Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma tokea tarehe 27 mwezi wa 8, 2012. Tarehe ambayo kila jambo litazungumuziwa inaonyeshwa pia ili kusaidia watu kutafuta majibu katika vitabu wanapotayarisha masomo ya huduma ya kila juma.
1. Mambo ambayo Ezekieli aliona katika ndoto juu ya taifa la Yuda lenye kuasi-imani yalifananisha nini mbele ya wakati, na hilo linatufundisha jambo gani la lazima? (Eze. 8:15-17) [Tokea tarehe 2 Mwezi wa 7, w07 1/7 uku. 13 fu. 6; w93 15/1 uku. 27-28 fu. 7, 12]
2. Namna gani viongozi wengi wa kidini wanaiga manabii wa uongo wa wakati wa Ezekieli? (Eze. 13:3, 7) [Tokea tarehe 9 Mwezi wa 7, w99 1/10 uku. 13 fu. 14-15]
3. Katika unabii ulio kwenye Ezekieli 17:22-24, “kitawi kichanga” ni nani, ‘mulima murefu ulio juu sana’ ambako anapandikizwa ni nini, na namna gani atakuwa ‘mwerezi mukubwa’? [Tokea tarehe 16 Mwezi wa 7, w07 1/7 uku. 12-13 fu. 6]
4. Kulingana na maneno ya mufano yaliyo katika andiko la Ezekieli 18:2, wale waliohamishwa pamoja na Ezekieli walimulaumu nani kwa ajili ya mateso yao, na ni jambo gani la lazima tunalojifunza kutokana na habari hiyo? [Tokea tarehe 23 Mwezi wa 7, w88 15/9 uku. 18 fu. 10]
5. Namna gani habari iliyo katika Ezekieli 21:18-22 inaonyesha kama iwe wanadamu wala roho waovu hawawezi kulizuia kusudi la Yehova? [Tokea tarehe 30 Mwezi wa 7, w07 1/7 uku. 14 fu. 4]
6. Kulingana na Ezekieli 24:6, 11, 12, kutu ya chungu cha kupikia inafananisha nini, na ni kanuni gani inayopatikana katika mustari wa 14? [Tokea tarehe 6 Mwezi wa 7, w07 1/7 uku. 14 fu. 2]
7. Unabii juu ya muji wa Tiro ulitimia namna gani? [Tokea tarehe 6 Mwezi wa 8, it-1-F kisanduku kwenye uku. 75; si uku. 133 fu. 4]
8. Ni maneno gani yanayotumiwa katika Ezekieli 28:2, 12-17 yanayomufaa ‘mufalme wa Tiro’ na Shetani, muasi wa kwanza kwanza? [Tokea tarehe 13 Mwezi wa 8, w05 15/10 uku. 23-24 fu. 10-14; it-2-F uku. 604 fu. 4-5]
9. Misri ilifanywa ukiwa kwa miaka 40 wakati gani, na ni nini kinatusaidia kuamini kama jambo hilo lilitokea kabisa? (Eze. 29:8-12) [Tokea tarehe 13 Mwezi wa 8, w07 1/8 uku. 8 fu. 5]
10. Namna gani Ezekieli aliweza kutangaza ujumbe wake ijapokuwa watu hawakupendezwa nao, walimucheka, na hawakumusikiliza; na Yehova alimuhakikishia nini? (Eze. 33:31-33) [Tokea tarehe 20 Mwezi wa 8, w91 15/3 uku. 17 fu. 16-17]