Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
© 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
TAREHE 5-11/5
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 12
Kazi ya Nguvu Inalipaka
Sifa Yenye Kumupendeza Mungu ya Maana Sana Kupita Alimasi
Inaweza kuwa vigumu kwa watumishi fulani wa Yehova kupata feza za kutimiza mambo yao yote ya lazima. Lakini, kuliko kujikaza kutafuta njia nyepesi na ya udanganyifu, wanatumika sana na kwa bidii. Kwa kufanya hivyo, wanaonyesha kama sifa za Mungu zenye kupendeza sana, hata sifa ya uaminifu, ni za maana sana kuliko vitu vingine vyote vya kimwili.—Methali 12:24; Waefeso 4:28.
wp15 1/2 uku. 5 fu. 4-6
Namna ya Kufurahia Kazi Ngumu
Ni muzuri sana kufikiria ulizo hilo la mwisho, kwa kuwa kazi inaleta furaha zaidi wakati tunaona faida yenye inaletea watu wengine. Yesu mwenyewe alisema hivi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Matendo 20:35) Zaidi ya wale wanaofaidika moja kwa moja kupitia kazi yetu, kama vile watu wanaotununulia vitu ao wakubwa wetu wa kazi, kuna watu wengine wanaofaidika na kazi yetu ngumu. Watu hao wanatia ndani watu wa familia yetu na watu walio na lazima ya musaada.
Watu wa familia yetu. Wakati kichwa cha familia anatumika sana ili kutolea watu wa familia yake vitu walivyo navyo lazima, anawaletea faida katika njia mbili hivi. Kwanza, anawasaidia kupata vitu vya kimwili vyenye wako navyo lazima katika maisha, kama vile chakula, nguo, na makao. Kwa kufanya hivyo, anatimiza daraka lake alilopewa na Mungu la ‘kuwaandalia mahitaji wale walio wake mwenyewe.’ (1 Timotheo 5:8) Jambo la pili, mutu anayetafuta kwa bidii vitu familia yake iko navyo lazima anafundisha wengine faida ya kazi ngumu kupitia mufano wake. Shane, aliyetajwa katika habari iliyotangulia anasema hivi: “Baba yangu ni mutu anayeonyesha mufano muzuri katika kuwa na tabia za muzuri za kazi. Ni mwanaume muaminifu ambaye amefanya kazi ngumu maisha yake yote, sehemu kubwa ya maisha yake amefanya kazi ya useremala. Kupitia mufano wake, nimejifunza faida ya kufanya kazi kwa mikono yangu, kutengeneza vitu vyenye vitakuwa na faida kwa watu wengine.”
Watu walio na lazima ya musaada. Mutume Paulo alishauria Wakristo “wafanye kazi ya bidii . . . ili wakuwe na kitu cha kumugawia mutu aliye na uhitaji.” (Waefeso 4:28) Kwa kweli, wakati tunafanya kazi ngumu ili kupata vitu tulivyo navyo lazima sisi wenyewe na familia yetu, tunaweza pia kuwa na uwezo wa kusaidia walio na lazima ya musaada. (Methali 3:27) Kwa hiyo, kazi ngumu inaweza kutusaidia kuwa na furaha kubwa ya kutoa.
Mali ya Kiroho
ijwyp habari ya 95 fu. 10-11
Niko na Roho Nguvu?
● Jua ukubwa wa magumu yako. Ujue kutofautisha magumu ya kidogo na ya munene. Biblia inasema: “Mupumbavu anaonyesha pale pale kwamba ameuzika, lakini mutu mwerevu anapuuza matusi.” (Mezali 12:16) Haiko kila magumu njo inapaswa kukusumbua sana.
“Ku masomo, wanafunzi wenzangu walikuwa wanalalamika-lalamika juu ya mambo yenye haiko hata ya kulalamikia. Kisha sasa marafiki wao wanatumia site za kupashana habari na watu wengi juu ya kuwaambia kama ni vile njo walipaswa kufanya—Na ile inafanya walalamike tena zaidi. Kufanya vile hakuwasaidie wajue namna ya kumaliza magumu yao.”—Joanne.
Onyesho: Unaamini Kama Dini Yenu tu Njo ya Kweli?
ijwfq habari ya 3
Je, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kama Dini Yao Tu Ndio ya Kweli?
Wale wanaochukua dini kwa uzito, wanapaswa kuhakikisha kama dini yao inakubaliwa na Mungu na Yesu. Kama sivyo, kwa nini waliichagua?
Yesu Kristo hakufundisha kama dini zote ni kama barabara zinaongoza kwenye uzima wa milele. Lakini, yeye alisema hivi: “Lango ni jembamba na barabara inayoongoza kwenye uzima ina nafasi ndogo, na wachache ndio wanaoipata.” (Mathayo 7:14) Mashahidi wa Yehova wanaamini kama wamepata barabara hiyo. Kama sivyo, wangechagua dini ingine.
TAREHE 12-18/5
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 13
Usidanganywe na “Taa ya Waovu”
it-2 uku. 109 fu. 4-5
Taa
Matumizi Ingine ya Mufano. Jambo yenye mutu anatumainia juu ya kuangazia njia yake inafananishwa na taa. Ni mu ile maana njo mezali inalinganisha mwenye haki na muovu wakati inasema hivi: “Mwangaza wa wenye haki unangaa sana, lakini taa ya waovu itazimishwa.” (Mez 13:9) Mwangaza wa mwenye haki unaendeleaka kungara. Lakini, hata kama tala ya muovu inangara sana na hata kama anaonekana kuwa amefanikiwa, Mungu atafanya yake yote juu muovu aishie mu giza na bila shaka mugulu wake utajikwala. Njo vile mambo itakuwa kwa mutu mwenye analaani baba yake na mama yake.—Mez 20:20.
Kusema kama ‘tala ya mutu fulani itazimwa’ inamaanisha pia kama hakuna tumaini juu ya ule mutu. Mezali ingine inasema hivi: “Hakuna wakati muzuri wenye kuja kwa ajili ya muovu hata mumoja; taa ya waovu itazimwa.”—Mez 24:20.
Umutumikie Mungu Anayetoa Uhuru
3 Ikiwa Shetani aliweza kuwadanganya wanadamu wakamilifu wa kwanza na kuwafanya malaika wengi wakatae utawala wa Mungu, basi anaweza kutudanganya sisi pia. Shetani anatumia njia ileile ili kutudanganya. Anajaribu kutufanya tufikiri kama sheria za Mungu ni nzito na zinatufunga-funga ili tusifurahie maisha. (1 Yoh. 5:3) Ikiwa tunafanya urafiki na watu wanaowaza hivyo, sisi pia tunaweza kuanza kufikiri kama wao. Dada mumoja mwenye umri wa miaka 24, ambaye aliangukia katika uasherati, alisema hivi: “Marafiki wabaya walinifanya niangukie katika kosa hilo kwa sababu niliogopa nisionekane kuwa na mawazo tofauti na yao.” Labda wewe pia umekwisha kujionea namna mikazo ya marafiki inavyoweza kumuchochea mutu kufanya makosa.
w04-SW 15/7 uku. 31 fu. 6
“Kila Mtu Aliye Mwerevu Atatenda kwa Ujuzi”
Mtu mwenye hekima na mnyoofu ambaye hutenda kwa ujuzi wa kweli atabarikiwa. Sulemani anatuhakikishia: “Mwadilifu anakula mpaka nafsi yake inaposhiba, lakini tumbo la waovu litakuwa tupu.” (Methali 13:25) Yehova anajua kinachotufaa katika kila sehemu ya maisha yetu—iwe ni mambo yanayohusu familia, uhusiano wetu na wengine, huduma yetu, au tunapotiwa nidhamu. Bila shaka, tukifuata kwa hekima shauri la Neno lake, maisha yetu yatakuwa bora.
Mali ya Kiroho
it-1 uku. 109 fu. 3
Upendo
Tunaweza kuonyesha upendo mu njia yenye haifae. Ni wazi kama juu mutu aonyeshe upendo wa kweli na wenye kufaa, anapaswa kutafuta na kufuata muongozo wa roho ya Mungu na ujuzi wenye kuwa mu Neno yake. Kwa mufano, muzazi anaweza kuwa anapendaka mutoto wake. Lakini ile upendo inaweza kuharibika ao anaweza kuionyesha mu njia yenye haifae. Pengine juu ya kuchochewa na hisia, anaweza kuanza kupatia mutoto kila kitu na kushindwa kumukatalia hata kitu moya. Anaweza kushindwa kutumia mamlaka yake kwa kukosa kumupatia mutoto nizamu ao kukosa kumupatia malipizi. (Mez 22:15) Upendo wa vile unaweza kufanya mutoto akuwe na kiburi na ajifikirie tu yeye mwenyewe. Biblia inaonyesha kama muzazi mwenye kuonyesha upendo mu ile njia, kusema kweli hamupende mutoto wake; anamuchukia njo, juu ile itamuingiza mu hatari.—Mez 13:24; 23:13, 14.
TAREHE 19-25/5
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 14
Fikiria Sana Kila Hatua Wakati Musiba Unatokea
Usamini Zawadi ya Mungu ya Uzima
10 Wakati fulani, hatuwezi kuzuia hali fulani ya mubaya itokee. Sawa vile misiba ya asili, magonjwa ya kuambukiza, na vita. Lakini wakati misiba ya vile inatokea, tunaweza kufanya yetu yote ili kuwa salama kadiri inawezekana, na tunaweza kuokoa uzima wetu kwa kutii wakati wenye mamlaka wanatuomba tutoke mu eneo ao wakati wanatupatia maagizo ingine. (Ro. 13:1, 5-7) Ni muzuri kujitayarisha mbele ya wakati, njo maana tunapaswa kufuata maagizo yenye inatolewa na wenye mamlaka wa mu eneo yetu yenye itatusaidia tukuwe tayari wakati musiba unatokea. Kwa mufano, ni muzuri kuwa na maji na chakula yenye haitaoza, na pia vitu vya musaada wa kwanza.
11 Tunapaswa kufanya nini kama ugonjwa fulani wa kuambukiza unaenea fasi kwenye tunaishi? Tunapaswa kutii maagizo ya wenye mamlaka, sawa vile kunawa mikono, kuheshimia umbali, kuvala maske, na kujitenga na wengine. Wakati tunajikaza kufanya ile mambo yote tutaonyesha kama tunasamini zawadi ya Mungu ya uzima.
12 Wakati musiba fulani unatokea, tunaweza kusikia marafiki ao majirani wetu wako naongea kuhusu habari fulani ya uongo, tunaweza pia kusikia habari ya vile kupitia vyombo vya kupashana habari. Kuliko kuamini “kila neno” yenye tunasikia, tunapaswa kusikiliza habari ya kweli yenye inatolewa na watu wenye kuwa na mamlaka ao yenye inatolewa na wanganga. (Soma Mezali 14:15.) Ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza na wa biro za tawi wanajikazaka kupata habari za kweli mbele ya kutoa muongozo kuhusu mikutano ya kutaniko na kazi ya kuhubiri. (Ebr. 13:17) Tukifuata ile maagizo, tunajilinda na tunalinda wengine. Ile inasaidia pia watu wakuwe na mawazo ya muzuri juu ya Mashahidi wa Yehova.—1 Pe. 2:12.
Ukuwe Hodari Kama Sadoki
11 Kama wanatuomba tusaidie ndugu zetu mu kipindi yenye kuwa hatari, namna gani tunaweza kuonyesha uhodari kama Sadoki? (1) Fuata muongozo. Mu hali ya vile, ni jambo ya maana kuendelea kuwa na umoja. Fuata muongozo wa tawi ya inchi yenu. (Ebr. 13:17) Wazee wanapaswa kuchunguza kwa ukawaida mipango mbalimbali ya kujitayarisha kwa ajili ya misiba, na pia muongozo wenye tengenezo inatoa kuhusu namna ya kutenda wakati musiba unatokea. (1 Ko. 14:33, 40) (2) Ukuwe hodari lakini muangalifu. (Mez. 22:3) Ufikiri mbele ya kutenda. Usijitie mu hatari bila sababu. (3) Umutegemee Yehova. Kumbuka kama Yehova anahangaikia sana usalama wako na wa ndugu zako. Anaweza kukusaidia juu utolee ndugu zako musaada mu njia yenye kuwa salama.
Mali ya Kiroho
it-1 uku. 398
Uwezo wa Kufikiri
Mutu mwenye kutumia kabisa uwezo wa kufikiri anaweza kuchukiwa. Ile njo wazo yenye iko mu Mezali 14:17: “Mutu mwenye kufikiri sana juu ya mambo anachukiwa.” Mara mingi, batu benye habakuwake nafikiri sana, habapendake batu benye banatumikishaka uwezo wabo wa kufikiri. Tena, mara mingi, batu benye kutumia akili yabo juu ya kufanya mapenzi ya Mungu banachukiwaka. Ile inapatana na maneno yenye Yesu alisemaka: “Sababu ninyi hamuko sehemu ya ulimwengu, lakini nimewachagua ninyi kutoka katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukia ninyi.” (Yoh 15:19) Mu Mezali 14:17, maneno “mwenye kufikiri sana juu ya mambo” inaweza pia kumaanisha mutu mwenye kufikiria mambo ya mubaya. Njo maana hii andiko inaweza pia kumaanisha kama mutu mwenye kufikiria mambo ya mubaya anachukiwaka, na njo vile inatafsiriwa mu tafsiri fulani za Biblia.
TAREHE 26/5–1/6
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 15
Saidia Bengine Bakuwe na Moyo Wenye Furaha
w10-SW 15/11 uku. 31 fu. 16
Tutatembea Katika Utimilifu Wetu!
16 Ayubu aliwakaribisha wageni. (Ayu. 31:31, 32) Ingawa huenda tusiwe matajiri, tunaweza ‘kufuata mwendo wa ukaribishaji-wageni.’ (Rom. 12:13) Tunaweza kula pamoja na wengine chakula chepesi, huku tukikumbuka kwamba “afadhali chakula cha mboga za majani mahali penye upendo kuliko ng’ombe-dume aliyenoneshwa pamoja na chuki.” (Met. 15:17) Kula chakula chepesi katika mazingira yenye upendo pamoja na Mkristo mwenzetu ambaye anashika utimilifu kutafanya hata chakula hicho kiwe chenye kufurahisha na bila shaka tutafaidika kiroho.
Tutiane Moyo, Zaidi Sana Leo
16 Inaweza kuwa makosa kufikiri kama hatuwezi kutia wengine moyo kwa sababu hatuzoee kabisa kuzungumuza na wengine. Haiombe mambo mengi ili kutia wengine moyo, pengine tunaweza tu kuonyesha sura ya kicheko wakati tunasalimia mutu. Ikiwa mutu huyo hatuonyeshe sura ya kicheko, hilo linaweza kumaanisha kama pengine iko na tatizo fulani, na kumusikiliza kunaweza kumufariji.—Yak. 1:19.
17 Henri, ndugu kijana, alihuzunika sana wakati watu wa familia yake, waliacha kweli, kutia ndani baba yake mwenye alikuwa muzee mwenye kuheshimiwa. Mwangalizi mumoja wa muzunguko alimutia Henri moyo wakati alimupeleka nafasi ya kuuzia vyakula vidogo-vidogo na akamuuzia kahawa na kumuacha afungue moyo wake. Kisha mazungumuzo hayo, Henri alitambua kama ili kusaidia watu wa familia yake warudie katika kweli, alipaswa kubakia muaminifu. Alitiwa moyo wakati alisoma Zaburi ya 46; Sefania 3:17; na Marko 10:29, 30.
18 Mufano wa Marthe na Henri unaonyesha kama tunaweza kutia moyo ndugu ao dada mwenye kuwa na lazima ya faraja. Mufalme Sulemani aliandika hivi: ‘Neno linalosemwa wakati unaofaa ni njema kama nini! Kungaa kwa macho kunafanya moyo ushangilie; habari ambayo ni njema inaifanya mifupa inone.’ (Met. 15:23, 30) Zaidi ya hilo, kusomea mutu fulani mwenye kuvunjika moyo habari fulani katika gazeti Munara wa Mulinzi ao kwenye site yetu ya Internete kunaweza kumutia nguvu. Paulo anaonyesha kama kuimba pamoja nyimbo za Ufalme kunaweza kututia moyo. Aliandika hivi: ‘Muendelee kufundishana na kuonyana [ao, “kutiana moyo”] kwa zaburi, sifa kwa Mungu, nyimbo za kiroho kwa neema, mukimuimbia Yehova mioyoni mwenu.’—Kol. 3:16; Mdo. 16:25.
Mali ya Kiroho
ijwbq habari ya 39 fu. 3
Je, Mukristo Anaweza Kukubali Matunzo ya Kiganga?
2. Je, nitafute mashauri kwa waganga wengine? Ndiyo, kuwauliza “washauri wengi” kunaweza kukusaidia, zaidi sana ikiwa umegonjwa sana.—Mezali 15:22.
TAREHE 2-8/6
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 16
Maulizo Tatu Yenye Inaweza Kutusaidia Kukamata Maaumuzi ya Muzuri
Kijana, Chukua Maamuzi Yenye Hekima
11 Furaha kubwa zaidi inatokana na kumutumikia Yehova. (Met. 16:20) Inaonekana kwamba Baruku, aliyekuwa mwandishi wa Yeremia, alisahau jambo hilo. Wakati fulani, hakufurahia tena kumutumikia Yehova. Yehova alimuambia hivi: ‘Unaendelea kujitafutia mambo makubwa. Usiendelee kuyatafuta. Kwa maana karibuni nitaleta musiba juu ya wote wenye mwili, . . . na nitakupa uzima wako kuwa nyara mahali popote utakapoenda.’ (Yer. 45:3, 5) Unawaza ni jambo gani ambalo lingemuletea Baruku furaha: Kutafuta mambo makubwa ao kumutumikia Yehova kwa uaminifu ili kuokoka uharibifu wa Yerusalemu?—Yak. 1:12.
12 Ndugu Ramiro alipata furaha kwa kuwatumikia wengine. Anasema hivi: “Nilikomalia katika kijiji kinachopatikana kwenye Milima ya Andes. Familia yangu ilikuwa maskini. Kwa hiyo wakati kaka yangu aliahidi kunilipia masomo ya juu, hiyo ilikuwa bahati kabisa. Lakini nilikuwa nimebatizwa hivi karibuni, na painia mumoja alikuwa amenialika ili nihubiri naye katika muji fulani mudogo. Nilienda huko, nilijifunza kukata nywele, na nilifungua chumba cha kukatia nywele ili nipate feza kwa ajili ya mahitaji yangu. Watu wengi ambao tulihubiria walikubali kujifunza Biblia. Baadaye, nilijiunga na kutaniko mupya ambalo lilikuwa limeanzishwa katika luga ya eneo hilo. Sasa nimefanya upainia kwa miaka kumi katika eneo hilo. Hakuna kazi ambayo ingeweza kuniletea furaha ninayopata kwa kuwasaidia watu wajifunze Biblia katika luga yao.”
Je, Umebadilika?
NAMNA sisi wote tulivyolelewa na mahali tunapoishi vinatufanya tufikiri ao tutende kwa njia fulani. Kwa mufano, tunazoea kuvaa kwa njia fulani, tunapenda aina fulani ya chakula; na tunatenda kwa njia fulani. Sababu gani? Kwanza, ni kwa sababu watu wanaotuzunguka wanatuchochea kutenda kwa njia fulani ao tunachochewa na hali mbalimbali tunazojionea katika maisha.
2 Hata hivyo, kuna mambo fulani yaliyo ya maana sana kuliko aina ya chakula na mutindo wa mavazi tunayochagua. Kwa mufano, tulipokuwa watoto tulifundishwa kwamba tunapaswa kuona mambo fulani kuwa mazuri na yenye kufaa na kuepuka mambo mengine yaliyo mabaya na yasiyofaa. Lakini watu wengi wana maoni tofauti kuhusu mambo hayo. Zamiri yetu inaweza hata kutuchochea kuchukua maamuzi mazuri ao mabaya. Biblia inaonyesha kwamba mara nyingi ‘watu wa mataifa wasio na sheria wanafanya kwa asili mambo ya sheria.’ (Rom. 2:14) Lakini, je, hilo linamaanisha kwamba ikiwa hakuna sheria ya Mungu iliyo wazi, tunapaswa kufuata desturi na kanuni tulizofundishwa tulipokuwa watoto na zinazopendwa na watu wengi wa mahali tunapoishi?
3 Kuna sababu kubwa mbili hivi zinazotufanya sisi Wakristo tuepuke jambo hilo. Sababu ya kwanza, Biblia inatukumbusha hivi: “Kuna njia ambayo imenyooka mbele ya mwanadamu, lakini njia za kifo ndizo mwisho wake baadaye.” (Met. 16:25) Kwa sababu ya hali yetu ya kutokamilika, sisi wanadamu hatuna uwezo wa kuongoza kabisa hatua zetu vizuri. (Met. 28:26; Yer. 10:23) Sababu ya pili, Biblia inaonyesha kwamba desturi na kanuni za ulimwengu zinaongozwa na Shetani, ambaye ni ‘mungu wa mufumo huu wa mambo.’ (2 Kor. 4:4; 1 Yoh. 5:19) Kwa hiyo, ikiwa tunataka kubarikiwa na kukubaliwa na Yehova, tunahitaji kufuata mashauri yanayopatikana katika andiko la Waroma 12:2.—Soma.
Mali ya Kiroho
it-1 uku. 651
Nizamu
Matokeo ya Kutii ao ya Kukosa Kutii. Baovu na bapumbavu banaonyeshaka kama banachukia nizamu ya Yehova kwa kukatala kabisa kutii. (Zb 50:16, 17; Mez 1:7) Mutu mwenye anatenda kwa upumbavu vile, anapataka nizamu ingine zaidi ao hata malipizi ya nguvu. Vile mezali inasema: “Wapumbavu wanapewa nizamu kwa upumbavu wao wenyewe.” (Mez 16:22) Banaweza kujiletea bumaskini, haya, magonjwa, na banaweza hata kufa mbele ya wakati. Mufano wa Baisraeli unaonyesha namna kukosa kutii inaweza kuwa na matokeo ya mubaya sana. Habakutii nizamu yenye Yehova alibatolea kupitia ujumbe wa manabii. Tena, Yehova alibapatia nizamu kwa kuacha kubalinda na kubabariki, lakini habakumutii. Ku mwisho, balipata malipizi ya nguvu yenye Yehova alikuwaka amebatangazia tangu zamani, ni kusema balikamatwa na bakahamishwa mu inchi ingine.—Yer 2:30; 5:3; 7:28; 17:23; 32:33; Ho 7:12-16; 10:10; Sef 3:2.
Hotuba: Mezali 16:3 Inamaanisha Nini?
ijwbv-SW habari ya 40
Mithali 16:3—“Mkabidhi BWANA Kazi Zako”
Methali hii inawahakikishia wale wanaomwabudu Mungu wa kweli kwamba kazi zao au mipango yao itafanikiwa ikiwa wataonyesha kwamba wanamtegemea Mungu kwa kutafuta mwongozo wake na kuufuata.
“Mkabidhi Yehova lolote unalofanya.” Kabla ya kufanya maamuzi, kwa unyenyekevu watumishi wa Yehovaa humwomba mwongozo. (Yakobo 1:5) Kwa nini? Sababu moja ni kwamba, kwa kawaida wanadamu hawana uwezo wa kuamua mambo yatakayowapata maishani. (Mhubiri 9:11; Yakobo 4:13-15) Kwa kuongezea, huenda wasiwe na hekima inayohitajika ili kutekeleza mipango yao. Hivyo, kwa busara wengi humkabidhi Mungu mambo yao. Wanafanya hivyo wanapomwomba mwongozo na kutenda kulingana na mapenzi yake yaliyofunuliwa katika Neno lake Biblia.—Methali 3:5, 6; 2 Timotheo 3:16, 17.
Maneno “Mkabidhi BWANA kazi zako” kihalisi yanamaanisha “mvingirishie BWANA kazi zako.” Kitabu kimoja cha marejeo kinasema kwamba maneno hayo yanaleta picha ya “mtu [ambaye] anatua mzigo aliokuwa amebeba na kuutwika mgongoni mwa mtu mwingine ambaye ana nguvu zaidi na uwezo wa kuubeba.” Wale ambao kwa unyenyekevu wanamtumaini Mungu wanaweza kuwa na uhakika kwamba atawasaidia na kuwategemeza.—Zaburi 37:5; 55:22.
Maneno “lolote unalofanya” hayamaanishi kwamba Mungu anakubaliana na mipango yote inayofanywa na watu na kuibariki. Ili watu wapate baraka za Yehova, ni lazima mipango yao ipatane na viwango vyake na pia mapenzi yake. (Zaburi 127:1; 1 Yohana 5:14) Mungu anabariki utii na si kutotii. Kwa kweli, yeye “huivuruga mipango ya waovu.” (Zaburi 146:9) Lakini kwa upande mwingine, anawasaidia wale wanaojitiisha kwake kwa kuheshimu viwango alivyoweka katika Biblia.—Zaburi 37:23.
“Na mipango yako itafanikiwa.” Tafsiri nyingine zinasema, “mawazo yako yatathibitika.” Katika Maandiko ya Kiebrania ambayo mara nyingi yanaitwa Agano la Kale, neno lililotafsiriwa “yatathibitika” linaleta maana ya kuweka msingi na mara nyingi linatumiwa kurejelea jinsi vitu ambavyo Mungu ameumba vilivyo imara. (Methali 3:19; Yeremia 10:12) Vivyo hivyo, Mungu atathibitisha kabisa mipango ya wale wanaofanya yaliyo mema machoni pake na atawasaidia kuwa na maisha yenye usalama, utulivu, na furaha.—Zaburi 20:4; Methali 12:3.
TAREHE 9-15/6
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 17
Furahia Amani mu Ndoa Yako
Namna ya Kuacha Kuweka Kinyongo
Jichunguze muzuri. Biblia inaonyesha kwamba watu fulani ni ‘wenye hasira na wenye muelekeo wa gazabu.’ (Methali 29:22) Je, ni vile uko? Jiulize: ‘Nina muelekeo wa kukasirika? Ninakasirika kwa vyepesi? Kila mara ninatafuta kubishana juu ya mambo madogomadogo?’ Biblia inasema kwamba mutu “anayeendelea kuongea juu ya jambo anawatenganisha watu wanaofahamiana.” (Methali 17:9; Mhubiri 7:9) Inaweza kuwa hivyo pia katika ndoa. Kwa hiyo, ikiwa una muelekeo wa kuweka kinyongo, jiulize, ‘Ninaweza kujikaza ili niwe muvumilivu zaidi kwa bibi ao bwana yangu?’—Kanuni ya Biblia: 1 Petro 4:8.
w08-SW 1/5 uku. 10 fu. 6–uku. 11 fu. 1
Kutatua Matatizo
1. Pangeni wakati wa kuzungumzia tatizo. “Kuna wakati uliowekwa wa kila kitu, . . . wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema.” (Mhubiri 3:1, 7) Kama kisa kilichosimuliwa mwanzoni kilivyoonyesha, matatizo fulani yanaweza kufanya hasira ipande. Hilo likitokea, jizuie na usimamishe mazungumzo kwa muda—‘kaa kimya’—kabla hasira haijawaka. Unaweza kuzuia uhusiano wenu usiharibike ukitii shauri hili la Biblia: “Kuanzisha ugomvi ni kama kufanya ufa kwenye bwawa; achana na ugomvi kabla haujafurika.”—Methali 17:14, Biblia Habari Njema.
Hata hivyo, pia kuna “wakati wa kusema.” Matatizo ni kama magugu ambayo yanasitawi yakiachiliwa. Basi usipuuze tatizo, ukifikiri kwamba litakwisha tu. Ukikatiza mazungumzo, mwonyeshe mwenzi wako wa ndoa heshima kwa kuchagua wakati wa kuzungumzia tatizo hilo bila kukawia. Ahadi kama hiyo inaweza kuwasaidia nyote wawili kufuata kanuni hii ya Biblia: “Jua lisitue mkiwa katika hali ya kuchokozeka.” (Waefeso 4:26) Bila shaka, unahitaji kutimiza ahadi yako.
Mali ya Kiroho
it-2 uku. 432 fu. 9
Jicho
Biblia inasema kama macho ya mujinga “yanaenda huku na huku mupaka kwenye miisho ya dunia.” Ile maneno inaonyesha kama mujinga hakazake akili ku jambo moya; anaachaka mawazo yake iende huku na huku kuliko kufikiria mambo yenye alipaswa kufikiria.—Mez 17:24.
Hotuba: Mezali 17:17 Inamaanisha Nini?
ijwbv habari ya 60
Mezali 17:17—“Rafiki wa Kweli Anapenda Nyakati Zote”
Rafiki wa kweli ni mutu mwenye tunaweza kutegemea na kutumainia. Sawa vile bandugu ba mu familia moya, rafiki wa kweli anakuwaka mushikamanifu na anahangaikianaka, zaidi sana wakati wa magumu.
“Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote.” Ile musemwa inaweza pia kumaanisha “barafiki banaonyeshanaka upendo kila siku.” Neno ya Kiebrania yenye inatafsiriwa “upendo” mu hii musemwa haiko tu kujisikia kuwa unapenda mutu fulani. Ni upendo wenye mutu anaonyesha kupitia matendo, bila kujifikiria tu yeye mwenyewe. (1 Wakorinto 13:4-7) Barafiki benye kupendana vile banaendeleaka kuwa pamoya hata kutokee nini, ikuwe kutoelewana ao magumu ingine. Banakuwaka pia tayari kusameheana bila kulazimishwa. (Mezali 10:12) Na tena, rafiki wa kweli hakuwake mwivu kama mambo inamuendea mwenzake muzuri. Kuliko kufanya vile, anakuwaka njo anafurahi pamoya naye.—Waroma 12:15.
“Rafiki . . . ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.” Mara mingi batu ya familia moya banakuwaka na uhusiano wa karibu sana. Njo maana hii mezali inafananisha rafiki na ndugu. Juu wakati tunafanya yetu yote juu ya kusaidia rafiki mwenye iko napata magumu, tunafanya tu sawa vile ndugu ao dada yake mwenye alizaliwa naye angefanya. Zaidi ya yote, uhusiano wenye uko kati ya barafiki ba vile hauvunjikake juu ya magumu. Upendo na heshima mingi binafanyaka ule uhusiano ukuwe njo nguvu zaidi.
TAREHE 16-22/6
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 18
Utie Moyo Bale Benye Biko na Matatizo ya Afya
Hekima ya Kweli Inaita Kwa Sauti Kubwa
17 Ufikiri mbele ya kusema. Kama hatuko waangalifu, tunaweza kuumiza wengine sana kupitia maneno yetu. Biblia inasema hivi: “Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga, lakini ulimi wa mwenye hekima unaponyesha.” (Mez. 12:18) Tunalinda uhusiano muzuri na wengine wakati tunaepuka kupiga porojo kuhusu makosa ya wengine. (Mez. 20:19) Juu maneno yetu iponyeshe kuliko kuumiza, tunapaswa kujaza mu moyo wetu ujuzi wa Neno ya Mungu. (Lu. 6:45) Kama tunafikiri sana juu ya mambo yenye Biblia inasema, maneno yetu itakuwa sawa vile “chemchemi ya hekima” yenye inatia moyo wengine.—Mez. 18:4.
mrt-SW habari ya 19 kisanduku
Jinsi ya Kukabiliana na Tatizo la Afya
Uwe msikilizaji mzuri. Njia moja bora ya kumsaidia rafiki yako ni kumsikiliza anapozungumza. Usihisi kwamba ni lazima uwe na jambo la kusema kila mara anapozungumza. Mara nyingi inatosha tu kusikiliza. Jaribu kuwa na mtazamo unaofaa na usimhukumu. Kumbuka kwamba hujui kabisa jinsi rafiki yako anavyohisi, hasa ikiwa haonekani kwa nje kuwa mgonjwa.—Methali 11:2.
Zungumza kwa njia inayotia moyo. Huenda usijue jambo la kusema lakini kusema maneno machache yanayoonyesha unatambua hali ngumu ya rafiki yako kunaweza kumfariji zaidi kuliko kunyamaza. Ikiwa hujui jambo la kusema, jaribu kumwambia maneno rahisi lakini yanayotoka moyoni, kama vile “Sijui jambo la kukuambia, lakini ningependa ujue kwamba ninakujali.” Epuka kusema maneno kama vile “shukuru kwamba hali yako si mbaya sana” au “Angalau ugonjwa wako si . . .”
Unaweza kuonyesha kwamba unapendezwa na rafiki yako kwa kujifunza kuhusu ugonjwa wake. Huenda atafurahi kwamba unajaribu kuelewa hali yake, na kuna uwezekano kwamba maneno yako yatakuwa na maana zaidi. (Methali 18:13) Hata hivyo, uwe mwangalifu usitoe mashauri bila kuombwa.
Toa msaada hususa. Badala ya kufikiria kwamba unajua jinsi ya kutoa msaada, uliza jambo unaloweza kufanya. Hata hivyo, kumbuka kwamba huenda rafiki yako asikubali anahitaji msaada, kwa sababu hataki kukuongezea mzigo. Ikiwa haombi msaada, jaribu kupendekeza msaada hususa unaoweza kutoa, kama vile kumfanyia ununuzi, usafi, au kazi nyingine.—Wagalatia 6:2.
Usife moyo. Rafiki yako anapoendelea kukabiliana na ugonjwa wake, huenda pindi nyingine akaahirisha mipango mliyokuwa nayo au akahisi kwamba hataki kuzungumza nawe. Uwe na subira na ujaribu kumwelewa. Endelea kumpa msaada anaohitaji.—Methali 18:24.
wp23.1 uku. 14 fu. 3–uku. 15 fu.1
Namna ya Kusaidia Wale Wenye Wako na Matatizo ya Akili
“Museme kwa namna yenye kufariji.”—1 WATESALONIKE 5:14.
Rafiki yako anaweza kuwa na wasiwasi ao anaweza kujiona kuwa wa bure. Hata kama haujue useme nini juu ya kumufariji, kama tu unaonyesha kuwa unamuhangaikia, ile inaweza kumufariji na kumutia moyo.
“Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote.”—MEZALI 17:17.
Umutolee musaada wenye kufaa. Kuliko kuwaza tu kama unajua namna ya kumusaidia, umuulize mambo yenye unaweza kumufanyia. Kama rafiki yako anashindwa kukuambia mambo yenye iko nayo lazima, upime kumuuliza kama munaweza kufanya jambo fulani pamoya, sawa vile kuenda kutembea. Ao unaweza kumusaidia kuenda kuuza vitu, kufanya usafi, ao kazi ingine.—Wagalatia 6:2.
“Mukuwe wavumilivu.”—1 WATESALONIKE 5:14.
Haiko kila wakati njo rafiki yako anaweza kuwa tayari kusema. Umuhakikishie kama utapenda kumusikiliza wakati atapenda kusema. Rafiki yako anaweza kufanya ao kusema jambo fulani yenye inakuhuzunisha. Pengine anaweza kubadilisha mipango yenye mulikuwa nayo, ao anaweza kubadilika tu na kuwa sawa mutu mwenye kukasirika. Ukuwe muvumilivu na ujikaze kumuelewa wakati uko namutolea musaada wenye iko nao lazima.—Mezali 18:24.
Mali ya Kiroho
it-2 uku. 1004
Kura
Kupiga kura ni desturi ya zamani yenye ilikuwaka nasaidia batu kukamata uamuzi. Wakati ya kupiga kura, batu balikuwaka nasali juu ya kutafuta muongozo wa Yehova.
Matumizi. Mezali 16:33 inasema hivi: “Kura inapigwa katika sehemu ya nguo yenye kufunika mapaja, lakini kila uamuzi wenye unafanywa kwa kura hiyo unatoka kwa Yehova.” Mu Israeli, kusudi yenye kufaa ya kura ilikuwa kumaliza ubishi. Njo maana Biblia inasema hivi: “Kupiga kura kunakomesha mabishano na kunakata maneno kati ya wapinzani wenye nguvu.” (Mez 18:18) Kura haikuwa natumikishwa mu mambo ya mazoezi, michezo, ao michezo ya makuta. Hakukuwaka bya ku parier, ni kusema hakuna mutu angepoteza ao kupata kitu. Kura haikuwaka natumiwa juu ya kupata makuta ya kutumikisha ku hekalu, ao juu ya kufanya makuhani bakuwe matajiri, ao juu ya kusaidia bengine. Tofauti na ile, wakati baaskari Baroma balipigiaka nguo ya Yesu kura, sawa vile Zaburi 22:18 ilisemaka, balikuwa natafuta tu faida yabo.—Mt 27:35.
Onyesho: Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kama Mungu Aliumba Mbingu na Dunia kwa Siku Sita Zenye Urefu wa Saa 24?
ijwfq habari ya 29
Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kama Mungu Aliumba Mbingu na Dunia kwa Siku Sita Zenye Urefu wa Saa 24
Hapana. Mashahidi wa Yehova wanaamini kama Mungu aliumba vitu vyote. Lakini, hawaamini kama Mungu aliumba mbingu na dunia kwa siku sita zenye urefu wa saa 24. Juu ya nini? Juu Biblia haiseme vile. Fikiria mifano mbili yenye kufuata:
1. Urefu wa zile siku sita za uumbaji. Watu fulani wanaamini kama siku sita za uumbaji zilikuwa na urefu wa saa 24. Lakini mu Biblia, neno “siku” inaweza kumaanisha wakati murefu sana.—Mwanzo 2:4; Zaburi 90:4.
2. Miaka ya dunia. Watu fulani wanafundisha kama Dunia iko tu na maelfu kidogo ya miaka. Lakini, Biblia inafundisha kama mbingu na dunia vilikuwa mbele ya zile siku sita za uumbaji. (Mwanzo 1:1) Njo maana, Mashahidi wa Yehova wanakubali mawazo ya wanasayansi ya kama inawezekana dunia iko na mamiliare ya miaka hivi.
Hata kama Mashahidi wa Yehova wanaamini kama Mungu njo aliumba vitu vyote, hawakatalake mambo yenye wanasayansi wanasemaka. Tunaamini kama mambo yenye sayansi ya kweli inasema inapatana na mambo yenye Biblia inasema.
TAREHE 23-29/6
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 19
Ukuwe Rafiki Muzuri kwa Bandugu na Badada Yako
Namna Tunaweza Kuendelea Kupendana Sana
16 Kazia sifa za muzuri za ndugu na dada zako, hapana uzaifu wao. Kwa mufano wazia munakutana pamoya na ndugu na dada ili kujifurahisha. Munapitisha wakati ya muzuri pamoja, na ku mwisho munakamata picha pamoja. Juu haujue kama ile picha ya kwanza itatoka muzuri, unakamata picha mbili zingine. Sasa uko na picha tatu. Lakini mu picha moya unaona kama ndugu fulani alifunga sura. Sasa utafanya nini na ile picha? Utavuta ile picha juu ungali na picha zingine mbili kwenye kila mutu iko nacheka, kutia ndani ule ndugu.
17 Zile picha ziko sawa vile mambo yenye tunachunga mu akili. Mara mingi tunachungaka mu akili wakati za muzuri zenye tulipitisha pamoya na ndugu na dada zetu. Lakini wazia wakati moya kati ya zile, ndugu ao dada alisema ao kufanya jambo fulani yenye haukufurahia. Utafanya nini juu ya ile? Hauone kama ni muzuri uivute mu akili sawa vile ulivuta ile picha moya? (Mez. 19:11; Efe. 4:32) Sawa vile hatupoteze kitu kama tunavuta picha moya ya mubaya, hatupoteze kitu kama tunasahau wakati moya ya mubaya yenye tulipitisha pamoja na ndugu na dada yetu, juu tuko na wakati zingine za mingi za muzuri zenye tumepitisha pamoja naye. Na zile njo tunapaswa kuweka mu akili na kuzifurahia.
Umupende Yehova Zaidi na Uendelee Kupenda Wengine
10 Na siye pia tunatafutaka njia mbalimbali za kusaidia ndugu na dada zetu. (Ebr. 13:16) Fikiria habari ya Anna, mwenye tulitaya mu habari yenye kutangulia. Kisha upepo mukali, yeye na bwana yake walitembelea familia moya ya Mashahidi na waliona kama ule upepo uliharibisha sehemu ya yulu ya nyumba ya ile familia. Ile ilifanya manguo ya ile familia ichafuke. Anna anasema hivi: “Tulikamata ile manguo, tukaifula, kuikunja na kuigoma, kisha tukabarudishia ayo. Tuliona kama ile ilikuwa tu tendo ya kidogo, lakini ilifanya tukuwe na urafiki wa nguvu sana pamoya nao tangu ile siku.” Kupenda ndugu na dada njo kulichochea Anna na bwana yake wasaidie ile familia.—1 Yo. 3:17, 18.
11 Wakati tunafanyia wengine mambo ya muzuri na kuwaonyesha kama tunawapenda, mara mingi wanaonaka vile tuko tunajikaza kumuiga Yehova, na wanaweza hata kusamini matendo yetu ya muzuri kuliko vile tunaweza kuwazia. Khanh, mwenye tulishataya, anakumbuka wale wenye walimusaidiaka. Anasema hivi: “Nashukuru sana dada zangu wote wenye walikuwa naenda na miye mu mahubiri. Walikuwa nakuya kunikamata ku nyumba, walinialika kuenda kula nao chakula fulani, na walikuwa wanahakikisha kama nilikuwa nafika muzuri ku nyumba. Kwa sasa njo natambua kama walikuwa najikaza sana ili kufanya vile. Na walifanya vile juu walinipenda.” Kusema kweli, haiko kila mutu njo atatushukuru juu ya jambo yenye tulimufanyia. Khanh anasema hivi juu ya wale wenye walimusaidiaka: “Ningependa kuwalipa juu ya mambo ya muzuri yenye walinifanyiaka, lakini sijue kwenye wote wanaishi kwa sasa. Juu Yehova anajua kwenye wote wanaishi, niko namuomba awalipe.” Khanh alisema kweli. Yehova anaonaka hata tendo ya muzuri ya kidogo sana yenye tunafanyiaka wengine. Yehova anasaminiaka ile sana na anaionaka kuwa deni yenye atalipa.—Soma Mezali 19:17.
Muendelee Kuonyeshana Upendo Mushikamanifu
6 Kama mufanyakazi fulani ametumika miaka mingi mu kompanyi fulani, tunaweza kusema kama iko mushikamanifu ku ile kompanyi. Lakini, pengine mu ile miaka yote, hayaonanaka na musimamizi wa ile kompanyi. Na pengine hakubalianake kila mara na maamuzi ya ile kompanyi. Hatuwezi kusema kama anapenda kompanyi yake. Anafurahia tu kutumika pale juu ile kazi njo inamusaidiaka apate makuta. Ataendelea kutumika mule mupaka afikie miaka ya kuacha kazi. Lakini akipata kazi ya muzuri fasi ingine, anaweza kuacha ile kazi.
7 Kuko tofauti gani kati ya mufanyakazi mwenye iko mushikamanifu ku komapanyi yake na mutu mwenye kuonyesha upendo mushikamani? Tofauti ni nia ya kila mumoja, ao jambo yenye inamusukuma kutenda. Nini njo ilisukuma watumishi wa Yehova wa zamani waonyeshe upendo mushikamanifu? Walionyesha upendo mushikamanifu, hapana juu ya kutafuta faida fulani, lakini juu moyo wao uliwasukuma kufanya vile. Tufikirie mufano wa Daudi. Moyo wake njo ulimusukuma aonyeshe Yonatani rafiki yake upendo mushikamanifu, hata kama baba yake alikuwa natafuta kumuua Daudi. Na miaka mingi kisha Yonatani kufa, Daudi aliendelea pia kuonyesha Mefibosheti, mutoto wa Yonatani, upendo mushikamanifu.—1 Sa. 20:9, 14, 15; 2 Sa. 4:4; 8:15; 9:1, 6, 7.
Mali ya Kiroho
it-1 uku. 516
Shauri
Yehova tu njo iko na hekima ya juu sana. Yeye tu njo mwenye hana lazima ya mashauri kutoka kwa mutu yeyote. (Isa 40:13; Ro 11:34) Mutoto wake ni “Mushauri wa Ajabu.” Anatoaka muongozo juu anapataka mashauri kutoka kwa Mungu na anakuwaka naitumikisha, na pia anakuwaka na roho ya Mungu. (Isa 9:6; 11:2; Yoh 5:19, 30) Ile inaonyesha kama ikiwa tunapenda kushauria mutu hatupaswe kusahau kutafuta mawazo ya Yehova. Shauri yoyote yenye haipatane na mawazo ya Mwenye Kuwa Juu Zaidi haina faida. Ile haiko shauri hata kidogo.—Mez 19:21; 21:30.
TAREHE 30/6–6/7
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 20
Urafiki wa Kimapenzi Wenye Utasaidia Mukamate Uamuzi wa Muzuri
Urafiki Wenu wa Kimapenzi Uwasaidie Kukamata Uamuzi Muzuri
3 Wakati wa urafiki wa kimapenzi ni wakati wenye kufurahisha, lakini pia ni hatua ya maana yenye inaweza kuongoza ku ndoa. Siku ya ndoa, ndugu na dada wenye kuwa mu uhusiano wa kimapenzi wanafanya naziri mbele ya Yehova kama watapendana na kuheshimiana muda wote wa maisha yao. Mbele ya kufanya naziri yoyote, tunapaswa kufikiria naziri yetu kwa uzito. (Soma Mezali 20:25.) Ni vile pia kuhusu naziri ya ndoa. Urafiki wa kimapenzi unasaidia ndugu na dada wajuane muzuri, na wakamate uamuzi wa muzuri. Ule uamuzi unaweza kuwa kuoana na wakati fulani unaweza kuwa kuvunja urafiki. Kama ndugu na dada wanavunja urafiki wao wa kimapenzi, ile haimaanishe kama wamekosea. Lakini inaonyesha kama ule urafiki ulitimiza kusudi yake, uliwasaidia kujua ikiwa wanaweza kuoana ao hapana.
4 Juu ya nini ni jambo ya maana tukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya urafiki wa kimapenzi? Wakati ndugu ao dada mwenye hayafunga ndoa iko na mawazo yenye kufaa, hatafanya urafiki wa kimapenzi na mutu mwenye hana nia ya kuoana naye. Lakini haiko tu Wakristo wenye hawayafunga ndoa njo wanapaswa kuwa na mawazo yenye kufaa. Siye wote tunapaswa kuwa na mawazo yenye kufaa. Kwa mufano, watu fulani wanawaza kama ikiwa ndugu na dada wako mu uhusiano wa kimapenzi wanapaswa tu kuoana. Ile mawazo inaweza kuwa na matokeo gani juu ya Wakristo wenye hawafunga ndoa? Melissa, dada mwenye hayaolewa wa mu Amerika anasema hivi: “Wakati Wakristo wawili wako nachumbiana, wengine wanatazamia tu kama wanapaswa kuoana. Matokeo ni kama, Wakristo fulani wenye kuwa mu uhusiano wa kimapenzi, wanaendelea na ule uhusiano hata kama wanaona kuwa uhusiano wao hauendelee muzuri. Pia ile inafanya Wakristo fulani waepuke kabisa kuanzisha uhusiano wa kimapenzi. Zile hali zote zinaweza kuleta mahangaiko ya mingi sana.”
Namna ya Kupata Mutu Mwenye Anaweza Kuwa Bibi ao Bwana Muzuri
8 Ku mikutano ya Kikristo ao wakati munakutana na ndugu na dada ili kujifurahisha, unaweza kutambua mambo fulani juu ya hali ya kiroho ya ule mutu, utu wake, na mwenendo wake. Marafiki wake ni nani? Anaongeaka kuhusu mambo gani? (Lu. 6:45) Miradi yake inapatana na miradi yako? Unaweza kuzungumuza na wazee wa mu kutaniko yake ao na Wakristo wenye kukomaa kiroho wenye wanamujua muzuri. (Mez. 20:18) Unaweza kuuliza kuhusu sifa zake na namna yake ya kuwa. (Rut. 2:11) Wakati uko nachunguza ule ndugu ao dada, usifanye ajisikie mubaya, usijiingize mu mambo yake ya kipekee, na usimufuate-fuate fasi yote.
Urafiki Wenu wa Kimapenzi Uwasaidie Kukamata Uamuzi Muzuri
7 Unaweza kufanya nini juu ujue mutu muzuri kabisa? Jambo moya ya maana ya kufanya ni kuzungumuza waziwazi na bila kuficha kitu, kuuliza maulizo, na kusikiliza kwa uangalifu. (Mez. 20:5; Yak. 1:19) Ili kufanya vile, inaweza kuwa muzuri kufanya mambo fulani yenye inawapatia nafasi ya kuzungumuza. Sawa vile kula pamoya, kutembea pamoya mahali pa watu wengi, na kuhubiri pamoya. Munaweza pia kujuana muzuri wakati munapitisha wakati pamoya na marafiki na watu wa familia. Zaidi ya ile, panga kufanya mambo yenye inaweza kukusaidia kujua namna mwenzako anatendaka mu hali tofauti-tofauti na wakati iko na watu tofauti-tofauti. Ona mambo yenye Aschwin, wa mu inchi ya Hollande, alijaribu kufanya. Anasema hivi kuhusu urafiki wake wa kimapenzi pamoya na Alicia: “Tulifanya mambo yenye ingetusaidia kujuana muzuri. Mara mingi ilikuwa mambo ya kawaida, sawa vile kupiga chakula pamoya ao kufanya kazi za ku nyumba pamoya. Wakati tulikuwa tunafanya ile mambo, kila mumoja wetu aliona sifa za muzuri za mwingine na uzaifu wake.”
8 Kujifunza pamoya mambo ya kiroho kunaweza pia kuwasaidia kujuana muzuri. Kama munaoana, itakuwa lazima mupange wakati wa kufanya ibada ya familia juu muweze kutia Mungu pa nafasi ya kwanza mu ndoa yenu. (Mez. 4:12) Hamuone kama ni muzuri mupange wakati wa kujifunza pamoya tangu sasa, wakati mungali mu urafiki wa kimapenzi? Ni kweli kama wale wenye wako mu urafiki wa kimapenzi hawayakuwa familia, na ndugu hayakuwa kichwa cha dada. Hata vile kujifunza pamoya kunaweza kusaidia kila mumoja wenu ajue hali ya kiroho ya mwingine. Max na Lyasa bibi na bwana wa mu Amerika, waliona faida ingine ya kufanya vile. Max anasema hivi: “Ku mwanzo tu wa urafiki wetu wa kimapenzi tulianza kuzungumuzia vichapo vyenye vilikuwa na habari sawa vile kufanya urafiki wa kimapenzi, ndoa, na maisha ya familia. Vile vichapo vilitusaidia kuzungumuzia mambo ya maana yenye hatungeweza kuzungumuzia siye wenyewe.”
Mali ya Kiroho
it-2 uku. 109 fu. 9
Taa
Mezali 20:27 inasema kama “pumuzi ya mutu ni taa ya Yehova,inachunguza kabisa utu wake wa ndani sana.” Mambo yenye mutu anasemaka, ikuwe ya muzuri ao ya mubaya, inaonyeshaka vile iko kabisa, ni kusema utu wake wa ndani.
Onyesho: Manyama Inaendaka Mbinguni?
ijwbq-SW habari ya 159
Je, Wanyama Wanaenda Mbinguni?
Biblia inafundisha kwamba kati ya viumbe wote duniani, ni wanadamu wachache tu watakaoenda mbinguni. (Ufunuo 14:1, 3) Wataenda huko ili watawale wakiwa wafalme na makuhani pamoja na Yesu. (Luka 22:28-30; Ufunuo 5:9, 10) Wanadamu wengi duniani watafufuliwa ili waishi katika paradiso duniani.—Zaburi 37:11, 29.
Biblia ina sababu nzuri za kutotaja kwamba kuna mbingu kwa ajili ya wanyama vipenzi au mbingu kwa ajili ya mbwa. Wanyama hawawezi kuchukua hatua zinazohitajiwa kustahili kupata “mwito wa mbinguni.” (Waebrania 3:1) Hatua hizo zinatia ndani kupata ujuzi, kuonyesha imani, na kutii amri za Mungu. (Mathayo 19:17; Yohana 3:16; 17:3) Ni wanadamu tu walioumbwa wakiwa na taraja la kuishi milele.—Mwanzo 2:16, 17; 3:22, 23.
Ili waende mbinguni, viumbe duniani wanahitaji kufufuliwa. (1 Wakorintho 15:42) Biblia ina masimulizi kadhaa yanayohusu ufufuo. (1 Wafalme 17:17-24; 2 Wafalme 4:32-37; 13:20, 21; Luka 7:11-15; 8:41, 42, 49-56; Yohana 11:38-44; Matendo 9:36-42; 20:7-12) Hata hivyo, kila mmoja aliyefufuliwa alikuwa mwanadamu, bali si mnyama.