UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 20-21
“Kila Mutu Mwenye Anataka Kuwa Mukubwa Katikati Yenu Anapaswa Kuwa Mutumishi Wenu”
Waandishi na Mafarisayo wenye majivuno walipenda watu wawaone na kuwasalimia kwenye soko
Waandishi na Mafarisayo wenye majivuno walipenda watu wawaone na walipenda kujulikana sana. (Mt 23:5-7) Yesu hakukuwa hivyo. ‘Mwana wa binadamu hakukuja ili watu wamutumikie, lakini ili yeye atumikie wengine.’ (Mt 20:28) Tunakubali kwanza migao yenye inaweza kufanya watu watuone na tujulikane sana? Yesu alisema mukubwa ni ule mwenye anatumikia wengine. Mara nyingi kazi hiyo inafanywa bila watu kuona; Yehova tu ndiye anaiona. (Mt 6:1-4) Mutumishi munyenyekevu anapaswa . . .
kusaidia kusafisha na kutengeneza Jumba la Ufalme
kuwa wa kwanza kusaidia wazee-wazee na wengine
kutoa feza zake ili kutegemeza mambo ya Ufalme