Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
1. Kitabu gani kilitolewa kwenye Mukusanyiko wa Wilaya wa 2010, na kilichapishwa kwa kusudi gani?
1 Tulifurahi sana wakati kitabu kipya “Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia” kilitolewa kwenye Mukusanyiko wa Wilaya wa 2010 wenye kichwa “Baki Karibu na Yehova!” Kitabu hicho kinatoa maelezo kuhusu kitabu cha Yeremia na cha Maombolezo; kinazungumuzia piamambo tunayoweza kutumia katika maisha yetu ya kila siku. (Rom. 15:4) Kitabu hicho kilichapishwa ili kitumiwe kwenye Funzo la Biblia la Kutaniko. Kwa hiyo, kuanzia tarehe 5 Mwezi wa 11, 2012, tutaanza kukitumia kwenye mukutano huo.
2. Sababu gani tunaweza kufaidika kwa kuchunguza kitabu cha Biblia cha Yeremia na cha Maombolezo?
2 Maandishi ya Yeremia Ni Yenye Faida Kwetu Leo: Nabii Yeremia alitoa unabii wakati wa kipindi chenye musukosuko huko Yuda. Mwanzoni, hakujisikia kama ataweza kazi aliyopewa. (Yer. 1:6) Pia, Yeremia aliteswa na watu aliojuana nao na labda hata watu wa jamaa yake waliokuwa katika muji wake wa kuzaliwa, Anathothi. (Yer. 11:21, 22) Wakati fulani Yeremia alivunjika moyo. (Yer. 20:14) Tunapotimiza kazi yetu ya “kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,” sisi pia mara nyingi tunapata matatizo na tunajisikia kama Yeremia. (Mt. 28:19) Kuchunguza mambo aliyoandika kutatusaidia tutimize kazi yetu ya kuhubiri kwa uhakika na bidii.
3. Namna gani tutatumia kitabu Yeremia?
3 Mambo Fulani Yaliyo Katika Kitabu Hiki: Maandiko yanayopaswa kusomwa wakati wa funzo yanaandikwa na italiki. Mwisho wa kila funzo la juma kuna ulizo moja ao maulizo mawili yanayoandikwa na maandiko mazito meusi yanayosaidia kurudilia mawazo makubwa. Maulizo hayo yanapaswa kuulizwa ili kujikumbusha. Tangu mwanzo mupaka mwisho wa kitabu hiki kuna picha nzuri. Tuko hakika kwamba ndugu na dada watafurahia kutoa maelezo juu ya picha hizo.
4. Wakati tutajifunza kitabu Yeremia, itatuomba kufanya nini ili kufaidika zaidi?
4 Ili ufaidike kabisa na funzo, ujitayarishe mbele ya wakati. Tafuta mambo unayoweza kutumia katika maisha yako na katika kazi ya kuhubiri. Shiriki katika funzo kwa kutoa maelezo. Kwa baraka ya Yehova, Yeremia alitimiza kazi aliyopewa kwa furaha na alikuwa mwenye kutosheka. (Yer. 15:16) Basi, kuchunguza kitabu kipya hiki na kutusaidie kutimiza kazi yetu ya kuhubiri kwa furaha na kuwa wenye kutosheka.