Je, Na Mimi Nisimamishe?
Wanapohubiri, wahubiri fulani wana zoea la kusimamisha mahubiri wakati waliopanga, labda na saa sita ya muchana. Ni kweli kwamba hali za wahubiri fulani zinaweza kuwalazimisha wasimamishe mahubiri wakati fulani. Lakini, je, wewe unasimamisha mahubiri kwa sababu tu wengine katika kikundi wanafanya hivyo ao kwa sababu ni zoea la watu wa eneo lenu kusimamisha mahubiri wakati fulani uliopangwa? Je, unaweza kuendelea na mahubiri kwa muda wa wakati fulani na kushiriki katika namna fulani ya kutoa ushahidi mahali pa watu wengi, kwa mufano kuhubiri barabarani? Je, unaweza kumurudilia mutu mumoja ao watu wawili unaporudi nyumbani? Fikiria jambo nzuri ambalo utatimiza ikiwa unapata hata mutu mumoja anayependezwa nyumbani ao ikiwa unamutolea mupita njia magazeti! Ikiwa hatusimamishe mahubiri, kuendelea na mahubiri kwa muda fulani ni njia rahisi ya kuongeza ‘zabihu yetu ya sifa.’—Ebr. 13:15.