Programu ya Juma Tokea Tarehe 24 Mwezi wa 12
JUMA TOKEA TAREHE 24 MWEZI WA 12
Wimbo 5 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 3 fu. 1-6 (Dak. 30)
□ Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi:
Usomaji wa Biblia: Zekaria 9-14 (Dak. 10)
Na. 1: Zekaria 11:1-13 (Isipite dak. 4)
Na. 2: Mungu Anapenda Kusikiliza Sala za Nani?—rs uku. 257 fu. 1–uku. 258 fu. 3 (Dak. 5)
Na. 3: Ni Katika Hali Gani Tunaweza Kutumia Andiko la Methali 15:1? (Dak. 5)
□ Mukutano wa Utumishi:
Wimbo 75
Dak. 30: Namna Tunavyoweza Kutumia Adresi Yetu ya Internete Inayojulikana Kisheria. Mazungumuzo yanayotegemea ukurasa 3-6. Munapozungumuzia ukurasa wa 4, kwa muda wa dakika tatu mufanye onyesho kuhusu familia ambayo imemaliza kufanya Ibada ya Familia ya mangaribi. Baba anawaomba washiriki wa familia watoe mapendekezo kuhusu mambo ambayo wangependa wazungumuzie juma linalofuata, na watoto wanataja habari fulani zilizo kwenye adresi yetu ya Internete katika sehemu yenye kichwa “Vijana”. Uwaombe wasikilizaji waeleze namna wametumia, ao namna wanapanga kutumia, jw.org katika funzo lao la pekee ao ibada ya familia. Munapozungumuzia ukurasa wa 5, kwa muda wa dakika tatu mufanye onyesho kuhusu muhubiri anayetumia adresi yetu ya Internete kwenye telefone ao ordinatere ya mukononi ili kujibu ulizo la musikilizaji kuhusu mambo tunayoamini. Munapozungumuzia ukurasa wa 6, kwa muda wa dakika ine mufanye onyesho kuhusu muhubiri anayezungumuza na mutu anayependezwa ambaye anapendelea kusoma vichapo vyetu katika luga tofauti. Muhubiri anatumia telefone ao ordinatere yake ya mukononi ao ordinatere ya musikilizaji ili kufungua trakte Kujua Kweli ao kitabu Biblia Inafundisha kwenye jw.org katika luga ya musikilizaji na kuizungumuzia pamoja naye. Uwaombe wasikilizaji waeleze namna wametumia jw.org katika mahubiri. (Habari hii inaendelea kwenye ukurasa wa 8, Matangazo, fungu la 4).
Wimbo 101 na Sala