UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 9-11
“Dunia Yote Iliendelea Kuwa na Luga Moja”
Kwenye Babeli, Yehova alivuruga luga ili kusambaza wanadamu wenye hawakumutii. Leo iko anakusanya kundi kubwa la watu wenye kutoka katika mataifa yote na luga zote na anawapatia “luga safi” ili “waitie jina la Yehova, wamutumikie bega kwa bega.” (Sef 3:9; Ufu 7:9) Ile “luga safi” ni kweli juu ya Yehova na juu ya makusudi yake, kama vile inaonyeshwa katika Maandiko.
Kujifunza luga mupya haiko tu kuweka maneno ya mupya mu akili, lakini inaomba kujifunza namna ya mupya ya kuwaza. Vilevile, wakati tuko tunajifunza luga safi ya ile kweli, akili yetu inageuzwa. (Ro 12:2) Kuendelea kufanya vile kunasaidia watu wa Mungu wakuwe na umoja.—1Ko 1:10.