Programu ya Juma Tokea Tarehe 12 Mwezi wa 12
JUMA TOKEA TAREHE 12 MWEZI WA 12
Wimbo 43 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 14 fu. 1-5, kisanduku kwenye uku. 112 (Dak. 25)
□ Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi:
Usomaji wa Biblia: Isaya 6-10 (Dak. 10)
Na. 1: Isaya 6:1-13 (Isipite dak. 4)
Na. 2: Kwa nini mungu anaruhusu muda murefu upite mbele ya kuharibu waovu?—rs uku. 291 fu. 4-6 (Dak. 5)
Na. 3: Kwa Nini Upendo Haushindwi Kamwe—1 Kor. 13:8; 1 Yoh. 4:8 (Dak. 5)
□ Mukutano wa Utumishi:
Wimbo 36
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 15: Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi ya Mwaka wa 2012. Hotuba itakayotolewa na mwangalizi wa Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi. Zungumuzia mambo yanayostahili kutiliwa mukazo katika kutaniko lenu ukitumia programu ya 2012. Zungumuzia daraka la mushauri musaidizi. Tia wote moyo wawe na bidii katika kutimiza migawo yao, kutoa maelezo kuhusu mambo makuu ya usomaji wa Biblia, na kutumia mapendekezo yanayotolewa kila juma kutoka kitabu Shule ya Huduma.
Dak. 15: “Tusiache Wakati Wetu Upite Bure.” Maulizo na majibu. Munapozungumuzia fungu la 2, uliza maulizo machache muhubiri anayepata matokeo mazuri anapohubiri wakati hakupanga kufanya hivyo. Umuombe aeleze jinsi anavyojitayarisha mbele ya wakati, na aeleze jambo fulani nzuri alilokutana nalo.
Wimbo 135 na Sala