Matangazo
◼ Mwezi wa 10: Tutawatolea watu Munara wa Mulinzi na Amkeni! Unapowarudilia watu, uwaonyeshe kitabu Biblia Inafundisha, ao ikiwa inafaa kulingana na mahitaji ya musikilizaji, umuonyeshe broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele, na jaribu kuanzisha funzo la Biblia. Mwezi wa 11 na wa 12: Je, Ungependa Kujua Kweli?, Kila Namna ya Kuteseka Itakwisha Karibuni!, Yehova—Yeye Ni Nani?, ao Yesu Kristo—Yeye Ni Nani? Ikiwa mutu anapendezwa, umuonyeshe namna funzo la Biblia linafanywa kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha, ao broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele. Mwezi wa 1 na wa 2: Tutawatolea watu broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Je! Kweli Mungu Anatujali?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, ao Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! Unapowarudilia watu, uwaonyeshe kitabu Biblia Inafundisha, ao ikiwa inafaa kulingana na mahitaji ya musikilizaji, umuonyeshe broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele, na jaribu kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Katika Mwezi wa 10, makutaniko yote yanayochangia Jumba la Ufalme yatachunguza programu yao ya mikutano ya kuanzia tarehe 1 Mwezi wa 1, 2013; kisha, makutaniko ambayo yatabadilisha programu yatajulisha biro ya tawi mbele ya tarehe 1 Mwezi wa 12. Ikiwa kutaniko lenu lina adrese ya internete kwenye jw.org, tafazali mubadilishe wakati wa mikutano yenu kwenye adrese hiyo.