UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MHUBIRI 7-12
‘Umukumbuke . . . Muumbaji Wako Mukubwa Katika Siku za Ujana Wako’
Umukumbuke Muumbaji wako Mukubwa kwa kutumia uwezo wako wote ili kumutumikia wakati ungali kijana
12:1, 13
Vijana wengi wanatimiza migawo migumu kwa sababu wako na afya ya muzuri na nguvu nyingi
Vijana wanapaswa kutumia wakati na nguvu yao ili kumutumikia Yehova mbele magumu ya wakati wa uzee yawazuie
Sulemani alitumia mashairi ili kuzungumuzia magumu yenye yanatokea wakati wa uzee
12:2-7
Mustari wa 3: “Mabibi wanaochungulia madirishani wameona giza”
Uwezo wa kuona unapunguka
Mustari wa 4: ‘Mabinti wote wa wimbo wanatoa sauti ya chini’
Uwezo wa kusikia unapunguka
Mustari wa 5: ‘Pilipili inapasuka’
Hamu ya kula inapunguka