Mabadiliko Kuhusu Mikutano Fulani
Kuanzia tarehe 3 mwezi wa 9, funzo la Biblia la kutaniko litaongozwa kwa dakika 30 pahali pa dakika 25. Katika maneno yake ya utangulizi, ndugu anayeongoza funzo atachukua dakika moja ili kurudilia mambo fulani yaliyochunguzwa katika funzo la juma lililopita. Pia, mukutano wa utumishi utaendeshwa kwa dakika 30 pahali pa dakika 35. Hakutakuwa tena sehemu ya matangazo. Lakini, ikiwa kuna matangazo, yatatolewa mwanzoni mwa sehemu ya kwanza ya mukutano wa utumishi. Kwa kawaida hakutakuwa matangazo yoyote, na ikiwa kuna matangazo, yatakuwa machache tu. Haitakuwa lazima kutangazia kutaniko vipindi mbalimbali vya mukutano wa utumishi. Matangazo kuhusu mukutano kwa ajili ya mahubiri, programu ya kusafisha Jumba la Ufalme, na salamu hayatatolewa. (km 10/08 uku. 1, fu. 4) Ikiwa kuna tangazo ndefu, itakuwa vizuri ndugu watakaoshiriki katika mukutano huo wajue mbele ya wakati ili wafupishe sehemu zao.