Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/03 uku. 4
  • Fundisheni Wengine Lugha Safi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Fundisheni Wengine Lugha Safi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Dunia Yote Iliendelea Kuwa na Luga Moja”
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Tuhubirie Watu Wanaozungumza Luga ya Kigeni
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 1/03 uku. 4

Fundisheni Wengine Lugha Safi

1 Ijapokuwa wanatoka katika ‘mataifa mengi, makabila, vikundi vya watu na lugha,’ Mashahidi wa Yehova ni watu wenye kuungana, undugu wa kimataifa wa kweli. (Ufu. 7:9) Hilo ni jambo lenye kutokeza katika ulimwengu wa leo wenye kugawanyika. Linawezekanaje? Kwa kuwa ‘tuligeuziwa lugha safi.’—Zef. 3:9.

2 Matokeo Mazuri Ajabu: Hiyo lugha safi ni nini? Ni uelewevu unaofaa wa kweli inayopatikana katika Neno la Mungu kuhusu Yehova na makusudi yake, zaidi sana kweli kuhusu Ufalme wa Mungu. Kama ilivyotabiriwa na Yesu, kweli hiyo ni yenye kutolewa kupitia njia ya kidunia yenye kuonekana, “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” tokeo likiwa kwamba watu “wa lugha zote za mataifa” wanakubali ibada safi.—Mt. 24:45; Zek. 8:23.

3 Watu wanapojifunza lugha safi, wanachochewa wapatanishe maisha zao na viwango vya Yehova. Wanajifunza kuwa wenye “kuunganishwa kwa kufaa katika akili ileile na katika mstari uleule wa fikira.” (1 Kor. 1:10) Ufundishaji wa kimungu unatokeza pia ndani yao mwenendo mzuri na usemi unaofaa na wenye kweli, zaidi sana kuhusiana na kuelezea wengine habari njema. (Tito 2:7, 8; Ebr. 13:15) Mabadiliko hayo mazuri ajabu yanamletea Yehova heshima.

4 Kwa mfano, mwanamume mmoja aliyesikia habari njema alikuwa na maulizo mengi, na yote yalipata majibu kutoka katika Biblia. Akichochewa na yale aliyosikia, akaanza kujifunza mara mbili kwa juma na kuhudhuria mikutano. Alishangaa kwa kuona ukaribishaji wenye shauku aliopokea kwenye Jumba la Ufalme, kwa kuwa wengi kati ya wahudhuriaji walikuwa wa rangi tofauti. Baada ya wakati mfupi, yeye na mke wake wakafanya mabadiliko katika maisha zao na kubatizwa. Tangu wakati huo amesaidia wengine karibu 40 wamtumikie Yehova, kutia ndani washiriki wengi wa familia. Ijapokuwa yeye ni kilema, alianza karibuni kutumikia akiwa painia.

5 Kuwafundisha Wengine: Matukio ya ulimwengu yanafanya watu wengi wanyofu wachunguze upya mafikiri yao na maisha zao. Kama Yesu, tunapaswa kutaka kuwasaidia. Ziara za kurudia zenye matokeo na mafunzo ya Biblia ni ufunguo wa kusaidia watu wanyofu wajifunze lugha safi.

6 Ufundi ambao umeonekana kuwa wenye matokeo kuhusiana na watu wenye shughuli ni kuendesha funzo fupi la Biblia unapokuwa mlangoni kwao. (km-ZS 5/02 uku. 1) Je, umejaribu ufundi huo? Unapojitayarisha kufanya ziara ya kurudia, chagua kutoka nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002 utoaji unaofaa mwenye nyumba. Mwingi wa ule utoaji mbalimbali unaopatikana katika nyongeza hiyo umetayarishwa ili kuongoza moja kwa moja kwenye mazungumzo katika broshua Anataka au kitabu Ujuzi. Fanya mazoezi ya utoaji ili utangulizi wako ukuongoze ifaavyo kwenye mazungumzo kuhusu moja la yale mafungu. Chagua kutoka katika fungu andiko moja au mawili ya kusoma na kuzungumzia, na utayarishe ulizo utakalomalizia nalo. Hilo litasaidia kuongoza kwenye fungu unalopanga kuzungumzia kwenye ziara ijayo.

7 Watu wa Yehova wanapata baraka nyingi kutokana na kujifunza ile lugha safi. Acheni tusaidie kwa bidii wengine waungane nasi katika ‘kuitia jina la Yehova’ na ‘kumtumikia bega kwa bega.’—Zef. 3:9, NW.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine