Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma tokea tarehe 25 Mwezi wa 2, 2013. Tarehe ambayo kila jambo litazungumuziwa inaonyeshwa pia ili kusaidia watu kutafuta majibu katika vitabu wanapotayarisha masomo ya huduma ya kila juma.
1. Sababu gani Yesu alisema kama wenye furaha ni “wale wanaoomboleza”? (Mt. 5:4) [Juma tokea tarehe 7 Mwezi wa 1, w09 15/2 uku. 6 fu. 6]
2. Katika ile sala ya kielelezo ambayo Yesu aliwafundisha wanafunzi wake, alimaanisha nini aliposema: “Usituingize katika jaribu”? (Mt. 6:13) [Juma tokea tarehe 7 Mwezi wa 1, w04 1/2 uku. 16 fu. 13]
3. Sababu gani Yesu alisema kama wanafunzi wake hawatamaliza kuhubiri majiji yote ya Israeli “mupaka Mwana wa binadamu atakapofika”? (Mt. 10:23) [Juma tokea tarehe 14 Mwezi wa 1, w10 15/9 uku. 10 fu. 12; w87-F 1/8 uku. 8 fu. 6]
4. Ni mambo gani mawili yanayoonyeshwa katika mufano wa Yesu wa mbegu ya haradali? (Mt. 13:31, 32) [Juma tokea tarehe 21 Mwezi wa 1, w08 15/7 uk. 17-18 fu. 3-8]
5. Yesu alifundisha somo gani aliposema: ‘Musipogeuka na kuwa kama watoto wachanga, hamutaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni’? (Mt. 18:3) [Juma tokea tarehe 28 Mwezi wa 1, w07 1/2 uku. 9-10 fu. 3-4]
6. Yesu alimaanisha nini aliposema, “wewe mwenyewe umesema”? (Mt. 26:63, 64) [Juma tokea tarehe 11 Mwezi wa 2, w11 1/6 uk. 18]
7. Sababu gani Yesu anaitwa “Bwana hata wa sabato”? (Mk. 2:28) [Juma tokea tarehe 18 Mwezi wa 2, w08 15/2 uku. 28 fu. 7]
8. Sababu gani Yesu aliitikia kwa namna alivyosema kuhusu mama yake na ndugu zake, na hilo linatufundisha nini? (Mk. 3:31-35) [Juma tokea tarehe 18 Mwezi wa 2, w08 15/2 uk. 29 fu. 5]
9. Kama inavyoelezwa katika andiko la Marko 8:22-25, labda ni kwa sababu gani Yesu alimuponya mutu aliyekuwa kipofu kwa hatua mbili, na tunaweza kujifunza nini kutokana na hilo? [Juma tokea tarehe 25 Mwezi wa 2, w00 15/2 uku. 17 fu. 7]
10. Tunajifunza nini kutokana na jinsi ambavyo Yesu alimukaripia Petro kama inavyoelezwa kwenye Marko 8:32-34? [Juma tokea tarehe 25 Mwezi wa 2, w08 15/2 uku. 29 fu. 6]