Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 11
“Wengi kati yetu wanapenda waongozwe na serikali nzuri. Wewe unawaza ni serikali ya aina gani inayoweza kumaliza matatizo ya wanadamu? [Acha mutu ajibu.] Ona wazo lililo katika gazeti hili.” Umupatie musikilizaji Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 11, na muzungumuzie pamoja habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16 na musome andiko moja ao zaidi. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili muzungumuzie ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/11/12
“Tulipenda kukuuliza ulizo moja. Ikiwa ungepewa nafasi ya kumuuliza Mungu jambo fulani, wewe ungemuuliza nini? [Acha mutu ajibu.] Yesu alionyesha kama ni vizuri kutafuta majibu kwa maulizo yetu. [Soma Mathayo 7:7.] Gazeti hili linatoa majibu ya Biblia kwa maulizo haya matatu ya maana.” Umuonyeshe musikilizaji maulizo yaliyo mwishoni mwa ukurasa wa 3.
Amkeni! Mwezi wa 11
“Tunawatembelea watu kwa sababu tuna habari inayoweza kusaidia familia. Familia zilizo na muzazi mumoja tu zimekuwa nyingi. Unafikiri familia hizo zina matatizo mengi zaidi kuliko familia zilizo na wazazi wawili? [Acha mutu ajibu.] Wazazi wengi wamepata mashauri mazuri katika Biblia. [Soma 2 Timotheo 3:16.] Gazeti hili linaonyesha mambo ambayo muzazi anayewalea watoto peke yake anaweza kufanya ili ashugulikie vizuri daraka lake.”