Sarafu Mbili Zenye Samani Ndogo Sana
Kutoa michango ya feza kwa ajili ya kazi ya kuhubiri duniani pote ni njia moja ya lazima ili kutegemeza kazi ya Ufalme. Je, mutu aliye maskini naye anaweza kutoa michango?
Siku moja Yesu alimuona mujane masikini akitia sarafu mbili zenye samani ndogo sana katika sanduku ya hazina ya hekalu. Kwa sababu mujane huyo alikuwa na upendo kwa Yehova alitoa ‘kutokana na uhitaji wake, vyote alivyokuwa navyo, riziki yake yote.’ (Mk. 12:41-44) Kwa kuwa Yesu alisemea jambo hilo, hilo linaonyesha kama muchango wa mujane huyo ulikuwa wenye samani machoni pa Mungu. Vilevile, Wakristo wa wakati wa mitume hawakuwaza kama kutoa michango ya feza ili kutegemeza kazi ya kuhubiri ni pendeleo la Wakristo walio matajiri tu. Mutume Paulo alizungumuzia mufano wa Wakristo wa Makedonia, ambao, ijapokuwa walikuwa maskini sana ‘waliendelea kuomba kwa kusihi sana wapate pendeleo la kutoa kwa fazili.’—2 Kor. 8:1-4.
Kwa hiyo, hata ikiwa tunaweza kutoa muchango wa ‘sarafu mbili zenye samani ndogo sana,’ tunapaswa kukumbuka kwamba michango midogo-midogo mingi inapotiwa pamoja inakuwa kiasi kikubwa cha feza. Ikiwa tunatoa kama tulinavyoazimia moyoni, tutamufurahisha Baba yetu wa mbinguni, kwa kuwa ‘Mungu anamupenda mutoaji muchangamfu.’—2 Kor. 9:7.