Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
© 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
TAREHE 1-7/9
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 29
Katala Mafundisho na Desturi Zenye Hazipatane na Biblia
wp16.06 uku. 6, kisanduku
Maono Kuhusu Wale Wenye Kuishi Mbinguni
Kama vile wafungwa katika minyororo, mamilioni ya watu wanafungwa na mambo ya uchawi na wanaogopa sana roho waovu. Wanatafuta ulinzi katika hirizi na vitu vingine vya uchawi. Haiko lazima ufanye hivyo. Biblia inatuhakikishia jambo hili lenye kutia moyo: ‘Macho yake [Yehova] yanaenda huku na huku duniani kote ili aonyeshe nguvu zake kwa ajili ya wale ambao moyo wao ni mukamilifu kumwelekea yeye.’ (2 Mambo ya Nyakati 16:9) Yehova, Mungu wa kweli, ambaye ni mwenye nguvu nyingi sana kuliko Shetani, atakulinda ikiwa unamutegemea.
Ili Yehova akulinde, unapaswa kujua mambo yenye kumufurahisha na kufanya mambo hayo. Kwa mufano, wakati wa mitume, Wakristo wa muji wa Efeso walikusanya vitabu vyao vyote vya uchawi na kuvichoma. (Matendo 19:19, 20) Vilevile, ili Mungu akulinde, unapaswa kuachana na hirizi, vitu vyenye watu wanavaa ili “kujilinda” wasipatwe na mabaya, na vitu vingine vyenye kuwa na uhusiano na mambo ya uchawi.
Ushikamane na Kweli Juu ya Kifo
Kama uko na mashaka juu ya desturi ao mazoea fulani, usali kwa Yehova, na kumuomba akupatie hekima yake. (Soma Yakobo 1:5.) Kisha utafute habari mu vichapo vyetu. Kama ni lazima, uzungumuze na wazee wa kutaniko lenu. Hawatakuambia mambo yenye unapaswa kufanya, lakini wanaweza kukusaidia kupata kanuni za Biblia, kama zile zenye kuzungumuziwa mu habari hii. Wakati unafanya vile, unazoeza ‘nguvu zako za utambuzi,’ na nguvu hizo zitakusaidia “kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.”—Ebr. 5:14.
“Nitatembea Katika Kweli Yako”
Desturi na mazoea yenye hayamupendeze Mungu. Watu wa familia yetu, wafanyakazi wenzetu, na wanafunzi wenzetu wanaweza kutuchochea tujiunge nao ili kufanya sikukuu mbalimbali. Ni nini inaweza kutusaidia kupinga mukazo wa kufanya desturi na sikukuu zenye hazimupendeze Yehova? Tunapaswa kuendelea kukumbuka sababu zenye zinafanya Yehova asikubali sikukuu hizo. Tunaweza kutafuta habari katika vichapo vyetu na kujikumbusha namna sikukuu fulani zilianza. Wakati tunafikiri sana juu ya sababu zenye kutegemea Maandiko zenye kutuchochea tusifanye sikukuu hizo, tunakuwa hakika kama tunatembea katika njia yenye “kukubaliwa kwa Bwana.” (Efe. 5:10) Kama tunamutumainia Yehova na Neno lake, hatutaogopa mambo yenye watu wengine wanawaza juu yetu.—Mez. 29:25.
Mali ya Kiroho
it-F “Flatterie” fu. 1
Kusifu-sifu Bengine
Kusifu-sifu bengine ni kubapongeza na nia ya mubaya, ao kubasifu sana kupita kiasi. Mara mingi, mutu mwenye kusifu-sifu mwengine anajiwaziaka tu yepeke, na anapendaka kumushushia heshima ule mwenye iko nasifu na kumuharibishia sifa. Nia yake ni kupata kitu fulani kutoka kwa mwenye iko nasifu-sifu, kumufanya ajisikie kama anapaswa tu kumupatia kitu fulani juu alimusifu. Njo maana mara mingi, mutu mwenye banasifu anajikutaka tu mu wavu ao mutego wa kupana kitu fulani. (Mez 29:5)
TAREHE 8-14/9
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 30
“Usinipatie Umaskini Wala Utajiri”
Ni Upendo wa Aina Gani Wenye Kuleta Furaha ya Kweli?
Kwa kweli, sisi wote tuko na lazima ya feza. Zinatutolea ulinzi kwa kadiri fulani. (Mhu. 7:12) Lakini mutu anaweza kuwa na furaha kabisa ikiwa iko tu na feza za kutosha ili kutimiza mambo yake ya lazima? Ndiyo kabisa! (Soma Mhubiri 5:12.) Aguri mwana wa Yake aliandika hivi: ‘Usinipe umaskini wala utajiri. Acha nikule chakula nilichoamuriwa.’ Tunaweza kuelewa kabisa sababu gani hakupenda akuwe maskini sana. Kama vile alifikia kueleza, hakupenda akuwe katika jaribu la kuiba kwa sababu kuiba kunamuvunjia Mungu heshima. Lakini sababu gani alisali asipate utajiri? Aliandika hivi: “Nisije nikashiba nikakukana, nikasema: ‘Yehova ni nani?’” (Met. 30:8, 9) Pengine unajua watu wenye kutumainia mali yao kuliko kumutumainia Mungu.
Wale wenye kupenda feza hawawezi kumupendeza Mungu. Yesu alisema hivi: ‘Hakuna anayeweza kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana ama atamuchukia mumoja na kumupenda yule mwingine, ama atashikamana na mumoja na kumuzarau yule mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na Utajiri.’ Mbele ya kusema maneno hayo, alikuwa amesema kwanza hivi: ‘Muache kujiwekea hazina duniani, ambako nondo na kutu wanakula, na ambako wezi wanavunja na kuiba. Badala yake, mujiwekee hazina mbinguni, ambako nondo na kutu havikule, na ambako wezi hawavunje na kuiba.’—Mt. 6:19, 20, 24.
Wengi wametambua kama kuishi maisha mepesi kunawaletea furaha, lakini pia kunawatolea wakati mwingi zaidi wa kumutumikia Yehova. Jack, mwenye kuishi Amerika, aliuzisha nyumba yake kubwa na biashara yake kwa sababu alijua kama kufanya hivyo kungemusaidia yeye pia akuwe painia kama bibi yake. Anaeleza hivi: “Ilikuwa vigumu kuacha nyumba yetu yenye kupendeza na kiwanja chetu chenye kilikuwa mbali na muji. Lakini, kwa miaka mingi, nilikuwa ninarudia nyumbani nikiwa mwenye kuchoka akili kwa sababu ya matatizo kwenye kazi. Bibi yangu mwenye alikuwa painia wa kawaida, alikuwa na furaha sikuzote. Alikuwa anasema, ‘Ninatumikia mukubwa wa kazi muzuri zaidi!’ Kwa sababu sasa mimi pia ninafanya kazi ya upainia, sisi wawili tunatumikia Mutu uleule, ni kusema, Yehova.”
w87-SW 15/5 uku. 30 fu. 7
Mwogope Yehova Nawe Utakuwa Mwenye Furaha
◆ 30:15, 16—Ni nini maana ya mifano hii?
Hiyo inaonyesha kule kutoweza kutoshelezwa kwa pupa. Miruba hujivimbisha yenyewe kwa damu, sawa na vile watu wenye pupa sikuzote wanadai fedha na uwezo zaidi na zaidi. Vivyo hivyo, Sheoli haitosheki kamwe bali inabaki wazi kupokea wengine zaidi wanaouawa na kifo. Tumbo lisilozaa ‘hulia’ lipate watoto. (Mwanzo 30:1) Nchi iliyokumbwa na ukame hunywa maji ya mvua na upesi inaonekana kuwa imekauka tena. Na moto ambao umeteketeza vitu vilivyotupwa ndani yao unatupa miali ambayo huchoma na kumaliza vitu vingine vinavyoweza kuchomeka vilivyo karibu. Ndivyo ilivyo kwa watu wenye pupa. Lakini wale wanaoongozwa na hekima ya kimungu hawasukumwi mbele na ubinafsi wa namna hiyo bila kukoma.
Mambo ya Feza
Epuka deni zenye haziko za lazima. Kama inawezekana, uepuke deni. Kuliko kukamata deni, ukuwe unaweka feza kidogo-kidogo ili kufikia kununua kitu chenye uko nacho lazima. Kama unalazimika kujikopesha feza, ujikaze kulipa mbele ya wakati juu deni isiongezeke. Kama uko na deni, ufanye mipango ya kulipa ile deni na uiheshimie.
Mutu mwenye kuwa na tabia ya kujikopesha feza, anakuwaka pia na zoezi ya kuzitumia sana. Kwa hiyo, kama unaona ni lazima ujikopeshe, ufikiri sana mbele ya kufanya vile.
Endelea Kuwa Mugeni wa Yehova Milele!
Ni muzuri tuchunguze namna yetu ya kuona makuta. Ujiulize hivi: ‘Mara mingi ninajikutaka niko nafikiria makuta na vitu vyenye ninaweza kuuza? Kama wananikopesha makuta, ninachelewaka kulipa, na kuwaza kama mutu mwenye alinikopesha hana lazima ya ile makuta? Kuwa na makuta kunanifanya nijisikie kuwa mutu wa maana na kunanifanya nikuwe muchoyo? Ninahukumu ndugu na dada zangu kuwa wanapenda vitu vya kimwili juu tu wako na makuta? Ninafanyaka urafiki na matajiri na kuepuka maskini?’ Tuko na pendeleo kubwa sana ya kuwa wageni mu hema ya Yehova. Tunaweza kulinda ile pendeleo kwa kuendelea kuepuka kupenda makuta. Kama tunafanya vile, Yehova hatatuacha hata siku moya!—Soma Waebrania 13:5.
Mali ya Kiroho
w09 15/4 uku. 17 fu. 11-13
Hekima ya Yehova Iko Naonekana mu Uumbaji
Wibari ni kiumbe ya kidogo yenye inaweza kutufundisha mambo ya maana. (Soma Mezali 30:26.) Wibari inafanana na sungura ya munene, lakini iko na masikio ya mufupi na ya kiviringo, na pia migulu ya mufupi. Inakuwaka naishi fasi kwenye kuko miamba. Macho yake inaonaka mbali, na ile inaisaidiaka kufichama wakati inaona banyama benye banawindaka bengine. Wibari iliumbwa juu ya kuishi mu kundi, hapana yopeke. Ile kundi inakuwaka nailinda, na inaisaidiaka kwa kuipatia kifukutu wakati ya baridi.
Tunaweza kujifunza nini wakati tunachunguza Wibari? Kwanza, wibari ni nyama mwenye hakuwake naishi yepeke juu ya kuepuka banyama bengine benye banawindaka basimukule. Tena, inatumiaka macho yake juu ya kuona mbali sana banyama benye banawindaka, na inabakiaka karibu na mashimu na matundu kwenye inaweza kujificha. Sawa wibari, tuko na lazima ya macho ya kiroho juu ya kuona kwa mbali mitego yenye iko mu hii ulimwengu ya Shetani. Mutume Petro alionya Bakristo kwa kusema hivi: “Mulinde akili zenu, mukuwe macho! Adui yenu, Ibilisi, anatembea huku na huku kama simba mwenye kunguruma, akitafuta kumumeza mutu.” (1Pe 5:8) Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alikuwa macho na aliepuka mitego yote ya Shetani yenye ingeweza kuvunja uaminifu-mushikamanifu wake kwa Yehova. (Mt. 4:1-11) Yesu aliachia banafunzi yake mufano muzuri sana!
Njia moya ya kuonyesha kama tuko macho ni kufaidika na ulinzi wa kiroho wenye Yehova iko natupatia. Kusoma Biblia na kukusanyika ni mambo yenye tunapaswa kuona kuwa ya maana kabisa. (Lu 4:4; Ebr 10:24, 25) Tunajifunza pia kama, sawa tu vile wibari inabakiaka mu kikundi, tuko na lazima ya kubakia karibu na Bakristo benzetu juu ya kufurahia “ubadilishanaji wa kitia-moyo.” (Ro 1:12) Kama tunafaidika na ulinzi wenye Yehova iko natupatia, tutakubaliana na Daudi mwenye aliandika hivi: “Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu na ule mwenye ananiokoa. Mungu wangu ni mwamba wangu, mwenye ninakimbilia.”—Zb 18:2.
Hotuba: Kucheza Michezo ya Makuta ni Zambi?
ijwbq-SW habari ya 102
Je, Kucheza Kamari Ni Dhambi?
Ingawa Biblia haizungumzi kwa undani kuhusu kucheza kamari, tunapochunguza kanuni za Biblia tunaweza kuelewa kwamba Mungu huona kucheza kamari kuwa ni dhambi.—Waefeso 5:17.
Kucheza kamari kunaongozwa na pupa, na Mungu anachukia pupa. (1 Wakorintho 6:9, 10; Waefeso 5:3, 5) Watu wanaocheza kamari wanatazamia kupata pesa wengine wanapopoteza, lakini Biblia inashutumu kutamani mali za wengine.—Kutoka 20:17; Waroma 7:7; 13:9, 10.
Kucheza kamari, hata kwa ajili ya pesa kidogo, kunaweza kuchochea tamaa mbaya ya pesa.—1 Timotheo 6:9, 10.
Mara nyingi wacheza kamari hutegemea ushirikina au bahati. Hata hivyo, Mungu huona imani kama hizo kuwa aina ya ibada ya sanamu, ambayo haipatani na ibada yake.—Isaya 65:11.
Badala ya kuchochea tamaa ya kupata kitu bila kutia jitihada, Biblia inatutia moyo tufanye kazi kwa bidii. (Mhubiri 2:24; Waefeso 4:28) Wale wanaofuata ushauri wa Biblia wanaweza ‘kula chakula ambacho wao wenyewe wamefanyia kazi.’—2 Wathesalonike 3:10, 12.
Kucheza kamari kunaweza kuchochea roho isiyofaa ya mashindano, jambo ambalo Biblia inashutumu.—Wagalatia 5:26.
TAREHE 15-21/9
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 31
Mafundisho Yenye Tunapata mu Mashauri ya Upendo Yenye Mama Iko Napatia Mutoto Yake
Wafundishe Watoto Wako Maadili Mema
Wafundishe ukweli wote kuhusu ngono. Maonyo ni muhimu. (1 Wakorintho 6:18; Yakobo 1:14, 15) Hata hivyo, Biblia inaitaja ngono kuwa zawadi kutoka kwa Mungu, bali si mtego wa Shetani. (Methali 5:18, 19; Wimbo wa Sulemani 1:2) Kuwaeleza vijana wako kuhusu tu hatari za kufanya ngono, kunaweza kuwaacha na mtazamo uliopotoka na usio wa Kimaandiko kuihusu. Mwanamke mmoja kijana aitwaye Corrina kutoka Ufaransa anasema, “Wazazi wangu walikazia tu mwenendo mpotovu kingono na hilo lilinifanya niwe na mtazamo mbaya kuhusu ngono.”
Hakikisha kwamba unawaeleza watoto wako ukweli wote kuhusu ngono. Mama mmoja nchini Mexico aitwaye Nadia, anasema, “Kile ambacho wakati wote nimejaribu kuwaeleza vijana wangu ni kwamba ngono ni nzuri na ni jambo la kawaida, na kwamba Yehova Mungu aliwapa wanadamu ili waifurahie. Lakini inapaswa kufurahiwa tu katika ndoa. Ngono inaweza kutuletea furaha au mateso, ikitegemea jinsi tunavyoitumia.”
ijwhf-SW habari ya 4 fu. 11-13
Kuzungumza na Watoto Kuhusu Kileo
Chukua hatua ya kwanza kuzungumzia jambo hilo. Mark, ambaye ni baba nchini Uingereza anasema: “Watoto wanaweza kuchanganyikiwa wanapofikiria suala la kileo. Nilimuuliza mwana wangu mwenye umri wa miaka minane ikiwa alifikiri ni sawa au si sawa kunywa kileo. Niliandaa mazingira matulivu, na hilo lilimsaidia kueleza maoni yake waziwazi.”
Utamsaidia zaidi ukizungumzia suala hilo mara kadhaa. Ikitegemea umri wa mtoto tia ndani mazungumzo kuhusu kileo pamoja na masuala mengine maishani, kama usalama barabarani na elimu ya ngono.
Weka kielelezo kinachofaa. Watoto ni kama sifongo, wanafyonza kila kitu kwenye mazingira, na utafiti unaonyesha kwamba wazazi ndio walio na uvutano mkubwa zaidi kwa watoto wao. Hiyo inamaanisha kwamba ikiwa kileo ndiyo njia yako ya msingi ya kutulia au kupunguza mkazo, mtoto wako ataelewa kwamba kileo ndiyo njia ya kuondoa mahangaiko maishani. Basi weka mfano mzuri wa kuigwa. Hakikisha kwamba unatumia kileo kwa hekima.
Kufundisha Watoto Unyenyekevu
Umufundishe kuwa mutoaji. Onyesha mutoto wako kwamba “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Matendo 20:35) Namna gani? Wewe pamoja naye, munaweza kutayarisha liste ya watu wenye kuwa na lazima ya musaada ili kuwanunulia vitu mbalimbali, kuwabeba, ao kuwatengenezea vitu vyao. Kisha, uende pamoja na mutoto wako wakati unasaidia wamoja kati yao. Uache mutoto wako aone furaha yako wakati unatimizia wengine mambo yenye wako nayo lazima. Kufanya hivyo kutafundisha mutoto wako unyenyekevu katika njia kubwa zaidi, ni kusema, kupitia mufano wako.—Kanuni ya Biblia: Luka 6:38.
Mali ya Kiroho
w92 1/11 uku. 11-12 fu. 7-8
Namna Balikuwaka Nafundisha Zamani mu Israeli
Mu Israeli, baba na mama balikuwaka bote bawili nafundisha batoto yabo wakati balikuwa batoto sana. (Kumbukumbu la Torati 11:18, 19; Mezali 1:8; 31:26) Mu kitabu ya Kifaransa Dictionnaire de la Bible, E. Mangenot mwenye anajifunzaka mambo ya Biblia aliandika hivi: “Wakati tu mutoto alianza kusema, balikuwa namufundisha maandiko fulani ya Sheria. Mama yake alikuwa nasema na kurudilia andiko moya; kama mutoto anaijua, mama yake alikuwa namupatia ingine. Kisha, balikuwa natia mu mikono ya batoto maandiko yenye balikuwa balishaweka mu akili. Kwa kufanya vile, balikuwa nabafundisha kusoma. Sasa wakati bale batoto banakomala, balikuwa naendelea kujifunza mambo ya kiroho kwa kusoma na kutafakari juu ya sheria ya Bwana.”
Ile inafanya tuseme kama njia moya ya kujifunza yenye balikuwa natumia ilikuwa kutia mu akili (mémoriser). Balipaswa kuweka kabisa ku moyo mambo yenye balikuwa najifunza kuhusu sheria za Yehova na kuhusu namna alikuwa natendea batu yake. (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7) Balipaswa kutafakari juu ya ile mambo. (Zaburi 77:11, 12) Balikuwa natumia njia mbalimbali juu ya kusaidia bijana na bale benye balishakomala kukumbuka mambo yenye balishajifunza. Njia moya ilikuwa kutumia herufi za kialfabeti, kwa mufano maandiko fulani ya kufuatana ya zaburi ilikuwa naanza na herufi mbalimbali, za kufuatana kialfabeti (ordre alphabétique) (Ona pia Mezali 31:10-31); njia ingine ilikuwa allitération (Maneno yenye inaanza na herufi ileile ao sauti ileile); balikuwa natumia pia namba, sawa vile ile yenye kuwa mu Mezali 30:16-33.
TAREHE 22-28/9
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MUHUBIRI 1-2
Endelea Kuzoeza Kizazi ya Kufuata
Mambo Hayo Uwapatie Wanaume Waaminifu
Tunapenda kumutumikia Yehova na tunaona migawo yetu kuwa ya maana sana. Wengi kati yetu tunafurahia sana kazi yetu; ndiyo sababu tunapenda kuendelea kufanya kazi hiyo kadiri inawezekana. Lakini, jambo la kuhuzunisha ni kwamba, wakati watu wanazeeka, hawawezi tena kufanya mambo yote yenye walizoea kufanya wakati walikuwa vijana. (Mhubiri 1:4) Hilo linaleta magumu ya pekee kwa watu wa Yehova. Leo, kazi ya kuhubiri inaendelea kuongezeka, na tengenezo la Yehova linaendelea kutumikisha teknolojia ya sasa ili habari njema ifikie watu wengi zaidi. Lakini wakati fulani inaweza kuwa vigumu kwa wale wenye kuzeeka kujifunza namna ya kutumikisha njia za mupya. (Luka 5:39) Pia, ni jambo la kawaida watu wapungukiwe na nguvu na uwezo wao wakati wanaendelea kuzeeka. (Methali 20:29) Kwa hiyo, ni jambo lenye kuonyesha upendo na lenye kufaa wakati wale wenye kuzeeka wanazoeza vijana ili wapate madaraka zaidi katika tengenezo la Yehova.—Soma Zaburi 71:18.
Haiko vyepesi sikuzote kwa wale wenye kuwa na madaraka kuachia vijana wanaume madaraka yenye walikuwa nayo. Inaweza kufanya ndugu wahuzunike wakati wanafikiri kuwa watapoteza mugawo wenye wanapenda sana. Inaweza kuwaumiza wakati wanafikiria kuacha kazi fulani ya pekee yenye walikuwa wanafurahia kufanya. Ao wanaweza kuogopa kwamba ikiwa hawaongoze tena kazi hiyo, haitafanywa muzuri. Pengine wanafikiri kuwa hawana wakati wa kuzoeza wengine. Wakati huohuo, ni lazima vijana wanaume wakuwe na uvumilivu wakati hawapewe madaraka zaidi.
Mali ya Kiroho
it-F “Ecclesiastes” fu. 1
Muhubiri
Jina ya Kiebrania Qoheleth (yenye inamaanisha “Mukutanishaji, Mukusanyishaji”) inaonyesha daraka yenye mufalme alikuwa nayo mu kazi ya kiteokrasi ya ufalme wake yenye Baisraeli balikuwa nafaidika nayo. (Muh 1:1, 12) Mufalme alikuwa na daraka ya kuchochea batu benye balikuwa balishajitoa kwa Mungu baendelee kuwa na umoja, na babakie bashikamanifu kwa Mufalme wabo wa kweli, Mungu. (1Fa 8:1-5, 41-43, 66) Njo maana, mufalme alikuwa najulikana kuwa mufalme muzuri kama anachochea batu bamuabudu Mungu; na alikuwa najulikana kuwa mufalme mubaya kama hachochee batu bamuabudu Mungu. (2Fa 16:1-4; 18:1-6) Kwa mara mingi, Sulemani mwenye alikuwa mukutanishaji, alikuwa tayari alishakutanisha Baisraeli na benye habakuwa Baisraeli ku hekalu. Mu hii kitabu, alikuwa naambia batumishi ya Mungu baachane kabisa na mambo ya mubaya ya hii ulimwengu, na bashikamane na mambo ya muzuri ya Mungu, mwenye balikuwa balishajitoa kwake bakiwa taifa.
TAREHE 29/9–5/10
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MUHUBIRI 3-4
Mufanye Kamba Yenu ya Nyuzi Tatu Ikuwe Nguvu
ijwhf habari ya 10 fu. 2-8
Namna ya Kuacha Mambo ya Teknolojia pa Nafasi Yake
● Kutumia muzuri mambo ya teknolojia, sawa vile telefone, kunaweza kuwa na matokeo ya muzuri mu ndoa. Kwa mufano, bwana na bibi fulani wanaitumia juu ya kupashana habari muchana wakati hawako fasi moja.
“Kutumiana tu sms yenye kusema ‘Nakupenda’ ao ‘Niko nakuwaza’ kunaweza kufanya weye na bibi yako mujisikie kuwa karibu sana.”—Jonathan.
● Kutumia mubaya mambo ya teknolojia kunaweza kuharibisha ndoa. Kwa mufano, watu fulani wanatumiaka telefone ao tablete zao kila wakati, ile inafanya wasikuwe na wakati wa kuhangaikia bibi ao bwana yao.
“Niko hakika kama kulikuwa wakati bwana yangu angependa kuzungumuza na miye kama singekuwa natumikisha telefone yangu.”—Julissa.
● Watu fulani wanasema kama wanaweza kuzungumuza muzuri na bibi ao bwana yao hata kama wako wanatumikisha telefone ao tablete yao. Sherry Turkle, mwanamuke fulani mwenye elimu ya sociolojia alionyesha kama ile haiwezekane. Ni wazi kama, hata ikiwa watu wanawaza kama wako na uwezo wa kufanya mambo ya mingi kwa wakati moja, ile haiko jambo ya muzuri. Sherry anasema kama, kwa kweli, ‘kadiri tunajikaza kufanya mambo ya mingi wakati ileile, ni vile tunashindwa kuifanya muzuri.”
“Napendaka sana kuzungumuza na bwana yangu, lakini hapana wakati iko anazungumuza na miye na wakati ileile iko anafanya mambo ingine, sawa vile kutumikisha telefone. Akifanya vile naonaka kama hanihangaikie.”—Sarah.
Wazo kubwa: Namna unatumia mambo ya teknolojia, sawa vile telefone ao tablete, inaweza kusaidia ao kuharibu ndoa yako.
Usiache “Mwali wa Moto wa Yah” Uzimike
Bibi na bwana wanaweza kufanya nini ili kuiga Akila na Prisila? Mufikirie mambo mingi yenye munapaswa kufanya. Kuliko kila mutu kufanya ile mambo yeye peke, munawaza nini kama munaifanya pamoya? Kwa mufano, Akila na Prisila walihubiri pamoya. Nyiye pia munapangaka kufanya vile kila mara? Akila na Prisila walitumika pia pamoya. Pengine weye na bibi ao bwana yako hamutumikake kazi fulani ya kimwili pamoya, lakini, munawaza nini kama munatumika pamoya kazi ya mu nyumba? (Muh. 4:9) Wakati muko nafanya kazi fulani pamoya, mutakuwa sawa vile watu wenye kutumika mu ekipe na mutakuwa na nafasi ya kuongea. Robert na Linda walishafanya zaidi ya miaka 50 mu ndoa. Robert anasema hivi: “Kusema kweli, hatukuwake na wakati mingi ya kupitisha pamoya ili kujifurahisha. Lakini, nafurahiaka sana wakati niko nasafisha masahani na bibi yangu iko naipanguza ao wakati niko inje niko natengeneza bustani naye anakuya kunisaidia. Kufanya mambo pamoya kunatuunganishaka na kunafanyaka tupendane sana.”
Lakini, mukumbuke kama haiko tu kupitisha wakati pamoya njo itafanya mukaribiane. Bibi moya wa mu Brazili anasema hivi: “Leo kuko mambo mingi ya kukengeusha. Kwa hiyo, nilifikia kuona kama inaweza kuwa mwepesi kuwaza kama tuko napitisha wakati pamoya juu tu tuko naishi mu nyumba moya. Niliona kama kuko mambo ingine ya kufanya zaidi tu ya kupitisha wakati pamoya. Napaswa pia kumuhangaikia bwana yangu.” Ona namna Bruno na bibi yake, Tays, wanatendeanaka. Bruno anasema hivi: “Wakati wenye tunapitishaka pamoya, tunatiaka telefone zetu pembeni na tunafurahiaka ile wakati.”
Sasa, munaweza kufanya nini kama hamupendake kupitisha wakati pamoya? Pengine kila mutu iko na mambo yenye anapendaka ao pengine munakasirishanaka. Munaweza kufanya nini? Fikiria moto wenye tulishazungumuzia. Moto hauwakake sana ku mwanzo. Inaomba kuongeza kuni ya munene pole kwa pole. Vilevile, munawaza namna gani kama munaanza kwanza kupitisha wakati kidogo pamoya? Mujikaze kufanya jambo yenye nyiye wote munapendaka, hapana jambo yenye itafanya muanze kukasirishana. (Yak. 3:18) Wakati munaanza na mambo ya kidogo, mutapendana tena zaidi.
Usiache “Mwali wa Moto wa Yah” Uzimike
Juu “mwali wa moto wa Yah” usizimike, bibi na bwana wanapaswa kuwa na uhusiano wa nguvu pamoya na Yehova. Ile itasaidia namna gani ndoa yao? Wakati bibi na bwana wanaona uhusiano wao pamoya na Baba yao wa mbinguni kuwa wa maana, watakuwa tayari kutii mashauri yake, na ile itawasaidia kuepuka na kupambana na magumu yenye inaweza kufanya upendo wao upunguke. (Soma Muhubiri 4:12.) Watu wa kiroho wanajikazaka pia kumuiga Yehova na kuwa na sifa zenye anaonyeshaka, sawa vile fazili, uvumilivu, na musamaha. (Efe. 4:32–5:1) Ni mwepesi zaidi kwa bibi na bwana wenye kuwa na zile sifa kupendana sana. Dada Lena, mwenye alishafanya zaidi ya miaka 25 mu ndoa, anasema hivi: “Inakuwaka mwepesi kupenda na kuheshimia mutu wa kiroho.”
Mali ya Kiroho
it-F “Amour” fu. 39
Upendo
“Wakati wa Kupenda.” Yehova haonyeshake upendo tu kwa bale benye anaona kuwa habastahili kupata ile upendo ao benye banafanyaka mambo ya mubaya. Mungu anapendaka batu bote. Lakini kama mutu anaonyesha kama anamuchukia Mungu, upendo wa Mungu kwa ule mutu utaishia pale. Yehova na Yesu Kristo banapendaka batu benye haki, lakini banachukiaka benye banavunjaka sheria. (Zb 45:7; Ebr 1:9) Bale benye banamuchukiaka kabisa Mungu wa kweli habastahili hata kidogo upendo wetu. Ni bure kuendelea kubaonyesha upendo, juu bale benye banamuchukiaka Mungu habawezi kuonyesha hata siku moya kama banamupenda. (Zb 139:21, 22; Isa 26:10) Njo maana, Mungu anabachukia na alishapanga wakati wa kubaharibu.—Zb 21:8, 9; Muh 3:1, 8.
TAREHE 6-12/10
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MUHUBIRI 5-6
Namna Tunaonyesha Kama Tunamuheshimia Sana Mungu Wetu Mukubwa
w08-SW 15/8 uku. 15-16 fu. 17-18
Mheshimu Yehova kwa Kuonyesha Heshima
Tunapaswa kujiendesha kwa heshima hasa tunapomwabudu Yehova. Andiko la Mhubiri 5:1 linasema hivi: “Linda miguu yako wakati wowote unapoenda kwenye nyumba ya Mungu wa kweli.” Musa na Yoshua waliamuriwa wavue viatu vyao waliposimama mahali patakatifu. (Kut. 3:5; Yos. 5:15) Walipaswa kufanya hivyo ili kuonyesha heshima au staha. Makuhani Waisraeli waliamuriwa wavae suruali za kitani “ili kuufunika mwili ulio uchi.” (Kut. 28:42, 43) Hilo liliwazuia wasionyeshe uchi wao walipotumikia kwenye madhabahu. Kila mshiriki wa familia ya kuhani alipaswa kufuata viwango vya Mungu vya heshima.
Kwa hivyo, tunapaswa kuonyesha heshima na staha katika ibada. Ili tustahili kuonyeshwa heshima na staha, ni lazima tutende kwa heshima. Hatupaswi kujifanya tu kuwa wenye heshima au kuwa na heshima kijuujuu tu. Haipaswi tu kuwa heshima inayoonwa na wanadamu, inapaswa kutoka moyoni ambamo Mungu anaweza kuona. (1 Sam. 16:7; Met. 21:2) Heshima inapaswa kuwa sehemu ya maisha yetu nayo inapaswa kuongoza tabia yetu, mtazamo wetu, uhusiano wetu na wengine, na hata jinsi tunavyohisi na kujiona. Kwa kweli, heshima inapaswa kuonekana nyakati zote na katika kila jambo tunalosema na kufanya. Tunaonyesha kwamba tunatii maneno haya ya mtume Paulo kupitia mwenendo wetu, mavazi na mapambo yetu, na jinsi tunavyowatendea wengine: “Sisi hatutoi sababu yoyote ya kukwaza kwa njia yoyote, ili huduma yetu isilaumiwe; bali katika kila njia tunajipendekeza kuwa wahudumu wa Mungu.” (2 Kor. 6:3, 4) ‘Tunalipamba fundisho la Mwokozi wetu, Mungu, katika mambo yote.’—Tito 2:10.
w09-SW 15/11 uku. 11 fu. 21
Boresha Sala Zako Kupitia Funzo la Biblia
Yesu alisali kwa heshima akiwa na imani kabisa. Kwa mfano, kabla ya kumfufua Lazaro, ‘Yesu aliinua macho yake kuelekea mbinguni na kusema: “Baba, ninakushukuru kwamba umenisikia. Kweli, nilijua kwamba sikuzote wewe hunisikia.”’ (Yoh. 11:41, 42) Je, sala zako zinaonyesha imani na heshima kama hiyo? Ukichunguza sala ya Yesu ya kielelezo yenye heshima, utaona kwamba mambo makuu katika sala hiyo hasa ni kutakaswa kwa jina la Yehova, kuja kwa Ufalme wake, na kutimizwa kwa mapenzi yake. (Mt. 6:9, 10) Fikiria kuhusu sala zako mwenyewe. Je, zinaonyesha kwamba unapendezwa sana na Ufalme wa Mungu, kufanya mapenzi yake, na kutakaswa kwa jina lake takatifu? Sala zako zinapaswa kuonyesha hivyo.
‘Kile Unachoweka Naziri, Timiza’
Wakati ulibatizwa, ulimuahidi Yehova kama utatumia maisha yako ili kumutumikia na kufanya yako yote ili kufuata kanuni zake. Lakini ubatizo ni mwanzo tu. Kadiri wakati unapita, sisi wote tunapaswa kuendelea kujichunguza. Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Urafiki wangu pamoja na Yehova umekomaa kwa kiasi gani tangu nibatizwe? Ninaendelea kumutumikia kwa moyo wangu wote? (Wakolosai 3:23) Ninasali kwa ukawaida? Ninasoma Biblia kila siku? Ninakusanyika kwa ukawaida? Ninafanya yangu yote ili kufanya kazi ya kuhubiri kwa ukawaida? Ao nimepunguza bidii yangu kwa ajili ya mambo hayo?’ Mutume Petro alituonya kama kuko hatari ya kufikia kuwa watu wasiotenda katika utumishi wetu kwa Yehova. Tunaweza kuepuka jambo hilo ikiwa tunajikaza sana kukomalisha imani, ujuzi, uvumilivu, na ushikamanifu wetu kwa Mungu.—Soma 2 Petro 1:5-8.
Mali ya Kiroho
Maulizo ya Wasomaji Wetu
Muhubiri 5:8 inazungumuzia mutawala mwenye iko anatesa maskini na kuwatendea bila haki. Anapaswa kukumbuka kama kuko mutawala mwingine mwenye iko na mamlaka zaidi kuliko yeye, mwenye iko anaona mambo yote yenye iko anafanya. Na kunaweza kuwa watawala wengine wenye wako na mamlaka zaidi kuliko wale watawala wawili. Inahuzunisha kuona kama mu serikali za wanadamu, wale watawala wote, wanaweza kutendea wengine bila haki. Na ile inaweza kufanya wale wenye wako chini ya mamlaka yao wateseke.
Lakini tunajua kama Yehova iko anaona mambo yenye ‘maofisa wakubwa’ wa serikali za wanadamu wako wanafanya. Kwa hiyo, hata wakati wanatutendea bila haki na tunawaza kama hakuna tena tumaini, hatuache ile ituvunje moyo. Kuliko kufanya vile, tunasali kwa Yehova na kumuomba atusaidie. (Zb. 55:22; Flp. 4:6, 7) Tunajua kama “macho ya Yehova yanaenda huku na huku katika dunia yote ili kuonyesha nguvu zake kwa ajili ya wale wenye moyo wao ni kamili kumuelekea yeye.”—2 Ny. 16:9.
Kwa kifupi, Muhubiri 5:8 inatukumbusha kama mu serikali za wanadamu, kunakuwaka mutu mwenye iko na mamlaka zaidi ya wengine. Na jambo la maana zaidi, ile andiko inatukumbusha kama Yehova njo iko na mamlaka ya juu zaidi. Na sasa iko anatawala mbinguni kupitia Mwana wake Yesu Kristo, Mufalme wa Ufalme wake. Yehova, Mungu Mweza-Yote, iko anaona mambo yote yenye iko inafanyika, na haiko sawa vile watawala wanadamu, yeye ni mwenye haki kabisa na Yesu Kristo Mwana wake ni mwenye haki pia.
TAREHE 13-19/10
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MUHUBIRI 7-8
‘Uende Katika Nyumba ya Maombolezo’
it-F “Deuil” fu. 9
Kilio
Wakati wa Kulia. Muhubiri 3:1, 4 inasema kama kunakuwaka “wakati wa kulia na wakati wa kucheka; wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza.” Juu kifo inaweza kutufikia siye bote, mutu ataonyesha kama iko na hekima wakati anaenda “katika nyumba ya maombolezo” kuliko kuenda ku fete. (Muh 7:2, 4; linganisha na Mez 14:13.) Mutu mwenye hekima atatumia ile nafasi juu ya kufariji na kutia moyo benye balifisha, kuliko kufanya tu sawa vile hakuna kitu na kutoka kuenda kujifurahisha. Kufanya vile kutamusaidia hasisahau kama kifo kinafikiaka batu bote, na kutamusaidia pia aendelee kuwa na mawazo ya muzuri juu ya Muumbaji wake.
Saidia Wengine Wapiganishe Mahangaiko
William, mwenye bibi yake alikufa miaka fulani yenye imepita, anasema hivi: “Ninafurahi wakati wengine wananielezea mambo ya muzuri yenye wanakumbuka juu ya bibi yangu; hilo linanihakikishia kama walikuwa wanamupenda na kumuheshimia. Kunitegemeza katika njia hiyo kunanisaidia sana. Maneno yao inanifariji sana, kwa sababu bibi yangu alikuwa wa samani sana kwangu na alikuwa mutu wa maana katika maisha yangu.” Mujane mumoja mwenye kuitwa Bianca anasema hivi: “Ninafarijiwa wakati wengine wanasali pamoja na mimi na kunisomea andiko moja ao maandiko mbili. Ninajisikia muzuri wakati wanazungumuza juu ya bwana yangu na wakati wananisikiliza nikizungumuza juu yake.”
‘Mulie Pamoja na Watu Wanaolia’
Usizarau nguvu ya sala zenye unaweza kutoa pamoja na Mukristo mwenye amefiwa ao sala zenye unaweza kutoa wakati mwingine kwa ajili yake. Hata kama inaweza kuwa vigumu kusema muzuri mawazo yako katika hali kama hiyo, kusali kwa moyo wote kwa ajili yake, hata kwa kutoa machozi na kwa sauti yenye kutetemeka, kunaweza kumufariji sana mutu mwenye amefiwa. Dalene anakumbuka hivi: “Wakati fulani, wakati dada wamekuja kunifariji, nimewauliza ikiwa watapenda kusali. Wakati wanaanza kusali, mara nyingi wanashindwa kusema, lakini kila wakati, kisha kusema maneno fulani, sauti zao zinaanza kupata nguvu na wanasali kwa moyo wao wote. Imani yao yenye nguvu, upendo wao, na namna wananihangaikia, vimetia nguvu sana imani yangu.”
‘Mulie Pamoja na Watu Wanaolia
Muda wenye mutu anaweza kufanya ili huzuni yake ifikie kuisha unatofautiana sana kati ya watu mbalimbali. Kwa hiyo, ukuwe tayari kusaidia wakati wowote, haiko tu katika siku za kwanza-kwanza wakati marafiki wengi na watu wa jamaa wako pale, lakini pia katika miezi yenye kufuata wakati wengine wamerudilia mambo yao ya kawaida. “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote, naye ni ndugu aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.” (Met. 17:17) Wakristo wanaweza kufariji sana mutu fulani mwenye amefiwa kwa muda wote wenye anaendelea kupambana na huzuni yake.—Soma 1 Wathesalonike 3:7.
Kumbuka kuwa mambo kama vile siku fulani za kukumbuka, muziki fulani, picha, kazi mbalimbali, ao hata harufu fulani, sauti ao majira fulani ya mwaka, yanaweza kuletea huzuni watu wenye wamefiwa. Mambo mengi yenye bibi ao bwana mwenye amefiwa anafanya kwa mara ya kwanza yeye peke yake, kama vile kuenda kwenye mukusanyiko ao Ukumbusho, yanaweza kumuletea huzuni nyingi. Ndugu mumoja alisema hivi: “Nilitazamia kuwa kisha kifo cha bibi yangu, tarehe ya kukumbuka siku yenye tulifunga ndoa ingeniletea huzuni nyingi, na haikukuwa mwepesi. Lakini ndugu na dada fulani walifanya mipango ili tukutane pamoja na marafiki wangu wa sana ili nisibakie mimi mwenyewe.”
Hata hivyo, kumbuka kuwa watu wenye wamefiwa wako na lazima ya kufarijiwa haiko tu wakati wa matukio fulani ya pekee. Junia anasema hivi: “Mara nyingi musaada na urafiki wenye kutolewa wakati mwingine wowote hata kama haiko siku fulani ya pekee ya kukumbuka unaweza kuwa wa maana sana. Wakati kama huo ni wa maana sana na unaleta faraja kubwa.” Ni kweli kwamba hatuwezi kumaliza huzuni yote ya mutu fulani mwenye amefiwa ao kumaliza kabisa hali ya kujisikia kuwa peke yake, lakini tunaweza kutuliza na kufariji kwa kadiri fulani mutu mwenye amefiwa kwa kumutolea musaada wenye kufaa. (1 Yoh. 3:18) Gaby anakumbuka hivi: “Niko mwenye shukrani sana kwa Yehova kwa sababu ametutolea wazee wenye upendo wenye walinisaidia katika magumu yote yenye nilipata. Wamenifanya kabisa nijisikie kuwa mikono ya Yehova yenye upendo imenikumbatia.”
Mali ya Kiroho
“Kwa Jambo Hili Wote Watajua Kama Ninyi Ni Wanafunzi Wangu”
Wakati fulani, inaweza kuwa muzuri kuongea na muamini mwenzetu mwenye alitukosea. Kwanza, ni muzuri tujiulize hii maulizo: ‘Niko na habari zote?’ (Mez. 18:13) ‘Inawezekana hakunikosea kimakusudi?’ (Muh. 7:20) ‘Na miye siyakoseaka mutu fulani vile?’ (Muh. 7:21, 22) ‘Kama nazungumuza na ule mutu mwenye alinikosea, ile itafanya mambo iharibike tena zaidi?’ (Soma Mezali 26:20.) Kama tunakamata wakati ya kujiuliza ile maulizo, upendo unaweza kutuchochea kusamehe wengine wakati wanatukosea.
Onyesho: Mazishi ya Mashahidi wa Yehova Inakuwaka Namna Gani?
ijwfq-SW habari ya 50
Mashahidi wa Yehova Wana Maoni Gani Kuhusu Mazishi?
Maoni yetu kuhusiana na mazishi yanategemea mafundisho ya Biblia. Yafuatayo ni baadhi ya mafundisho hayo:
Ni jambo la kawaida kuhuzunika mpendwa wetu anapokufa. Wanafunzi wa Yesu waliomboleza walipofiwa na wapendwa wao. (Yohana 11:33-35, 38; Matendo 8:2; 9:39) Hivyo, hatuoni mazishi kuwa pindi ya sherehe. (Mhubiri 3:1, 4; 7:1-4) Badala yake, tunaiona kuwa pindi ya kuwafariji waliofiwa.—Waroma 12:15.
Wafu hawajui lolote. Hata iwe tumetoka kabila gani au tuna malezi gani, tunaepuka mila au desturi zinazotegemea imani zisizo za kimaandiko kwamba wafu wanaendelea kuishi na wanaweza kuwaathiri walio hai. (Mhubiri 9:5, 6, 10) Desturi hizo zinatia ndani kukesha, sherehe za mazishi zenye gharama kubwa, sherehe za kila mwaka za kukumbuka siku ya mazishi, kutoa dhabihu kwa ajili ya wafu, kuzungumza na kuomba wafu watusaidie, na desturi za kuwatakasa wajane. Tunaepuka mila na desturi hizo kwa kuwa tunatii amri hii ya Biblia: ‘Jitengeni, na mwache kugusa kitu kilicho najisi.’—2 Wakorintho 6:17.
Kuna tumaini kwa wafu. Biblia inafundisha kwamba kutakuwa na ufufuo na kutakuwa na wakati ambapo kifo hakitakuwapo tena. (Matendo 24:15; Ufunuo 21:4) Tumaini hilo linatusaidia kuepuka desturi za kuomboleza kupita kiasi, kama tu lilivyowasaidia Wakristo wa mapema.—1 Wathesalonike 4:13.
Biblia inatushauri tuwe na kiasi. (Methali 11:2) Hatuamini kwamba mazishi yanapaswa kutumiwa ‘kuonyesha’ hali yetu ya kiuchumi au jinsi tunavyoheshimika katika jamii. (1 Yohana 2:16) Hatupangi mazishi yenye madoido mengi yaliyokusudiwa tu kuwatumbuiza watu au kununua majeneza ya gharama kubwa sana au mavazi maalamu ili tu kujionyesha mbele za watu.
Hatujaribu kuwalazimisha wengine wafuate maoni yetu kuhusu mazishi. Tunafuata kanuni hii: “Kila mmoja wetu atatoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.” (Waroma 14:12) Hata hivyo, tukipewa nafasi, tunawaeleza wengine imani yetu “kwa tabia-pole na heshima kubwa.”—1 Petro 3:15.
Mashahidi hufanyaje mazishi yao?
Mahali: Familia ikipanga kuwe na hotuba ya mazishi, inaweza kutolewa mahali popote ambapo familia hiyo itachagua, kama vile kwenye Jumba la Ufalme, nyumba ya mazishi, nyumbani kwa mtu, nyumba ya kuchomea maiti, au kwenye eneo la kaburi.
Hotuba: Hotuba hutolewa kuwafariji waliofiwa kwa kueleza mambo ambayo Biblia inasema kuhusu kifo na tumaini la ufufuo. (Yohana 11:25; Waroma 5:12; 2 Petro 3:13) Hotuba ya mazishi inaweza kutaja sifa nzuri za mtu aliyekufa, na labda kukazia mambo yenye kutia moyo tunayojifunza kutokana na mfano wa uaminifu wa mtu huyo.—2 Samweli 1:17-27.
Wimbo unaotegemea Maandiko unaweza kuimbwa. (Wakolosai 3:16) Programu yote hufungwa kwa sala yenye kufariji.—Wafilipi 4:6, 7.
Malipo au sadaka: Hatudai malipo yoyote kwa ajili ya huduma za kidini tunazotoa, kutia ndani mazishi, wala hatukusanyi sadaka katika mikutano yetu.—Mathayo 10:8.
Wahudhuriaji: Watu ambao si Mashahidi wanakaribishwa kuhudhuria programu ya mazishi inayofanywa kwenye Jumba la Ufalme. Kama tu mikutano yetu mingine, watu wote wanaweza kuhudhuria programu hiyo.
Je, Mashahidi huhudhuria mazishi yanayoendeshwa na dini nyingine?
Kila Shahidi hujiamulia kwa kutegemea dhamiri yake iliyozoezwa na Biblia. (1 Timotheo 1:19) Hata hivyo, hatushiriki katika desturi za kidini zinazopingana na Biblia.—2 Wakorintho 6:14-17.
TAREHE 20-26/10
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MUHUBIRI 9-10
Ukuwe na Mawazo ya Muzuri Juu ya Magumu Yako
Yehova Iko Anakusaidia
Biblia inasema kama “mambo ya mubaya inafikiaka kila mutu.” (Muh. 9:11, Holy Bible—Easy-to-Read Version) Wakati fulani tunapataka magumu yenye iko “kawaida kwa watu,” ni kusema, magumu yenye watu wote wanapataka. (1 Ko. 10:13) Ao tunaweza kupata magumu juu tu tuko wanafunzi wa Yesu. Kwa mufano, watu wanaweza kutucheka, kutupinga, ao hata kututesa juu ya imani yetu. (2 Ti. 3:12) Hata upate magumu ya namna gani, Yehova anaweza kukusaidia.
Yehova Anaona Watumishi Wake Wanyenyekevu Kuwa wa Maana
Pia, sifa ya unyenyekevu inafanya ikuwe mwepesi kwetu kuvumilia magumu mu maisha. Kwa kweli, wakati fulani tunaweza kuona mambo fulani yenye inaonekana kuwa haiko ya haki. Sulemani, mufalme mwenye hekima, alisema hivi: “Nimeona watumishi wakiwa kwenye migongo ya farasi lakini wakubwa wakitembea kwa miguu kama vile watumishi.” (Muh. 10:7) Wakati fulani, watu wenye kuwa na uwezo mukubwa hawapate sifa. Na wakati fulani, watu wenye hawana uwezo mingi wanapata sifa. Hata hivyo, Sulemani alitambua kama ni jambo la hekima tukubali maisha namna iko kuliko kukasirika wakati mambo haiendeke muzuri mu maisha. (Muh. 6:9) Kama tuko wanyenyekevu, itakuwa mwepesi zaidi kukubali mambo yenye hatupendi mu maisha yetu.
Je, Tafrija Unayochagua Inakujenga?
KATIKA Biblia nzima, tunapata maneno yanayoonyesha kwamba Yehova hataki tuishi tu bali pia anataka tufurahie maisha. Kwa mfano, andiko la Zaburi 104:14, 15 linasema kwamba Yehova anafanya ‘chakula kitokezwe duniani, na divai ambayo hufanya moyo wa mwanadamu anayeweza kufa ushangilie, na kuufanya uso ung’ae kwa mafuta, na mkate unaotegemeza moyo wa mwanadamu anayeweza kufa.’ Kwa kweli, Yehova anafanya mimea ikue na kutokeza nafaka, mafuta, na divai ili kutegemeza uhai wetu. Lakini pia divai inafanya ‘moyo ushangilie.’ Hata ingawa divai si ya lazima ili kuendeleza uhai, inaweza kutuletea shangwe zaidi. (Mhu. 9:7; 10:19) Ndiyo, Yehova anataka tushangilie, anataka mioyo yetu ijae “uchangamfu.”—Mdo. 14:16, 17.
Kwa hiyo, hakuna sababu ya kujihisi kuwa na hatia tunapopanga mara kwa mara kuwa na wakati wa ‘kuwaangalia kwa makini ndege wa mbinguni,’ na “mayungiyungi ya shamba” au kufurahia utendaji mbalimbali ambao unatuburudisha na kufanya maisha yetu yawe yenye kufurahisha. (Mt. 6:26, 28; Zab. 8:3, 4) Kuwa na afya nzuri na furaha maishani ni “zawadi ya Mungu.” (Mhu. 3:12, 13) Kuona kwamba wakati wa kujifurahisha ni sehemu ya zawadi hiyo kutatuchochea kutumia wakati huo kwa njia ambayo inampendeza Mpaji wa zawadi hiyo.
Mali ya Kiroho
it-F “Bavardage, Calomnie” fu. 4, 8
Kusema mingi, Buchongezi
Kusema mingi kunaweza kufanya mutu afikie kuwa muchongezi, na ile inaweza kuwa hatari sana kwake. Hekima yenye kuwa mu hii andiko ya Muhubiri 10:12-14 inaonekana kuwa ya kweli: “Midomo ya mujinga ndiyo inamuharibu. Maneno ya kwanza yenye kutoka katika kinywa chake ni upumbavu, na maneno yake ya mwisho ni wazimu wenye kuleta musiba. Lakini mupumbavu anaendelea kusema.”
Wakati fulani, kusema mingi kunaweza kuwa mubaya sana, na mara ingine hakuweze tu kuwa mubaya sana (hata kama kusema mingi kunaweza kufanya mutu akuwe muchongezi), lakini buchongezi inakuwaka tu ya mubaya na inaumizaka. Hata kama mwenye anachongea iko nafanya vile na nia ya muzuri ao ya mubaya, atajiweka tu yepeke mu hali ya mubaya, juu kati ya mambo yenye Mungu anachukiaka, muko “mutu yeyote mwenye kupanda ugomvi kati ya ndugu.” (Mez 6:16-19) Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “muchongezi” ao “mushitaki” ni diabolos. Biblia inatumikisha pia ile neno juu ya kuzungumuzia cheo ya Shetani “Ibilisi,” muchongezi mukubwa wa Mungu. (Yoh 8:44; Ufu 12:9, 10; Mwa 3:2-5) Ile inaonyesha kwenye buchongezi yote ya mubaya ilianziaka.
TAREHE 27/10–2/11
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MUHUBIRI 11-12
Endelea Kuwa na Afya ya Muzuri na Ufurahie Maisha
Hewa ya Muzuri na Mwangaza wa Jua—Ni “Dawa” za Asili za Kuua Bakteria?
Mwangaza wa jua uko pia na uwezo wa kuua mikrobe. Gazeti moja linasema hivi: “Mikrobe mingi zenye zinaleta magonjwa yenye kuambukizwa 2hewa haziwezi kuvumilia mwangaza wa jua.” (Journal of Hospital Infection)
Namna gani unaweza kutumia habari hii? Unaweza kuenda inje, mahali ambapo utabaki kwa wakati wa kadiri ili kuota jua na kuvuta hewa ya muzuri. Bila shaka itakusaidia.
Usamini Zawadi ya Mungu ya Uzima
Hata kama Biblia haiko kitabu yenye inazungumuzia namna ya kuhangaikia afya yako na nini njo unapaswa kula, lakini inazungumuzia mawazo mingi ya Yehova juu ya ile mambo. Kwa mufano, anatuambia tuepuke “mambo yenye kuleta mahangaiko,” yenye inaweza kuharibisha mwili wetu. (Muh. 11:10) Biblia inasema kama tunapaswa kuepuka ulafi na ulevi juu inaweza kuharibisha afya yetu. (Mez. 23:20) Yehova anapenda tuonyeshe sifa ya kujizuia kuhusu kula na kunywa.—1 Ko. 6:12; 9:25.
Tunaweza kukamata maamuzi yenye kuonyesha kama tunamushukuru sana Yehova juu ya zawadi ya uzima kwa kutumia uwezo wetu wa kufikiri. (Zb. 119:99, 100; soma Mezali 2:11.) Kwa mufano, tutachagua kwa hekima chakula yenye tutakula. Kama tunapendaka chakula fulani lakini tunajua kama inatugonjweshaka, uwezo wetu wa kufikiri utatusaidia tusiikule. Tutaonyesha pia kama tunatumia muzuri uwezo wetu wa kufikiri kwa kulala vya kutosha, kufanya mazoezi kwa ukawaida, na kwa kuendelea kufanya usafi wa mwili na wa nyumba yetu.
“Mukuwe Watendaji wa Neno”
Siye waabudu wa Yehova tuko watu wa furaha. Juu ya nini? Kuko mambo mingi yenye inatuletea furaha, kati ya ile mambo kuko kusoma Neno ya Mungu kwa ukawaida na kujikaza kutumikisha mambo yenye tunajifunza.—Soma Yakobo 1:22-25.
Tunapata faida mingi wakati ‘tunakuwa watendaji wa neno.’ Kwa mufano, tunajua kama wakati tunatumikisha mambo yenye tunasoma, tunamufurahisha Yehova, na kumufurahisha Yehova kunatuletea furaha. (Muh. 12:13) Wakati tunatumikisha mambo yenye tunasoma mu Neno ya Mungu yenye kuongozwa na roho yake, tunakuwa na furaha mu familia na tunakuwa na urafiki muzuri pamoya na waabudu wenzetu. Pengine na weye umejionea ile. Zaidi ya ile, tunaepuka magumu yenye watu wenye hawafuate amri za Yehova wanapata. Kwa kweli, tunakubaliana kabisa na mambo yenye Mufalme Daudi alisema. Kisha kutaya sheria, maagizo, na hukumu za Yehova mu wimbo wake, alimalizia kwa kusema hivi: “Katika kuzishika, kuko zawabu kubwa.”—Zb. 19:7-11.
Mali ya Kiroho
it-F “Inspiration” fu. 10
Kuongozwa na Roho ya Mungu
Inaonekana kama baandikaji ya Biblia habakukuwa natumika sawa vile robo, habakukuwa naandika-andika tu wakati roho ya Mungu ilikuwa nabaongoza. Kwa mufano, tunajua kama Ufunuo “Iliongozwa na Roho ya Mungu.” Biblia inasema kama Yohana aliona ile Ufunuo “kwa njia ya alama” kupitia malaika, na kisha pale, Yohana “alitoa ushahidi juu ya neno lenye Mungu alitoa na juu ya ushahidi wenye Yesu Kristo alitoa, ndiyo, juu ya mambo yote yenye aliona.” (Ufu 1:1, 2) Ilikuwa “kwa muongozo wa roho [inamaanisha moja kwa moja “katika roho”]” njo Yohana “alikuja kuwa katika siku ya Bwana” na ni kupitia ileile roho njo balimuambia: “Mambo yenye unaona, uyaandike katika kitabu cha kukunjwa.” (Ufu 1:10, 11) Inaonekana kama Mungu aliona kama ni muzuri aruhusu baandikaji ya Biblia batumie uwezo wabo na akili yabo juu ya kuchagua maneno na misemwa yenye ingeweza kufasiria muzuri mambo yenye balikuwa naona (Hab 2:2). Lakini, aliendelea kubaongoza na kuchunguza byenye balikuwa naandika, juu ku mwisho byote bifikie kuwa kabisa bile byenye balikuwa naambiwa, bifikie kuwa bya kweli, na zaidi ya yote juu bipatane na mapenzi yake. (Mez 30:5, 6) Maneno yenye kuwa mu Muhubiri 12:9, 10 inaonyesha kama muandikaji alipaswa kujikaza kuchunguza na kupanga mawazo muzuri juu ya kupata “maneno yenye kupendeza na kuandika maneno ya kweli yenye hayana makosa.”—Linganisha na Lu 1:1-4.