Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/12 uku. 1
  • Linda Zamiri Yako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Linda Zamiri Yako
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unaweza Kufanya Nini ili Zamiri Yako Iendelee Kuwa Safi?
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Kuwa na Zamiri ya Muzuri Mbele ya Mungu
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Namna gani Ninaweza Kuzoeza Zamiri Yangu?
    Vijana Wanauliza
  • Zamiri Yako Ni Kiongozi Mwenye Kutumainika?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 8/12 uku. 1

Linda Zamiri Yako

1. Mukusanyiko wetu wa pekee wa mwaka wa utumishi wa 2013 utakuwa na kichwa gani, na mukusanyiko huo una kusudi gani?

1 Kila siku tunakutana na hali ambazo zinaweza kutufanya tusisikilize zamiri yetu. Ndiyo sababu programu ya mukusanyiko wa pekee wa mwaka wa utumishi wa 2013, ambao utaanza tarehe 1 Mwezi wa 9, 2012, una kichwa “Linda Zamiri Yako.” (1 Tim. 1:19) Kusudi la programu hii ni kumusaidia kila mumoja wetu afikirie kwa uangalifu namna anavyotumia zamiri yake ambayo ni zawadi kila mutu alipewa na Mungu.

2. Ni maulizo gani ya maana ambayo yatajibiwa wakati wa mukusanyiko huo?

2 Tafuta Majibu ya Maulizo Yafuatayo: Programu ya mukusanyiko huu itajibu maulizo saba ya maana kuhusu zamiri:

• Ni mambo gani yanayoweza kuhatarisha zamiri?

• Namna gani tunaweza kuzoeza zamiri yetu?

• Inawezekana namna gani kuwa safi kutokana na damu ya watu wote?

• Tunapofikiri na kutenda kulingana na kanuni za Biblia, hilo linaonyesha nini juu yetu?

• Namna gani tunaweza kuepuka kuiumiza zamiri ya wengine?

• Vijana, namna gani munaweza kuendelea kuwa waaminifu wakati wenzenu wanawachochea kufanya mabaya?

• Wale wanaosikiliza zamiri yao iliyozoezwa na Neno la Mungu wanapata baraka gani?

3. Namna gani programu inaweza kutusaidia?

3 Kwa musaada wa Yehova, tunaweza kumupinga Shetani ili asiharibu zamiri yetu. Kupitia Neno la Mungu na tengenezo lake, Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo anatuambia hivi: ‘Hii ndiyo njia. Mutembee ndani yake.’ (Isa. 30:21) Programu hii ni njia moja ambayo Yehova anatumia ili kutuonyesha njia zake. Kwa hiyo, ufanye mipango ili kuhuzuria programu yote ya mukusanyiko huo. Fuata kwa uangalifu, na fikiria jinsi unavyoweza kutumia habari hiyo katika maisha yako. Muzungumuzie programu hiyo katika familia. Ikiwa tutatumia mashauri tutakayopewa, hilo litatuchochea tuendelee ‘kuwa na zamiri njema’ na kutatusaidia tusishawishiwe na raha ya ulimwengu wa Shetani iliyo ya muda tu inayoweza kutufanya tusifuate uongozi wa Yehova—1 Pet. 3:16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine