungu katika pande zote za maisha. Hotuba yenye kichwa “Jinsi Unabii Uliotimizwa Unavyokuwa na Uvutano juu Yetu” itasaidia kujaza akili zetu na mioyo yetu na upendo kwa Neno la Mungu. Hotuba ya watu wote yenye kichwa “Njia za Mungu Ni Zenye Mafaa!” itatia mkazo juu ya faida zenye kutumika zinazopatikana sasa kwa kuendelea kutembea kulingana na matakwa ya Yehova yenye uadilifu.
Je! unatamani kuonyesha hadharani kupitia ubatizo wa maji kwamba unataka kutembea katika njia za Mungu, ukiwa mmoja wa watumishi wake walio wakfu? Ikiwa ni hivyo, zungumza na mwangalizi msimamizi kusudi mipango inayohitajiwa ichukuliwe.
Fanya liwe azimio lako kutokosa mkusanyiko huo wa mzunguko, unaopangwa kwa wakati wenye kufaa. Uweko muda wa programu hiyo yote ya siku mbili, kwa kuwa “heri [mwenye furaha, NW] ni kila mutu anayeogopa BWANA [Yehova, NW], anayetembea katika njia zake.”—Zab. 128:1.