Njia Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 12
“Ni kweli kwamba kila mutu ana lazima ya marafiki, sivyo? Ungetaka rafiki yako awe na sifa gani? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo gazeti hili linasema kuhusu sababu ya kuchagua marafiki wetu kwa uangalifu.” Umwonyeshe mutu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 12, na musome na kuzungumuzia habari ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16. Soma andiko moja hivi kati ya maandiko yanayotajwa. Umutolee mutu magazeti, na ufanye mupango wa kumurudilia ili kuzungumuzia jibu la ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/12/11
“Je, umekwisha kujiuliza kwa nini kuna misiba mingi siku zetu? [Acha mutu ajibu.] Jambo la ajabu ni kwamba Biblia ilitabiri kwamba kutakuwa misiba mingi siku zetu. [Soma Mathayo 24:7, 8.] Gazeti hili linajibu maulizo haya: Kwa nini kuna misiba mingi leo? Je, ni malipizi kutoka kwa Mungu? Linaonyesha pia sababu zinazotufanya tuamini kwamba Mungu atamaliza misiba yote hivi karibuni.”
Amkeni! Mwezi wa 12
Soma 2 Timotheo 3:16. Kisha sema hivi: “Watu fulani wanakubali kwamba Biblia iliongozwa na roho ya Mungu, wengine hawakubali hivyo. Wewe unafikiri nini? [Acha mutu ajibu.] Hata ikiwa watu wana maoni tofauti kuhusu wazo hilo, kwa kawaida watu wanakubali kwamba hakuna kitabu kingine kilichoshambuliwa sana kama Biblia. Gazeti hili linaeleza jinsi watu walivyofanya yote wawezayo ili kuiharibu Biblia na kukataza watu wasiisome. Linaeleza pia kwa nini Biblia imeshinda upinzani huo.”