Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 12
“Katika kipindi hiki cha mwaka, watu wengi ni wenye kufikiri juu ya Yesu. Kwa maoni yako, ni jambo gani kubwa zaidi ambalo Yesu alitimiza? [Acha mutu ajibu.] Ona kichwa cha habari hii kwenye ukurasa wa 16.” Umupatie musikilizaji Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 12, na muzungumuzie habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16, na musome andiko moja ao zaidi. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili muzungumuzie ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/12/12
“Watu wengi wanajikaza kufanya mambo mazuri katika kipindi hiki cha Noeli. Kati ya mambo haya, wewe unawaza ni jambo gani ndilo la maana zaidi kufanya? [Umuonyeshe mambo yanayotajwa kwenye ukurasa wa 3 na umuache ajibu. Kisha, ufungue habari inayozungumuzia jambo alilochagua na usome andiko la musingi la habari hiyo.] Gazeti hili linaonyesha njia mbalimbali zinazofaa za kumukumbuka Yesu katika mwaka wote, hapana tu katika kipindi cha Noeli.”
Amkeni! Mwezi wa 12
“Tunawatembelea kwa sababu tunajua watu wengi wana mahangaiko na mikazo mingi. Je, wewe pia umetambua kwamba siku hizi watu hawana tena uvumilivu kama zamani? [Acha mutu ajibu.] Watu fulani wanaamini kama tunaishi katika siku zenye mikazo mingi kama ilivyotabiriwa kwenye 2 Timotheo 3:1. [Soma] Gazeti hili linaeleza sababu gani ni hatari kukosa uvumilivu na inatoa mapendekezo kuhusu namna tunavyoweza kuonyesha uvumilivu zaidi.”