Programu ya Juma Tokea Tarehe 13 Mwezi wa 8
JUMA TOKEA TAREHE 13 MWEZI WA 8
Wimbo 63 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 25 fu. 1-7, kisanduku kwenye uku. 199-200 (Dak. 25)
□ Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi:
Usomaji wa Biblia: Ezekieli 28-31 (Dak. 10)
Na. 1: Ezekieli 28:17-26 (Isipite dak. 4)
Na. 2: Jinsi ya Kutofautisha Hadisi za Kutunga na Mambo ya Kweli Kumuhusu Yesu Kristo (Dak. 5)
Na. 3: Ni Maandiko Gani Yanayoonyesha Maoni Ambayo Wakristo Wanapaswa Kuwa Nayo Kuhusu Kujiingiza Katika Mambo ya Politike?—rs uku. 137 fu. 1-5 (Dak. 5)
□ Mukutano wa Utumishi:
Wimbo 115
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 10: Tayarisha Musikilizaji ili Umurudilie Tena. Mazungumuzo yatakayotegemea maulizo yafuatayo: (1) Sababu gani ni jambo la faida kuweka musingi unapozungumuza na mutu mara ya kwanza ili umurudilie tena? (2) Namna gani tunaweza kuchagua ulizo lenye kupendeza musikilizaji ambalo tutajibia tutakapomurudilia? (3) Sababu gani ni vizuri kukubaliana juu ya wakati wa kumurudilia, na ikiwezekana, kumuomba namba yake ya telefone, ao adrese ya e-mail? (4) Sababu gani tujikaze kurudi bila kuchelewa, labda kisha siku chache? (5) Ni habari gani tunapaswa kuandika tukisha kuzungumuza na mutu kwa mara ya kwanza?
Dak. 10: Uliza mutumishi mumoja wa wakati wote ao wawili. Ni nini kilichowachochea waamue kuanza utumishi wa wakati wote? Ni matatizo gani waliyopata ambayo yangewazuia kuendelea na utumishi wa wakati wote, na ni nini kilichowawezesha waendelee? Ni baraka gani ambazo wamepata? Tia moyo wahubiri wafikirie kuwa mapainia wa kawaida katika mwaka wa utumishi unaokuja.
Dak. 10: “Linda Zamiri Yako.” Maulizo na majibu. Tangazia kutaniko tarehe ya mukusanyiko wa muzunguko ikiwa inajulikana.
Wimbo 65 na Sala