Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr25 Mwezi wa 7 uku. 1-13
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2025
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 7-13/7
  • TAREHE 14-20/7
  • TAREHE 21-27/7
  • TAREHE 28/7–3/8
  • TAREHE 4-10/8
  • TAREHE 11-17/8
  • TAREHE 18-24/8
  • TAREHE 25-31/8
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2025
mwbr25 Mwezi wa 7 uku. 1-13

Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

© 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania

TAREHE 7-13/7

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 21

Mashauri ya Hekima Juu ya Kuwa na Ndoa Yenye Furaha

w24.05 uku. 30 fu. 13

Urafiki Wenu wa Kimapenzi Uwasaidie Kukamata Uamuzi Muzuri

13 Urafiki wenu wa kimapenzi unapaswa kuwa na urefu gani? Kukamata maamuzi haraka-haraka kunaletaka matokeo ya mubaya. (Mez. 21:5) Kwa hiyo, uhusiano wa kimapenzi unapaswa kukamata wakati wa kutosha ili mujuane muzuri. Lakini haupaswe kuwa murefu sana bila sababu. Biblia inasema hivi: “Tazamio lenye kucheleweshwa linafanya moyo ugonjwe.” (Mez. 13:12) Zaidi ya ile, kadiri munapitisha wakati mingi pamoya, inaweza kuwa nguvu kuzuia tamaa yenu ya ngono. (1 Ko. 7:9) Kuliko kukazia akili muda wenye mumefanya mu uhusiano wenu wa kimapenzi, ujiulize hivi: ‘Ni mambo gani ingine yenye ni lazima nijue juu ya mwenzangu ili niweze kukamata uamuzi?’

g-SW 7/08 uku. 7 fu. 2

Jinsi ya Kuwa na Ndoa Yenye Mafanikio

Onyesha unyenyekevu. ‘Usifanye jambo lolote kwa ugomvi au kwa kujisifu, bali kwa unyenyekevu wa akili ukiwaona wengine kuwa ni bora.’ (Wafilipi 2:3) Ugomvi mwingi hutokea kwa sababu badala ya kujinyenyekeza na kutafuta njia za kuboresha hali, kiburi huwafanya watu walaumu wenzi wao matatizo yanapotokea katika ndoa. Unyenyekevu wa akili unaweza kukusaidia usisisitize kwamba wewe ndiye uko sawa ugomvi unapotokea.

w06-SW 15/9 uku. 28 fu. 13

‘Shangilia Pamoja na Mke wa Ujana Wako’

13 Namna gani ndoa ikikabiliwa na mkazo kwa sababu ya vile wenzi wanavyotendeana? Jitihada zinahitajiwa ili kupata suluhisho. Tuseme wenzi wa ndoa walianza kuzungumziana kwa maneno yasiyo ya fadhili, na sasa wamezoea kufanya hivyo. (Methali 12:18) Kama ilivyozungumziwa katika makala iliyotangulia, hilo linaweza kuwa na matokeo mabaya. Methali moja ya Biblia inasema hivi: “Ni afadhali kukaa nyikani kuliko kukaa pamoja na mke mgomvi pamoja na uchokozi.” (Methali 21:19) Ikiwa wewe ni mke katika ndoa ya aina hiyo, jiulize hivi: ‘Je, mtazamo wangu unafanya iwe vigumu kwa mume wangu kuwa pamoja nami?’ Biblia inawaambia waume hivi: “Endeleeni kuwapenda wake zenu nanyi msiwakasirikie kwa uchungu.” (Wakolosai 3:19) Ikiwa wewe ni mume, jiulize hivi: ‘Je, nimekosa huruma na hivyo kumshawishi mke wangu kutafuta faraja mahali pengine?’ Bila shaka, hakuna kisingizio cha kufanya uzinzi. Hata hivyo, kwa kuwa msiba huo unaweza kutokea, hiyo ni sababu nzuri ya kuzungumzia matatizo waziwazi.

Mali ya Kiroho

w21.10 uku. 12 fu. 16

Tunatumikia Mungu Mwenye Iko “Tajiri Katika Rehema”

16 Wakristo wote wanajikaza kuiga rehema ya Yehova. Juu ya nini? Sababu moja ni kwamba, Yehova hatasikiliza sala za wale wenye wanakatala kuonyesha wengine rehema. (Soma Mezali 21:13.) Hakuna mutu kati yetu mwenye atapenda Yehova akatale kusikiliza sala zake. Njo maana tunajikaza sana ili kuepuka roho ya mubaya. Kuliko kukatala kusikiliza Mukristo mwenye iko mu magumu, tunapaswa kuwa tayari kila wakati ili kusikiliza “kilio cha mutu wa hali ya chini.” Vilevile pia, tunakamata kwa uzito hii maneno yenye iliongozwa na roho ya Mungu: “Ule mwenye hazoee kuonyesha rehema atapata hukumu yake bila rehema.” (Yak. 2:13) Kama kwa unyenyekevu tunakumbuka kama siye wote tuko na lazima ya rehema, ile itatusaidia pia kuonyesha rehema. Tunapenda zaidi sana kuonyesha rehema wakati mutenda-zambi mwenye anatubu, anarudia katika kutaniko.

TAREHE 14-20/7

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 22

Mashauri ya Hekima Juu ya Kukomalisha Batoto

w20.10 uku. 27 fu. 7

Watoto Wako Watamutumikia Yehova Wakati Watakoma?

7 Bibi na bwana wenye wanapenda kuwa na watoto, wanapaswa kujiuliza hivi: ‘Kama Yosefu na Maria, tuko watu wenye kumupenda Yehova na Neno lake, wenye Yehova anaweza kuchagua ili kukomalisha mutoto?’ (Zb. 127:3, 4) Wazazi wanapaswa kujiuliza hivi: ‘Tuko tunafundisha watoto wetu kama kutumika sana ni jambo la maana?’ (Muh. 3:12, 13) ‘Tuko tunalinda watoto wetu wasipatwe na mambo ya mubaya mu ulimwengu wa Shetani?’ (Mez. 22:3) Kwa kweli, hata kama munajikaza sana ili kulinda watoto wenu, wakati fulani wanaweza kupata magumu. Lakini kama munaendelea kuwatayarisha kwa kuwafundisha kwa upendo, watajua kama wakati wanapata magumu wanapaswa kutafuta mashauri mu Biblia. (Soma Mezali 2:1-6.) Kwa mufano, kama mutu fulani wa familia anaacha kumutumikia Yehova, utumie Biblia ili kusaidia watoto wako wajue juu ya nini ni jambo la maana waendelee kubakia washikamanifu kwa Yehova. (Zb. 31:23) Ao kama mutu fulani mwenye wanapenda anakufa, uwaonyeshe maandiko fulani ya Biblia yenye inaweza kuwasaidia wapiganishe huzuni yao na wakuwe na amani.​—2 Ko. 1:3, 4; 2 Ti. 3:16.

w19.12 uku. 26 fu. 17-19

Wazazi, Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova

17 Anza kufundisha watoto wakati wangali wadogo sana. Wazazi watapata matokeo ya muzuri zaidi kama wanaanza kufundisha watoto wao wakati wangali wadogo sana. (Mez. 22:6) Fikiria mufano wa Timoteo, mwenye kisha wakati fulani, alianza kusafiri pamoja na mutume Paulo. Eunike, mama ya Timoteo, na Loisi, tate (ao nkambo) yake walimufundisha “tangu utoto.”​—2 Ti. 1:5; 3:15.

18 Jean-Claude na Peace, bwana mwingine na bibi yake mu inchi ya Cote d’Ivoire, waliweza kufundisha watoto wao wote sita wamupende Yehova na kumutumikia. Ni nini iliwasaidia waweze kufanya vile? Walifuata mufano wa Eunike na Loisi. Wanasema hivi: “Tulikazia Neno la Mungu katika watoto wetu tangu utoto, muda mufupi tu kisha wao kuzaliwa.”​—Kum. 6:6, 7.

19 “Kukazia” Neno la Yehova katika watoto wako, maana yake nini? “Kukazia” maana yake “kufundisha na kukumbusha kwa kurudilia-rudilia.” Ili kufanya vile, wazazi wanapaswa kupitisha wakati kwa ukawaida pamoja na watoto wao. Wakati fulani, wazazi wanaweza kuvunjika moyo juu wanapaswa kurudiliarudilia maagizo ya Yehova kwa watoto wao. Hata hivyo, wazazi wanapaswa kujikaza kuona kama ile njo njia ya kusai-dia watoto wao waelewe Neno la Mungu na kulitumia.

w06-SW 1/4 uku. 9 fu. 4

Wazazi​—Iweni Vielelezo Bora kwa Watoto Wenu

Bila shaka, watoto ni watoto, na wengine wao wana mwelekeo wa ukaidi, na hata wa kuasi. (Mwanzo 8:21) Wazazi wanaweza kufanya nini? Biblia inasema hivi: “Ujinga umefungwa pamoja na moyo wa mvulana; fimbo ya nidhamu ndiyo itakayouondolea mbali.” (Methali 22:15) Wengine wana maoni ya kwamba kutumia fimbo ni kumnyanyasa mtoto na kwamba jambo hilo limepitwa na wakati. Ni kweli kwamba Biblia inapinga jeuri ya aina yoyote. Ingawa wakati mwingine “fimbo” hiyo humaanisha mamlaka ya wazazi ya kutia adhabu kwa uthabiti, adhabu hiyo inapaswa kutolewa kwa upendo na kwa njia inayofaa kwa kufikiria faida za milele za watoto.​—Waebrania 12:7-11.

Mali ya Kiroho

w21.08 uku. 22 fu. 11

Furahia Mambo Unaweza Kufanya Kwa Ajili ya Yehova

11 Vilevile, tunaweza kuongeza furaha yetu kwa kujikaza kufanya mambo yote yenye wametupatia kufanya mu utumishi wa Yehova. ‘Uhangaikie sana’ kazi ya kuhubiri, na ujikaze kutumika sana pamoja na kutaniko. (Mdo. 18:5; Ebr. 10:24, 25) Ujitayarishe muzuri kwa ajili ya mikutano juu utoe maelezo yenye kutia moyo. Ukamate kwa uzito migao yote yenye uko nayo ku mukutano wa katikati ya juma. Kama unaombwa kusaidia mu kazi fulani mu kutaniko, ukuwe tayari kuifanya kwa wakati. Usiwaze kama kazi yenye unapewa haiko ya maana sana na kama haiko lazima upitishe wakati wako juu ya kuifanya. Ujikaze kukomalisha ufundi wako. (Mez. 22:29) Kadiri unajikaza kumutumikia Yehova, ni vile urafiki wako pamoja naye utaongezeka na ni vile utakuwa na furaha. (Gal. 6:4) Itakuwa pia mwepesi kwako kufurahi pamoja na wengine wakati wanapata madaraka yenye pengineungependa kupata.​—Ro. 12:15; Gal. 5:26.

Hotuba: Nilishavunja Sheria ya Familia​—Nifanye Nini Sasa?

ijwyp habari ya 100

Nilishavunja Sheria ya Familia​—Nifanye Nini Sasa?

Karibu mu kila familia muko sheria. Kwa mufano, kuko sheria yenye inakuonyesha saa yenye unapaswa kurudia ku nyumba, namna unapaswa kutumia vyombo vya kielektroniki, na namna ya kutendea wengine.

Utafanya nini kama unavunja sheria moja ya familia yenu? Hauwezi kubadilisha jambo yenye ilishatokea. Lakini kuko kitu unaweza kufanya juu mambo isiharibike zaidi. Hii habari itakuonyesha mambo ya kufanya.

Jambo yenye haupaswe kufanya

Ikiwa wazazi wako hawajue kama ulivunja sheria fulani, pengine utapenda kuwaficha.

Kama wanajua, utapenda kujitetea ao kutupia mutu mwingine ile kosa.

Ile yote haiko muzuri. Juu ya nini? Kuficha mambo yenye ulifanya ao kujitetea-tetea, ni kutenda sawa mutoto. Na inaonyesha wazazi wako kama hauyakomala.

“Kusema uongo haisaidiake hata kidogo. Bipande bishuke, mambo yenye ulifanya itajulikana. Na malipizi yenye watakupatia itakuwa ya nguvu kupite ile yenye wangekupatia kama ungesema kweli ku mwanzo.”​—Diana.

Namna muzuri ya kufanya

Itika mambo yenye ulifanya. Biblia inasema: “Mwenye anafunika makosa yake hatafanikiwa.” (Mezali 28:13) Wazazi wako wanajua kama haukamilike, wanapenda tu ukuwe nasema kweli.

“Wazazi wako watakuwa tayari kukusamehe kama unasema kweli. Kama unasemaka kweli watakutumainia sana.”​—Olivia.

Omba musamaha. Biblia inasema: “Muvae unyenyekevu.” (1 Petro 5:5) Inaomba kuwa munyenyekevu juu ufikie kusema “unisamehe” bila kujitetea-tetea.

“Watu wenye wanaendelea kujitetea-tetea wanaweza kuharibisha zamiri yao. Na wakati zamiri inaharibika, haitakusumbua tena hata wakati unafanya jambo ingine ya mubaya.”​—Heather.

Itika mashauri ao malipizi yenye watakupatia. Biblia inasema: “Musikilize nizamu (ao malipizi).” (Mezali 8:33) Acha kujitetea-tetea, na uitike mashauri ao malipizi yenye wazazi watakupatia.

“Ukilaumu wazazi juu wanakupatia malipizi fulani, utafanya mambo ikuwe nguvu tena zaidi. Itika tu vizuizi vyenye wanakutilia, usikaze akili juu ya mambo yenye hautaweza kufanya juu ya vile vizuizi.”​—Jason.

Fanya nguvu juu wakutumainie tena. Biblia inasema: ‘Muondoe utu wa zamani wenye unapatana na mwenendo wenu wa zamani.” (Waefeso 4:22) Kamata maamuzi ya hekima juu wazazi wako wakutumainie tena.

“Kama unaendelea kukamata maamuzi ya hekima na kuonyesha wazazi wako kama hautafanya tena ile makosa, watakutumainia tena.”​—Karen.

SHAURI: Fanya mambo mingi zaidi ya ile yenye walikuomba, ile itawasaidia wakutumainie tena sana. Kwa mufano, wakati uko unarudia kutoka kwenye ulienda, uwaite ku telefone na kuwaonyesha kama uko mu njia, hata kama hauyapitisha saa ya kurudia ku nyumba. Ile itawasaidia wajue kama unapenda wakutumainie tena.

TAREHE 21-27/7

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 23

Mashauri ya Hekima Juu ya Pombe

lff somo ya 43 nukta ya 2

Wakristo Wanapaswa Kuwa na Mawazo Gani Juu ya Pombe?

Yehova anakataza kunywa sana na kulewa. (Wagalatia 5:21) Neno yake Biblia inasema hivi: “Usikuwe kati ya wale wenye kunywa divai nyingi sana.” (Mezali 23:20) Njo maana, kama tunaamua kunywa pombe, hata wakati tuko siye peke, hatupaswe kunywa sana mupaka akili yetu inaacha kutumika muzuri, tunaanza kusema na kutenda ovyo-ovyo, ao mupaka tunaharibisha afya yetu. Kama hatutaweza kujizuia, ni muzuri tusikuwe nakunywa hata kidogo

w23.12 uku. 14 fu. 4

Uone Pombe Vile Mungu Anaiona

Lakini Wakristo wako na muongozo wenye hekima wa Muumbaji wao mwenye upendo. Kwa mufano, Mungu ametuonya juu ya matokeo ya mubaya ya kunywa pombe sana. Pengine ulishakasoma Mezali 23:29-35 yenye inazungumuzia namna mutu mwenye anakunywa pombe sana anapata matokeo ya mubaya. Daniel, muzee Mukristo katika Ulaya, anakumbuka vile maisha yake ilikuwa mbele akuwe Mukristo wa kweli, anasema hivi: “Kunywa pombe sana kulinifanya nikamate maamuzi ya mubaya na nikutane na mambo ya mubaya sana mu maisha yangu. Na wakati ninafikiria ile mambo najisikia mubaya sana.”

Mali ya Kiroho

w04 1/11 uku. 31 fu. 2

Maulizo ya Basomaji Yetu

Kunenepa sana (ao obesité) inaweza kuwa alama ya bulafi, lakini haiko kila kunenepa sana njo bulafi. Mutu anaweza kuwa munene sana pengine juu ya magonjwa. Na ingine bunene ni ya mu kizazi tu. Tusisahau pia kama kunenepa sana ni mu mwili, lakini bulafi ni mu akili. Mutu mwenye kunenepa sana anakuwaka njo na mafuta mingi mu mwili. Lakini mutu mulafi ni mwenye anapendaka chakula kupita kiasi. Njo maana, haiko bunene njo inaonyeshaka kama mutu ni mulafi. Namna mutu anaonaka chakula njo inaonyeshaka kama ni mulafi ao hapana. Mutu anaweza kuwa mwembamba ao hata mwembamba sana na kumbe ni mulafi. Tena, mawazo ya batu juu ya bunene ao bwembamba iko tofauti mu maeneo mbalimbali. Mu eneo fulani batu banaweza kuona kama mutu iko munene lakini mu eneo ingine banaona kama iko tu sawa.

TAREHE 28/7–3/8

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 24

Ujitayarishe Juu ya Kupambana na Magumu

it-2 uku. 563 fu. 4

Kuteswa juu ya Imani

Kujua muzuri tumaini ya ufufuo na kumujua muzuri ule mwenye anatupatia ile tumaini kunatusaidia tukuwe na nguvu. Ile ujuzi inatusaidia pia tuendelee kuwa bashikamanifu kwa Mungu hata wakati batu benye kutupinga banatuambia kama batatuua.

w21.02 uku. 30-31 fu. 17-19

Namna ya Kuendelea Kuwa na Furaha Wakati wa Majaribu

17 Tatizo: Kuvunjika moyo. Neno la Mungu linasema hivi: “Kama unavunjika moyo siku ya taabu, nguvu zako zitakuwa kidogo.” (Mez. 24:10) Neno la Kiebrania lenye linatafsiriwa ‘kuvunjika moyo’ linaweza kumaanisha “kupoteza uhodari.” Ikiwa unapoteza uhodari, bila kukawia utapoteza pia furaha.

18 Jambo la kufanya: Umuombe Yehova akupatie uhodari ili uvumilie. Tuko na lazima ya uhodari ili tuvumilie majaribu. (Yak. 5:11) Neno lenye Yakobo alitumia lenye linatafsiriwa “uvumilivu” linaleta wazo la mutu mwenye anaendelea kusimama fasi kwenye iko. Tunaweza kufikiria askari mwenye, bila kuogopa, anaendelea kusimama fasi kwenye iko na hakimbie wakati maadui wanamushambulia.

19 Mutume Paulo alituwekea mufano muzuri wa uhodari na uvumilivu. Wakati fulani, alijisikia kuwa zaifu. Lakini, aliweza kuvumilia kwa sababu alimuomba Yehova amupatie nguvu yenye alikuwa nayo lazima. (2 Ko. 12:8-10; Flp. 4:13) Sisi pia tunaweza kuwa na nguvu na uhodari kama yeye ikiwa kwa unyenyekevu tunamuomba Yehova atusaidie.​—Yak. 4:10.

w20.12 uku. 15

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Mezali 24:16 inasema hivi: “Mwenye haki anaweza kuanguka mara saba (7), na atasimama tena.” Ile maneno inahusu mutu mwenye kufanya zambi tena na tena na kisha Mungu anamusamehe?

Haiko vile. Ile maneno inahusu mutu mwenye anaanguka, ni kusema, anapata magumu mingi na kisha anasimama, ni kusema, anavumilia ile magumu.

Kwa hiyo, ile mambo yote inaonyesha kama andiko la Mezali 24:16 halizungumuzie mutu mwenye anaanguka katika zambi, lakini linazungumuzia mutu mwenye anapata magumu ao matatizo, pengine hata mara kwa mara. Mu ulimwengu huu muovu, mwenye haki anaweza kupambana na matatizo ya afya ao matatizo ingine. Anaweza hata kuteswa sana na wakubwa wa serikali. Lakini anaweza kuwa hakika kama Mungu atamutegemeza na kumusaidia ili aweze kupambana na ile magumu na kuivumilia. Fikiria mambo yenye umejionea yenye kuonyesha kama kila mara watu wa Mungu wanakuwaka wanafanikiwa. Juu ya nini tunakuwaka tunafanikiwa? Tuko hakika kama “Yehova anategemeza wale wote wenye kuanguka na anasimamisha wale wote wenye kuinama chini.”​—Zb 41:1-3; 145:14-19.

Mali ya Kiroho

w09 15/10 uku. 12

Maulizo ya Basomaji Yetu

Mu wakati ya zamani, kama mwanaume anapenda ‘kujenga nyumba yake,’ ni kusema kuoa juu ya kuanzisha familia, alipaswa kujiuliza kama iko tayari kuhangaikia bibi na batoto benye banaweza kufikia kuzala. Mbele ya kuanzisha familia, alipaswa kutumika nguvu sana mu mashamba yake. Ile kanuni ingali ya maana leo?

Ndiyo. Mwanaume mwenye anapenda kuoa anapaswa kujitayarisha muzuri juu ya ile daraka. Kama hana matatizo ya afya, itaomba akuwe natumika. Lakini, kutumika kwa bidii haiko tu kuhangaikia mahitaji ya kimwili ya familia yake. Biblia inaonyesha kama mutu mwenye hahangaikie mahitaji ya kimwili, ya kiakili, na ya kiroho ya familia yake ni mubaya kushinda hata mwenye hana imani! (1 Tim. 5:8) Njo maana, kijana mwenye iko najitayarisha juu ya kuoa na kuanzisha familia anapaswa kujiuliza hii maulizo: ‘Niko tayari kwa kiasi fulani, juu ya kutimiza mahitaji ya kimwili ya familia yangu? Niko tayari juu ya kutimiza mahitaji ya kiroho ya familia yangu? Nitaweza kukuwa najifunza Biblia pamoya na bibi yangu na batoto yangu?’ Neno ya Mungu inaonyesha kama ile ni mambo ya maana sana yenye mwanaume anapaswa kutimizia familia yake.​—Kum. 6:6-8; Efe. 6:4.

Njo maana kijana mwanaume mwenye iko natafuta bibi anapaswa kufikiria sana kanuni yenye kuwa mu Mezali 24:27. Vilevile, kijana mwanamuke anapaswa kujiuliza kama iko tayari kabisa juu ya kutimiza daraka ya kuwa bibi na pia mama. Bibi na bwana benye habayakuwa na batoto banapaswa kujiuliza pia maulizo ya vile mbele ya kuamua kama batazala batoto ao hapana. (Lu. 14:28) Kutumikisha hii mashauri kunaweza kusaidia batumishi ya Mungu baepuke huzuni ya mingi na bafurahie maisha ya muzuri ya familia.

TAREHE 4-10/8

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 25

Mashauri ya Hekima Juu ya Kusema

w15 15/12 uku. 18 fu. 6-7

Utumie Muzuri Uwezo wa Ulimi Wako

6 Sababu gani ni jambo la maana tuchague wakati wenye kufaa ili kusema? Andiko la Methali 25:11 linasema hivi: ‘Neno linalosemwa wakati unaofaa ni kama matunda ya mutofaa ya zahabu kwenye chombo cha feza kilichopambwa.’ Matunda ya mutofaa (pommes) ya zahabu ni yenye kupendeza sana, lakini inaweza kupendeza zaidi wakati inatiwa kwenye chombo cha feza. Vilevile, tunaweza kuwa na jambo fulani nzuri la kumuambia mutu fulani. Lakini, ikiwa tunachagua wakati wenye kufaa ili kusema, tunaweza kumusaidia zaidi. Namna gani tunaweza kufanya hivyo?

7 Ikiwa hatuchague wakati wenye kufaa, watu wanaweza kukosa kuelewa mambo yenye tunasema ao kuikubali. (Soma Methali 15:23.) Kwa mufano, katika Mwezi wa 3, 2011, tetemeko la inchi na tsunami viliharibu miji yenye kupatikana mashariki katika inchi ya Japani. Watu zaidi ya 15000 walikufa. Mashahidi wengi wa Yehova walipoteza watu wa familia na marafiki; lakini, walikuwa tayari kutumia Biblia ili kusaidia watu wengi wenye walipatwa pia na mugumu hayo. Lakini, Mashahidi wa Yehova walijua kwamba wengi kati ya watu hao wako katika dini ya Wabuda na hawajue mambo mengi juu ya Biblia. Kwa hiyo, kuliko kuzungumuza nao wakati huo juu ya ufufuo, ndugu na dada waliwatia moyo na kuwaelezea sababu gani watu wazuri wanapatwa na mambo mabaya kama hayo.

w15 15/12 uku. 20-21 fu. 15-16

Utumie Muzuri Uwezo wa Ulimi Wako

15 Namna tunaongea na wengine inaweza kuwa ya maana sana sawasawa na mambo yenye tunasema. Watu walifurahia kumusikiliza Yesu kwa sababu alisema kwa njia “yenye kuvutia sana [yenye kupendeza sana],” ao kwa upole. (Luka 4:22) Wakati tunasema kwa upole, watu wanaweza kufurahia zaidi kutusikiliza na kukubali mambo yenye tunasema. (Methali 25:15) Ikiwa tunawaheshimu wengine na kuhangaikia namna wanajisikia, hilo litatusaidia kuzungumuza nao kwa upole. Yesu alifanya hivyo. Kwa mufano, wakati aliona kikundi cha watu wanajikaza sana kumusikiliza, alifurahi sana kupitisha nao wakati na kuwafundisha. (Marko 6:34) Hata wakati watu walimutukana, Yesu hakuwarudishia matukano.​—1 Petro 2:23.

16 Hata kama tunapenda watu wa familia na marafiki wetu, tunaweza kusema nao kwa kutumia maneno yenye haifae kwa sababu tunawajua muzuri sana. Tunaweza kufikiri kwamba haiko jambo la lazima kutumia maneno yetu kwa uangalifu wakati tunazungumuza nao. Lakini, Yesu hakutumia hata kidogo maneno yenye haifae wakati alizungumuza na marafiki wake. Wakati wamoja kati yao walikuwa wanabishana ili kujua ni nani mwenye alikuwa mukubwa zaidi kati yao, aliwashauria kwa upole na alitumia mufano wa mutoto mudogo ili kuwasaidia wabadilishe mawazo yao. (Marko 9:33-37) Wazee wanaweza kuiga mufano wa Yesu kwa kutolea wengine mashauri kwa upole.​—Wagalatia 6:1.

w95-SW 1/4 uku. 17 fu. 8

Kuchochea Kwenye Upendo na Kazi Zilizo Bora​—Jinsi Gani?

8 Katika kutumikia Mungu wetu, sisi sote twaweza kuchocheana kupitia kielelezo. Kwa hakika Yesu aliwachochea wasikilizaji wake. Alipenda kazi ya huduma ya Kikristo na aliitukuza huduma. Alisema ilikuwa kama chakula kwake. (Yohana 4:34; Warumi 11:13) Idili hiyo yaweza kuwa yenye kuambukiza. Je, wewe pia waweza kudhihirisha shangwe yako katika huduma? Huku ukiepuka kwa uangalifu kuwa na mwelekeo wa kujivuna, shiriki na wengine kutanikoni maono yako mazuri. Unapoalika wengine wahubiri nawe, ona ikiwa waweza kuwasaidia wapate raha ya kweli katika kuongea na wengine juu ya Muumba wetu Mtukufu, Yehova.​—Mithali 25:25.

Mali ya Kiroho

it-1 uku. 670

Upole

Mambo yenye inasaidiaka mutu akuwe mupole ni imani na nguvu yenye Mungu anamupatiaka. Haikuwake mwepesi kwa mutu wa vile kupoteza usawaziko na uwezo wa kufikiri. Mambo yenye inafanyaka mutu asikuwe mupole ni wasiwasi, kukosa kujua bya kufanya, kukosa imani, na kupoteza tumaini. Biblia inasema hivi juu ya mutu mwenye haiko mupole: “Kama muji wenye umebomolewa, wenye hauna ukuta ni vile pia mutu mwenye hawezi kuzuia kasirani yake.” (Mez 25:28) Ile maneno inaonyesha kama inakuwaka mwepesi kwa mutu mwenye haiko mupole kuanza kuwa na mawazo ya mubaya, na ile inaweza kumuchochea atende mu njia yenye haiko sawa.

Hotuba: Nifanye Nini Kama Batu Biko Nanisema Mubaya?

ijwyp-SW habari ya 23

Nifanye Nini Ikiwa Watu Wanaeneza Porojo Kunihusu?

Kwa nini porojo inadhuru

Porojo fulani hutolewa kwa nia mbaya​—kwa mfano, mtu akisema uwongo kimakusudi ili akuchafulie jina. Hata ikiwa mtu anaeneza porojo ambayo haihusu jambo zito, porojo hiyo inaweza kumuumiza mwingine hisia​—hasa ikienezwa na mtu uliyemdhania kuwa rafiki yako wa karibu sana!​—Zaburi 55:12-14.

“Niligundua kwamba rafiki yangu alikuwa akieneza porojo kunihusu, akisema kwamba mimi siwajali wengine. Jambo hilo liliniumiza sana! Nilishindwa kuelewa kwa nini alisema jambo kama hilo.”​—Ashley.

Ukweli wa Mambo: Iwe yule anayeeneza porojo kukuhusu ni rafiki yako au la, haipendezi hata kidogo unapojua kwamba watu wamekuwa wakisema mambo mabaya kukuhusu.

Jambo baya ni kwamba​—huwezi kuzuia porojo

Watu wanaweza kueneza porojo kwa sababu kadhaa, kutia ndani sababu hizi:

Upendezi wa kweli. Wanadamu ni viumbe wanaopenda kuchangamana na wengine. Kwa hiyo ni jambo la kiasili kuzungumza kuhusu kitu au mtu fulani. Biblia yenyewe hututia moyo tuangalie “faida za kibinafsi” za wengine.​—Wafilipi 2:4.

“Kwa kawaida, kuzungumza kuhusu watu ndiyo mada inayosisimua zaidi!”​—Bianca.

“Lazima nikiri kwamba ninapenda sana kujua mambo ambayo wengine wanafanya na kuzungumzia mambo hayo na watu wengine. Sijui ni kwa nini​—inasisimua tu.”​—Katie.

Kukosa jambo la kufanya. Katika nyakati za Biblia, kulikuwa na watu ambao “hawakuwa wakitumia wakati wao wa starehe wakifanya chochote ila kuambiana jambo au kusikiliza jambo jipya.” (Matendo 17:21) Hivyo ndivyo ilivyo leo!

“Hata wakati ambapo hakuna lolote la kuchangamsha, watu hubuni jambo fulani ili wawe na kitu cha kuzungumzia.”​—Joanna.

Kutojiamini. Biblia ina sababu nzuri ya kutuonya dhidi ya mwelekeo wa kujilinganisha na wengine. (Wagalatia 6:4) Jambo la kusikitisha ni kwamba, watu wengine hukabiliana na tatizo la kutojiamini walilo nalo kwa kueneza habari mbaya kuwahusu wengine.

“Mtu anayeeneza porojo hufunua jambo fulani kuhusu jinsi alivyo. Mara nyingi inafunua kwamba ana wivu na ndio maana anaeneza habari mbaya kuhusu mtu mwingine. Anaeneza porojo hiyo ili tu ajihisi vizuri na ajisadikishie mwenyewe kwamba yeye ni bora kuliko yule mwingine.”​—Phil.

Ukweli wa mambo: Upende usipende, watu watazungumza kuhusu watu wengine​—kutia ndani wewe.

Jambo zuri ni kwamba​—si lazima porojo ikudhoofishe hisia

Huenda usifaulu kabisa kuwazuia watu kueneza porojo kukuhusu, hata hivyo unaweza kuchagua jinsi utakavyoitikia ukigundua kwamba mtu fulani ameeneza porojo kukuhusu. Ukigundua kwamba habari fulani kukuhusu imeenea, kuna angalau mambo mawili unayoweza kufanya.

JAMBO LA 1: Puuza. Mara nyingi kupuuza jambo fulani ndio uamuzi bora kabisa​—hasa ikiwa habari zilizoenezwa ni za upuuzi. Fuata ushauri huu wa Biblia: “Usiwe na haraka kuudhika katika roho yako.”​—Mhubiri 7:9.

“Habari zilienea kuwa nilikuwa nikimchumbia mvulana fulani​—mtu ambaye hata sikuwahi kukutana naye! Ulikuwa upuuzi mtupu na kwa hiyo niliamua kuupuza.”​—Elise.

“Ukiwa na sifa nzuri ni rahisi kwako kukabiliana na porojo. Hata habari mbaya zikienezwa kukuhusu, ni watu wachache watakaoziamini, kwa sababu wanajua kwamba una sifa nzuri. Zitakusaidia uendelee kudumisha hadhi yako.”​—Allison.

Dokezo: Andika (1) jambo ambalo lilienezwa kukuhusu na (2) jinsi ulivyohisi. ‘Ukishasema moyoni mwako,’ huenda ukatambua kwamba ni rahisi zaidi kuamua kulipuuza au kulisahau jambo hilo.​—Zaburi 4:4.

JAMBO LA 2: Mfikie mtu aliyeanzisha porojo hiyo. Katika visa fulani huenda ukahisi kwamba habari mbaya sana kukuhusu imeenezwa hivi kwamba ukaamua kuchukua hatua ya kumfikia yule aliyeianzisha.

“Unapowafikia watu wanaoeneza porojo kukuhusu, huenda ukawasaidia watambue kwamba hatimaye mambo wanayosema humfikia mtu wanayeeneza habari zake. Hilo huenda likakusaidia ujisafishie jina au hata kusuluhisha tatizo lenyewe.”​—Elise.

Kabla ya kumfikia mtu anayeeneza porojo kukuhusu, fikiria kanuni zifuatazo za Biblia na ujiulize maswali yaliyoambatanishwa na kanuni hizo.

“Yeyote anapojibu jambo kabla ya kulisikia, huo ni upumbavu na aibu kwake.” (Methali 18:13) ‘Je, nina habari zote zinazohusika? Je, inawezekana kwamba mtu aliyeniletea porojo hizo hakuelewa vizuri mambo aliyosikia?’

‘Uwe mwepesi wa kusikia, si mwepesi wa kusema, si mwepesi wa ghadhabu.’ (Yakobo 1:19) ‘Je, huu ndio wakati unaofaa wa kumfikia mtu anayeeneza porojo kunihusu? Je, nina uhakika kwamba ninatumia njia inayofaa kusuluhisha jambo hilo? Au ni afadhali zaidi nisubiri wakati fulani upite ili hisia zangu zitulie?’

“Chochote ambacho mngetaka mtendewe na watu, ninyi nanyi watendeeni vivyo hivyo.” (Mathayo 7:12, Holy Bible) ‘Ikiwa ningekuwa nimeeneza porojo kumhusu mtu mwingine, ningetaka mtu huyo anifikie kwa njia gani? Ningependa tuzungumzie tatizo hilo chini ya hali gani? Ningependa atumie maneno ya aina gani na azungumze kwa njia gani?’

Dokezo: Kabla ya kumfikia yule anayeeneza porojo kukuhusu, andika mambo utakayomwambia. Kisha subiri juma moja au mawili, halafu urudie mambo uliyoandika uone kama kuna mabadiliko yoyote unayohitaji kufanya. Kisha zungumzia mambo hayo na mzazi wako au rafiki mkomavu na umwombe mashauri.

Ukweli wa mambo: Kama ilivyo na mambo mengi maishani, huwezi kuwazuia watu wasieneze porojo. Lakini hilo halimaanishi kwamba ni lazima porojo ikudhibiti!

TAREHE 11-17/8

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 26

Ukuwe Mbali na “Mujinga”

it-2 uku. 602 fu. 1

Mvua

Bipindi. Mu Inchi ya Ahadi muko bipindi biwili bikubwa bya wakati, kipindi ya joto na kipindi ya baridi. Bile bipindi biwili binaweza kufananishwa na kipindi ya kipwa na kipindi ya mvua. (Linganisha na Zb 32:4; Wim 2:11, maelezo ya chini.) Mvua kidogo sana inanyeshaka kuanzia katikati ya Mwezi wa 4 mupaka katikati ya Mwezi wa 10. Ile njo inakuwaka kipindi ya mavuno na mvua hainyeshake tu sana. Mezali 26:1 inaonyesha kama haikuwa jambo ya kawaida kuona mvua inanyesha mu wakati ya mavuno. (Linganisha na 1Sa 12:17-19.) Mu kipindi ya mvua, mvua inanyeshaka masiku moya na ingine masiku haitanyesha. Juu ile wakati inakuwaka kipindi ya baridi, kulobana na mvua inafanyaka mutu asikie tena baridi sana. (Ezr 10:9, 13) Njo maana, mu ile hali mutu anakuwaka kabisa na lazima ya fasi ya kujificha.​—Isa 4:6; 25:4; 32:2; Yob 24:8.

w87-SW 1/10 uku. 19 fu. 12

Nidhamu Inazaa Tunda Lenye Kuamanika

12 Huenda hatua za nguvu zaidi zikahitajiwa kabisa kuchukuliwa kwa watu fulani, kama vile Mithali 26:3 (NW) inavyoonyesha: “Kiboko ni kwa ajili ya farasi, lijamu ni kwa ajili ya punda, na fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa watu wapumbavu.” Nyakati nyingine Yehova aliacha taifa lake la Israeli litiishwe na taabu ambazo wao walileta juu yao wenyewe “kwa sababu waliyaasi maneno ya Mungu, wakalidharau shauri lake Aliye juu. Hata akawadhili moyo kwa taabu, wakajikwaa wala hakuna msaidizi. Wakamlilia BWANA [Yehova, NW] katika dhiki zao, akawaponya na shida zao.” (Zaburi 107:11-13) Hata hivyo, wapumbavu fulani wanajifanya wagumu kwa kadiri ambayo hawawezi kufikiwa na aina yo yote ya nidhamu inayoponya: “Mtu mwenye kukaripiwa kwa kurudia-rudia lakini anafanya shingo yake ngumu atavunjwa kwa ghafula, na hilo bila maponyo.”​—Mithali 29:1, NW.

it-1 uku. 357 fu. 3

Kilema, Ulemavu

Sulemani, mufalme mwenye hekima, alisemaka hivi: “Kama mutu mwenye anajivunja miguu yake mwenyewe na kujiumiza mwenyewe, ni vile pia mutu mwenye anatia mambo katika mikono ya mujinga.” Kama mutu anajivunja migulu, anaweza kufikia kuwa kilema. Njo vile inakuwaka kama mutu anapatia mujinga kazi ya kusimamia. Kufanya vile ni kujiumiza tu weye peke juu ile kazi haitaendelea muzuri.​—Mez 26:6.

Mali ya Kiroho

it-2 uku. 1006

Mujinga

Mezali 26:4 inatushauria ‘tusimujibie mujinga kulingana na upumbavu wake.’ Ile maneno inaonyesha kama hatupaswe kujibia mujinga kwa kutumia maneno yenye kukosa heshima sawa yeye. Juu kama tunafanya vile, tutajishushia tu heshima na itaonekana sawa vile na siye tuko bajinga. Lakini Mezali 26:5 inasema kama tunapaswa kumujibia mujinga “kulingana na upumbavu wake.” Ni kusema, tunapaswa kufikiri naye kwa kutumia maneno yenye alisema juu ya kumusaidia afikie kuelewa kama byenye alisema habiko sawa.

TAREHE 18-24/8

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 27

Namna Barafiki Bazuri Banatusaidiaka

w19.09 uku. 5 fu. 12

Yehova Anaona Watumishi Wake Wanyenyekevu Kuwa wa Maana

12 Mutu munyenyekevu anaonyesha shukrani wakati anapewa shauri. Kwa mufano: Wazia uko ku mukutano wa kutaniko. Kisha kuzungumuza na ndugu na dada fulani, mumoja kati yao anakubeba pembeni na anakuambia kama uko na chakula fulani ku meno yako. Kwa kweli, hautajisikia muzuri. Lakini, utakuwa pia mwenye shukrani kuona ndugu ao dada huyo alikuambia jambo hilo. Kwa kweli, ungefurahi ikiwa mutu angekuambia vile mbele ya wakati! Vilevile, tunapaswa kuwa wanyenyekevu na wenye shukrani wakati ndugu ao dada anajikaza kutupatia shauri wakati tuko na lazima ya shauri hilo. Tunapaswa kumuona ndugu ao dada huyo kuwa rafiki yetu, hapana adui yetu.​—Soma Mezali 27:5, 6; Gal. 4:16.

it-2 uku. 669 fu. 7

Jirani

Mezali inatushauria kama tunapaswa kuaminia na kutumainia rafiki, zaidi sana wakati ya magumu. Inasema hivi: “Usimuache rafiki yako ao rafiki ya baba yako, na usiingie katika nyumba ya ndugu yako siku yenye uko na musiba;jirani wa karibu anashindia ndugu wa mbali.” (Mez 27:10) Inawezekana kama muandikaji wa hii mezali anapenda kusema kama rafiki wa karibu wa familia anaweza kutusaidia zaidi kuliko ndugu yetu mwenye kuishi mbali. Juu ndugu yetu mwenye kuwa mbali hatakuwa tayari kutusaidia ikiwa kunatokea jambo fulani.

w23.09 uku. 9 fu. 7

Vijana, Mutakuwa na Maisha ya Namna Gani?

7 Jambo moya yenye uamuzi mubaya wa Yehoashi unaweza kutufundisha ni kama tunapaswa kuchagua marafiki wenye watatuchochea kufanya mambo ya muzuri; marafiki wenye wanamupenda Yehova na wenye wanapenda kumufurahisha. Haiko lazima marafiki wetu wakuwe tu wa miaka yetu. Kumbuka kama Yehoashi alikuwa mudogo sana kuliko rafiki yake Yehoyada. Fikiria marafiki wenye uko nao kisha ujiulize hii maulizo: ‘Wananisaidia ili imani yangu kwa Yehova ikuwe nguvu zaidi? Wananitia moyo nitumikishe kanuni za Mungu mu maisha yangu? Wanazungumuzia kuhusu Yehova na kweli za Biblia? Wanaheshimia kanuni za Mungu? Wananiambia tu mambo yenye ninapenda kusikia ao wako tayari kunirekebisha kama ninafanya makosa?’ (Mez. 27:5, 6, 17) Kusema kweli, hauna lazima ya marafiki wenye hawamupendi Yehova. Lakini kama uko na marafiki wenye wanamupenda Yehova, ushikamane nao; watakusaidia sana!​—Mez. 13:20.

Mali ya Kiroho

w06 15/9 uku. 19 fu. 12

Mawazo Makubwa ya mu Kitabu ya Mezali

27:21. Namna tunakuwaka kabisa inaweza kuonekana wazi wakati banatusifia. Kama maneno yenye banatuambia juu ya kutusifia inatuchochea kuonyesha kama mambo yote yenye tunafanyaka ni Yehova njo anatusaidiaka, na kama ile maneno inatusaidia tuendelee kumutumikia, ile itaonyesha kama tuko banyenyekevu. Lakini, kama maneno yenye banatuambia juu ya kutusifia inatufanya tujione kuwa ba maana sana kuliko bengine, ile itaonyesha kama hatuko banyenyekevu.

Hotuba: Nifanye Nini Kama Rafiki Yangu Ananikosea?

ijwyp-SW habari ya 75

Nifanye Nini Rafiki Yangu Akiniumiza?

Unachopaswa kujua

Hakuna uhusiano wa wanadamu usio na matatizo. Kwa sababu si mkamilifu, huenda rafiki yako​—hata yule unayemwona kuwa rafiki wa karibu sana​—anaweza kufanya au kusema jambo ambalo litakuumiza. Bila shaka, wewe pia si mkamilifu. Kwa hiyo, ni jambo la haki kukumbuka wakati wewe ulipomuumiza mtu fulani.​—Yakobo 3:2.

Intaneti inaweza kufanya iwe rahisi kuumia. Kwa mfano, tineja anayeitwa David, alisema hivi: “Ukifungua mtandao wa kijamii na kuona picha za rafiki yako akiwa katika tafrija, unaweza kuanza kujiuliza kwa nini hukualikwa. Na kisha unaweza kuanza kuhisi umesalitiwa na ukahuzunika.”

Unaweza kujifunza kushughulikia tatizo.

Unachoweza kufanya

Jichunguze. Biblia inasema hivi: “Usikasirike haraka, kwa maana hasira ni dalili ya mjinga.”​—Mhubiri 7:9, maelezo ya chini.

“Wakati mwingine, baada ya muda unatambua kwamba jambo lililokukasirisha si kubwa sana.”​—Alyssa.

Jambo la kufikiria: Je, unakasirika haraka? Je, unaweza kujifunza kuvumilia zaidi udhaifu wa wengine?​—Mhubiri 7:21, 22.

Fikiria faida za kusamehe. Biblia inasema hivi: “Ni fahari . . . kuachilia kosa.”​—Methali 19:11.

“Hata ikiwa una sababu ya kulalamika, ni jambo jema kusamehe kwa hiari, hilo halimaanishi kumfungia kinyongo na kufanya akuombe msamaha kila wakati kwa kosa ambalo umemsamehe. Ukisamehe, lifute kabisa kosa hilo.”​—Mallory.

Jambo la kufikiria: Je, ni jambo zito sana? Je, unaweza kusamehe ili kutafuta amani?​—Wakolosai 3:13.

Wafikirie wengine. Biblia inasema hivi: “Mkiangalia, si faida zenu wenyewe, bali pia faida za wengine.”​—Wafilipi 2:4.

“Ikiwa kuna upendo na heshima katika urafiki wenu, utakuwa na sababu yenye nguvu ya kusuluhisha matatizo haraka kwa sababu umejitoa katika urafiki wenu. Tayari umetumia jitihada nyingi katika urafiki huo, na usingependa kuupoteza.”​—Nicole.

Jambo la kufikiria: Je, kuna ukweli wowote katika maoni ya rafiki yako?​—Wafilipi 2:3.

Jambo kuu: Kujua jinsi ya kushughulika na hisia zenye kuumiza ni ustadi utakaokusaidia utakapokuwa mtu mzima. Kwa nini usijifunze kuwa na ustadi huo sasa?

TAREHE 25-31/8

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 28

Tofauti Kati ya Mutu Muovu na Mutu Muzuri

w93-SW 15/5 uku. 26 fu. 2

Je! Wewe Humfuata Yehova Kikamili?

“WENYE haki ni wajasiri kama simba.” (Mithali 28:1) Wanazoea imani, wanategemea Neno la Mungu kwa uhakika, na kwenda mbele kwa ujasiri katika utumishi wa Yehova dhidi ya hatari yoyote.

it-1 uku. 1197 fu. 6

Uelewaji

Wakati mutu anaanza kuishi maisha ya uovu, hafikiriake tena mawazo ya Mungu mu maamuzi yake na mu mipango yake. (Yob 34:27) Mutu wa vile anashindwaka kuona makosa yake na hakuwake tena na uelewaji. (Zb 36:1-4) Anaweza kusema kama iko namuabudu Mungu, lakini mawazo ya banadamu njo anapendaka kuliko mawazo ya Mungu. (Isa 29:13, 14) Anakuwaka anajitetea na kusema kama matendo yake ya mubaya ni “muchezo” tu. (Mez 10:23) Anafikiaka kupotoka sana na kukuwa mupumbavu mupaka anawaza kama Mungu haonake matendo yake ya mubaya. Kwake, ni sawa vile Mungu alishapoteza uwezo wa kuona muzuri. (Zb 94:4-10; Isa 29:15, 16; Yer 10:21) Kupitia matendo yake, ni sawa vile anasema, “hakuna Yehova” (Zb 14:1-3) na anamusahau kabisa. Juu haongozwe na kanuni za Mungu, hawezi kufikiri muzuri, hawezi kuchunguza mambo yote yenye inahusika na kufikia kukamata uamuzi muzuri.​—Mez 28:5.

it-1 uku. 1195 fu. 4

Uaminifu-Mushikamanifu

Hatuwezi kuishi maisha ya uaminifu-mushikamanifu kwa nguvu yetu siye benyewe. Ni kama tunamuamini kabisa Yehova na kutumainia kama iko na uwezo wa kutuokoa njo tutaweza. (Zb 25:21) Mungu anaahidi kama atakuwa “ngao” na pia “ngome” kwa bale benye kuishi maisha ya uaminifu-mushikamanifu. (Mez 2:6-8; 10:29; Zb 41:12) Juu banafanyaka yabo yote juu baendelee kukubaliwa na Yehova, ile inabasaidiaka bakuwe benye kutulia na baendelee kutembea mu njia ya muzuri. (Zb 26:1-3; Mez 11:5; 28:18) Sawa vile Yobu alijioneaka, hata batu benye habana lawama banatesekaka na kufa juu ya mambo ya mubaya yenye kuwa mu hii dunia. Hata vile, Yehova anaonaka namna banajikazaka kuishi maisha ya muzuri na anabahakikishia kama uriti wabo hautapotea, batakuwa na amani wakati wenye kuya, na batakuwa na maisha ya muzuri. (Yob 9:20-22; Zb 37:18, 19, 37; 84:11; Mez 28:10) Sawa Yobu, haiko utajiri njo inapatiaka mutu valere. Kitu yenye inapatiaka mutu valere ya kweli, ni kuishi maisha ya uaminifu-mushikamanifu. Na ile njo inafanyaka batu bamuheshimie. (Mez 19:1; 28:6) Batoto benye biko na muzazi wa vile ni benye kubarikiwa, (Mez 20:7) juu muzazi wabo atabaachia mufano muzuri, batajulikana mu njia ya muzuri, na bataheshimiwa.

Mali ya Kiroho

w01 1/12 uku. 12 fu. 1

Unaweza Kuepuka Ugonjwa wa Moyo wa Mfano

Kujitumainia kupita kiasi. Batu bamingi benye biko na ugonjwa wa moyo balikuwaka nawaza kama biko na afya ya muzuri mbele ile jambo itokee. Mara mingi, balikuwaka hata nawaza kama haiko lazima kuenda kuonana na munganga juu ya kujua hali ya afya yabo. Vilevile, Bakristo fulani banaweza kuwaza kama juu balishafanya miaka mingi mu Bukristo, habawezi kuangukia mu zambi. Mbele hali ifikie kuwa mubaya, banaweza kuwaza kama hakuna lazima ya kukuwa najichunguza kiroho. Njo maana, ni jambo ya lazima tuendelee kukumbuka hii shauri ya mutume Paulo yenye inatusaidia tusijitumainie kupita kiasi: “Ule mwenye anawaza kama anasimama afanye angalisho asianguke.” Ni muzuri tukumbuke kama hatukamilike na tuendelee kujichunguza kiroho kila wakati.​—1 Wakorinto 10:12; Mezali 28:14.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine