MAISHA YA MUKRISTO
Yehova Ametufundisha Namna ya Kukomalisha Watoto Yetu
Mufano ya baba yetu wa mbinguni Yehova inaweza kupatia wazazi mafundisho gani ya kuwasaidia wakomalishe muzuri watoto yao? Muangalie video Yehova Ametufundisha Namna ya Kukomalisha Watoto Yetu, na kisha mujibie hii maulizo juu ya maisha ya Abilio na Ulla Amorim:
Namna gani mambo yenye Abilio na Ulla walijionea wakati walikuwa watoto iliwasaidia kukomalisha muzuri watoto yao?
Watoto ya Abilio na Ulla wanakumbuka mambo gani ya muzuri yenye waliwafundisha wakati walikuwa watoto?
Abilio na Ulla walifanya nini juu ya kutumikisha andiko ya Kumbukumbu la Torati 6:6, 7?
Sababu gani Abilio na Ulla hawakulazimisha watoto yao kufuata sheria za Mungu?
Namna gani Abilio na Ulla walisaidia watoto yao wafanye maamuzi ya muzuri mu maisha yao?
Abilio na Ulla walijiima jambo gani wakati walitia moyo watoto yao waingie mu utumishi wa wakati wote? (bt uku. 178 fu. 19)