Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 3-9/11
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU WIMBO WA SULEMANI 1-2
Habari Juu ya Upendo wa Kweli
Upendo wa Kweli Unawezekana?
Ndoa haiko tu mapatano kati ya mwanaume na mwanamuke ao mapatano yenye kukosa upendo. Upendo ni sifa ya maana sana katika ndoa ya Wakristo. Lakini, upendo huo unapaswa kuwa wa namna gani? Ni upendo wenye kuongozwa na kanuni za Biblia? (1 Yoh. 4:8) Ni ule upendo wenye kuunganisha watu wa familia moja? Ni ule upendo kati ya marafiki wa kweli? (Yoh. 11:3) Ni ule upendo wa kimapenzi kati ya mwanaume na mwanamuke? (Met. 5:15-20) Bila shaka, bibi na bwana wanapaswa kuonyeshana namna hizo zote za upendo ili ndoa yao ikuwe na upendo wa kweli na wenye kudumu. Upendo wa kweli unaonyeshwa kwa maneno na kwa matendo. Ni jambo la lazima sana bibi na bwana wasiache kazi zao mbalimbali ziwazuie kuonyeshana upendo. Bibi na bwana wakionyeshana upendo katika ndoa yao, hilo litafanya kila mutu amutumainie mwenzake na akuwe na furaha. Katika desturi ao maeneo fulani, mara nyingi ni watu wa familia ndio wanachagulia kijana wao mutu wa kuoana naye, na hilo linafanya mwanaume na mwanamuke wasijuane vizuri mbele ya kufunga ndoa. Hata hivyo, wakisha kuoana ni jambo la lazima waonyeshane upendo kwa maneno yao. Hilo litafanya upendo wao uongezeke na ndoa yao ikuwe muzuri.
Maonyesho ya mapenzi kati ya bibi na bwana yanaweza kuleta matokeo mengine mazuri. Mufalme Sulemani alimuahidi kijana mwanamuke Mushulami kwamba atamupatia ‘vitaji vya zahabu, pamoja na vifungo vya feza.’ Alimusifu na kusema kwamba yeye ni ‘murembo kama mwezi mupevu [wenye kuenea], mwenye kutakata kama jua linaloangaza.’ (Wim. 1:9-11; 6:10) Lakini kijana mwanamuke alibaki mwaminifu kwa mupenzi wake, muchungaji. Ni nini ilimusaidia aendelee kuwa mwaminifu hata kama hakuwa pamoja na muchungaji? Yeye mwenyewe anatuambia. (Soma Wimbo wa Sulemani 1:2, 3.) Alikumbuka ‘maonyesho ya mapenzi’ ya ule muchungaji. Anasema kwamba maonyesho hayo ya mapenzi yalikuwa “bora [muzuri zaidi] kuliko divai” yenye kufurahisha moyo, na kwamba jina lake lilimutuliza “kama mafuta” yenye kumwangwa juu ya kichwa. (Zab. 23:5; 104:15) Bibi na bwana wakikumbuka maonyesho yao ya mapenzi, hilo linaweza kufanya waendelee kupendana zaidi. Kwa hiyo, ni jambo la lazima sana kwamba bibi na bwana waonyeshane upendo kila mara.
Mali ya Kiroho
Upendo wa Kweli Unawezekana?
Mukristo mwenye hajaoa ao kuolewa anaweza pia kujifunza mambo mengi katika Wimbo wa Sulemani, zaidi sana Mukristo mwenye kutafuta mutu wa kuoana naye. Ule kijana mwanamuke hakupendezwa hata kidogo na Mufalme Sulemani. Aliwakataza kabisa wanawake wa Yerusalemu kumukaza amupende Sulemani. Aliwaambia hivi: ‘Musijaribu kuamusha ao kuwasha upendo ndani yangu mupaka wenyewe utake.’ (Wim. 2:7; 3:5) Sababu gani? Kwa sababu haifae kuanzisha urafiki wa kimapenzi na kila mutu. Kwa hiyo, Mukristo mwenye kuwa na hekima, anapaswa kungojea mupaka wakati atapata mutu wa kuoana naye, mutu mwenye atapenda kabisa.
TAREHE 10-16/11
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU WIMBO WA SULEMANI 3-5
Buzuri ya Ndani Njo ya Lazima
Upendo wa Kweli Unawezekana?
Maneno ya mapenzi yenye kuwa katika Wimbo wa Sulemani, hayazungumuzie tu uzuri wa mwili. Kwa mufano, fikiria yale muchungaji alisema kuhusu maneno ya kijana huyo mwanamuke. (Soma Wimbo wa Sulemani 4:7, 11.) Anasema kwamba midomo ya mwanamuke huyo “inadondosha asali ya sega.” Sababu gani? Kwa sababu asali ya sega ni yenye sukari sana na tamu sana kuliko asali zingine. Muchungaji alisema pia kwamba “asali na maziwa viko chini ya ulimi” wa kijana mwanamuke; hilo linamaanisha kwamba, maneno yake yalikuwa mazuri na yenye kufurahisha sana kama asali na maziwa. Ni wazi, wakati muchungaji anamuambia kwamba yeye ‘ni murembo [muzuri] kabisa, . . . wala hamuna kasoro [kosa] ndani yake,’ hakuwa tu anazungumuzia uzuri wake wa mwili, lakini pia sifa nzuri za kijana huyo mwanamuke.
Upendo wa Kweli Unawezekana?
Soma Wimbo wa Sulemani 4:12. Sababu gani muchungaji analinganisha mupenzi wake na “bustani” yenye kufungwa? Ni kwa sababu si kila mutu anaweza kuingia katika bustani yenye kufungwa. Ili mutu aingie humo anapaswa kufungua kwanza mulango. Mwanamuke Mushulami analinganishwa na bustani yenye kufungwa kwa sababu upendo wake ulikuwa tu wa ule muchungaji, mwenye atakuwa bwana yake. Alikataa vishawishi vyote vya mufalme; kwa hiyo hakuwa ‘mulango’ wenye kufunguliwa kwa kila mutu, lakini alikuwa “ukuta.” (Wim. 8:8-10) Vilevile, Mukristo wa kweli mwenye kutazamia kuoa ao kuolewa, anapaswa kuchunga upendo wake na matendo yake ya mapenzi kwa ajili ya ule atakuwa bibi ao bwana yake.
Uzuri Wa Mwili
Biblia inaonyesha kama kuko uhusiano kati ya “utimamu wa akili,” ao akili nzuri, na kiasi. (1 Timotheo 2:9) Fikiria jambo hili: Watu wenye kiasi hawaone mambo kijuu-juu tu, hawahangaikie kupita kiasi namna wanaonekana ao sura yao, lakini wako na mawazo yenye kufaa juu yao wenyewe. Wanafikiria pia namna wengine wanajisikia; kwa hiyo watu wengine wanawafurahia, wanawaheshimia, na zaidi ya yote, wanakubaliwa na Mungu. (Mika 6:8) Zaidi ya hilo, wanaweza kuwa na marafiki wa kweli na kuvutia watu fulani wenye wanaweza kuwa bibi ao bwana zao wenye hawafikirie tu kitendo cha ndoa, lakini wenye wanafikiria pia ndoa yenye furaha na yenye kudumu.
Ndiyo sababu, Biblia iko na sababu nzuri ya kutushauri kukazia akili mutu wa ndani, ni kusema, ‘mutu wa siri wa moyoni.’ (1 Petro 3:3, 4) Uzuri wa ndani hauwezi kupotea hata siku moja. Uzuri huo unaendelea kuwa muzuri zaidi wakati miaka inaendelea kupita! Andiko la Methali 16:31 linasema hivi: ‘Kichwa chenye imvi ni taji la uzuri kinapopatikana katika njia ya uadilifu [ao, haki].’ Kwa hiyo, wakuwe vijana ao wazee, watu wenye kufuata mashauri mazuri ya Biblia watapata siri ya kuwa na uzuri wa kweli, heshima, na watakuwa wenye kutosheka.
Mali ya Kiroho
w06 15/11 uku. 18 fu. 4
Mambo Makubwa Katika Kitabu ya Wimbo wa Sulemani
2:7; 3:5—Juu ya nini Mushulami anaapisha “mabinti wa Yerusalemu kwa swala na paa wa pori”? Swala (gazelle) na paa wa pori ni banyama benye banajulikana juu ya buzuri yabo na fieri yenye banakuwaka nayo. Wakati Mushulami anaapisha mabinti wa Yerusalemu kwa swala na paa wa pori, anabaapisha njo kupitia bitu byote bya muzuri juu basilamushe ao kuchochea upendo ndani yake.
Hotuba: Biblia Inasema Nini Juu ya Kujipodoa na Kuvaa Vitu vya Kujipamba?
ijwbq habari ya 131
Biblia Inasema Nini juu ya Kujipodoa na Kuvaa Vitu vya Kujipamba?
Jibu la Biblia
Hata kama haitoe maelezo mengi juu ya habari hiyo, Biblia haikataze kujipodoa, kuvaa vitu vya kujipamba ao aina ingine ya kujipamba. Lakini, kuliko kukazia sura ya inje, Biblia inakazia zaidi “vazi lisiloharibika la roho ya utulivu na ya upole.”—1 Petro 3:3, 4.
Haiko mubaya kujipamba
Wanawake waaminifu wenye kuzungumuziwa katika Biblia walijipamba. Rebeka, mwenye aliolewa na Isaka mutoto wa Abrahamu, alivaa pete ya zahabu kwenye pua, vikomo vya zahabu, na vitu vingine vya kujipamba vya bei vyenye alipewa kama zawadi kutoka kwa ule mwenye angekuwa baba mukwe wake. (Mwanzo 24:22, 30, 53) Vilevile, Esta alikubali vitu vya kumufanya akuwe na sura na umbo la muzuri zaidi ili kujitayarisha kwa ajili ya daraka kubwa la kuwa malkia ao bibi ya mufalme wa Utawala wa Perse. (Esta 2:7, 9, 12) Pengine hilo lilitia ndani kutumia “vitu mbalimbali vya kujipodoa.”—New International Version; Easy-to-Read Version.
Mifano ya Biblia inatumia vitu vya kujipamba ili kulinganisha mambo fulani ya muzuri. Kwa mufano, mutu mwenye kutoa mashauri ya muzuri analinganishwa na ‘pete ya pambo la zahabu . . . kwenye sikio linalosikia.’ (Methali 25:12) Vilevile, Mungu mwenyewe alijilinganisha namna alikuwa anatendea taifa la Israeli na bwana mwenye kupamba bibi yake na vikomo, vitu vya kuvaa kwenye shingo, na vitu vya kuvaa kwenye masikio. Mapambo hayo yalifanya taifa hilo likuwe ‘murembo [ao lenye kupendeza] sana.’—Ezekieli 16:11-13.
Mawazo ya uwongo juu ya kujipodoa na kuvaa vitu vya kujipamba
Mawazo ya uwongo: Kwenye 1 Petro 3:3, Biblia inakataza “kusuka nywele kwa nje na kule kujivika mapambo ya zahabu.”
Kweli: Maneno yenye kuwa juu na chini ya andiko hilo yanaonyesha kama Biblia inakazia faida ya uzuri wa ndani wenye kuwa tofauti na sura ya muzuri ao mapambo. (1 Petro 3:3-6) Tofauti hiyo inazungumuziwa pia mahali pengine katika Biblia.—1 Samweli 16:7; Methali 11:22; 31:30; 1 Timotheo 2:9, 10.
Mawazo ya uwongo: Kwa sababu Yezebeli, malkia mubaya sana alikuwa anatia rangi kwenye macho yake, hilo linaonyesha kama kutia rangi kwenye macho ni mubaya.—2 Wafalme 9:30.
Kweli: Yezebeli mwenye alikuwa anafanya ulozi na kuua watu, alihukumiwa kwa sababu ya matendo yake ya mubaya, haiko kwa sababu ya sura yake.—2 Wafalme 9:7, 22, 36, 37.
TAREHE 17-23/11
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU WIMBO WA SULEMANI 6-8
Ukuwe Ukuta, Hapana Mulango
Upendo wa Kweli Unawezekana?
Soma Wimbo wa Sulemani 4:12. Sababu gani muchungaji analinganisha mupenzi wake na “bustani” yenye kufungwa? Ni kwa sababu si kila mutu anaweza kuingia katika bustani yenye kufungwa. Ili mutu aingie humo anapaswa kufungua kwanza mulango. Mwanamuke Mushulami analinganishwa na bustani yenye kufungwa kwa sababu upendo wake ulikuwa tu wa ule muchungaji, mwenye atakuwa bwana yake. Alikataa vishawishi vyote vya mufalme; kwa hiyo hakuwa ‘mulango’ wenye kufunguliwa kwa kila mutu, lakini alikuwa “ukuta.” (Wim. 8:8-10) Vilevile, Mukristo wa kweli mwenye kutazamia kuoa ao kuolewa, anapaswa kuchunga upendo wake na matendo yake ya mapenzi kwa ajili ya ule atakuwa bibi ao bwana yake.
Wakati muchungaji alitaka waende na Mushulami kufanya matembezi, ndugu zake walimukatalia; na wakamupatia kazi ya kuchunga shamba lao la mizabibu. Sababu gani? Tunaweza kusema kwamba hawakumuaminia? Ao, kwamba waliwaza atafanya uasherati? Hapana, walikuwa tu waangalifu ili dada yao asiangukie katika mutego wa zambi. (Wim. 1:6; 2:10-15) Fundisho: Wale wenye kuchumbiana wanapaswa kuwa waangalifu ili wasifanye jambo lolote mbaya. Wanapaswa kuepuka kuwa pekee yao. Hata kama kuonyeshana upendo wenye kufaa ni jambo la kawaida, wanapaswa kuwa waangalifu ili wasiangukie katika mutego wa zambi.
yp uku. 188 fu. 2
Kufanya Ngono Mbele ya Kufunga Ndoa
Ni kweli kama kuepuka kufanya ngono mbele ya kufunga ndoa inasaidiaka sana bijana kuepuka matokeo ya mubaya, lakini haiko ile tu. Biblia inazungumuzia kijana mwanamuke moya mwenye aliepuka kufanya ngono mbele ya kuolewa hata kama alikuwa namupenda sana muchumba wake. Njo maana alifikia hata kusema: “Mimi ni ukuta, na maziwa yangu ni kama minara.” Wakati balikuwa namukaza kufanya ngono, Mushulami hakukuwa sawa “mulango” wenye kuwa mwepesi ‘kufungula’. Alikuwa sawa ukuta wa nguvu wenye haukukuwa mwepesi kubomola! Alistahili kabisa kuitwa “mwenye kuwa safi,” na alikuwa na sheria ya kusema hivi juu ya mwenye angefikia kuwa bwana yake: “Mbele ya macho yake nimekuwa kama mutu mwenye anapata amani.” Ile amani ya moyo yenye alikuwa nayo ilifanya bote bawili batosheke.—Wimbo wa Sulemani 6:9, 10; 8:9, 10.
yp2-SW uku. 33
Mfano wa Kuigwa—Mshulami
Msichana Mshulami anajua kwamba anahitaji kuwa na akili timamu katika mambo ya mahaba. Anawaambia wenzake: “Nimewaapisha ninyi, . . . msijaribu kuamsha au kuwasha upendo ndani yangu mpaka wenyewe utake.” Mshulami anajua kwamba hisia zinaweza kulemea akili kwa urahisi. Kwa mfano, anajua kwamba huenda wengine wakamsukuma akubali kutongozwa na mtu asiyemfaa. Hata hisia zake mwenyewe zingeweza kupumbaza akili zake. Kwa hiyo Mshulami anaazimia kuwa kama “ukuta.”—Wimbo wa Sulemani 8:4, 10.
Je, maoni yako kuhusu upendo yanaonyesha ukomavu kama wa Mshulami huyo? Je, unaweza kutumia akili badala ya kuvutwa tu na hisia? (Methali 2:10, 11) Nyakati nyingine, huenda wengine wakakusukuma uanzishe urafiki na mtu fulani kabla hujawa tayari. Huenda hata hisia zako mwenyewe zikakusukuma. Kwa mfano, unapoona mvulana na msichana wakitembea wakiwa wameshikana mikono, je, unatamani sana kuwa katika uhusiano kama huo? Je, ungekubali kuwa na urafiki na mtu ambaye imani yake ni tofauti na yako? Msichana Mshulami alionyesha ukomavu katika mambo ya mahaba. Wewe pia unaweza kuonyesha ukomavu!
Mali ya Kiroho
w23.05 uku. 20 fu. 1, maelezo ya chini
Usiache “Mwali Wa Moto wa Yah” Uzimike
Upendo wa kweli wenye hauwezi kubadilika na wa milele unaitwa “mwali wa moto wa Yah” juu Yehova njo Chanzo ya ule upendo.
Onyesho: Je, Mashahidi wa Yehova Wana Sheria Kuhusu Urafiki wa Kimapenzi?
ijwfq-SW habari ya 43
Je, Mashahidi wa Yehova Wana Sheria Kuhusu Urafiki wa Kimapenzi?
Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba kanuni na amri zinazopatikana katika Biblia zinatusaidia kufanya maamuzi yanayompendeza Mungu na zinatunufaisha. (Isaya 48:17, 18) Ingawa hatukubuni sheria hizo tunaishi kulingana nazo. Ona jinsi baadhi ya kanuni hizo zinavyotumika wakati wa urafiki wa kimapenzi.
Ndoa ni muungano wa kudumu. (Mathayo 19:6) Mashahidi wa Yehova wanaona urafiki wa kimapenzi kuwa jambo zito kwa sababu ni moja ya hatua zinazoongoza kwenye ndoa.
Urafiki wa kimapenzi ni kwa ajili ya wale tu walio na umri unaotosha kufunga ndoa. Wao ‘wamepita upeo wa ujana,’ au wakati ambapo tamaa ya ngono ni yenye nguvu zaidi.—1 Wakorintho 7:36.
Wanaoanzisha urafiki wa kimapenzi wanapaswa kuwa huru kufunga ndoa. Ingawa watu fulani wametalikiana kisheria, machoni pa Mungu hawako huru kufunga ndoa kwa sababu msingi pekee wa kutalikiana ambao Mungu anaruhusu ni uasherati.—Mathayo 19:9.
Wakristo wanaotaka kufunga ndoa wanaamriwa kuchagua mwenzi ambaye ni mwamini mwenzao. (1 Wakorintho 7:39) Mashahidi wa Yehova wanaelewa kwamba amri hii hairejelei mtu anayependezwa tu na yale tunayoamini bali anapaswa kuwa amebatizwa na anatenda kulingana na imani yetu. (2 Wakorintho 6:14) Tangu zamani Mungu amewaagiza waabudu wake wafunge ndoa na waamini wenzao tu. (Mwanzo 24:3; Malaki 2:11) Watafiti wamegundua kwamba amri hiyo ina faida.
Watoto wanapaswa kutii wazazi wao. (Methali 1:8; Wakolosai 3:20) Kwa watoto walio nyumbani, amri hiyo inatia ndani kutii maamuzi ya wazazi wao kuhusu urafiki wa kimapenzi. Huenda maamuzi hayo yakahusu umri ambao mwana au binti anaweza kuanzisha urafiki na mambo anayoruhusiwa kufanya.
Maadamu anafuata miongozo ya Kimaandiko, kila Shahidi anaweza kujiamulia ikiwa ataanzisha urafiki wa kimapenzi na atauanzisha na nani. Hilo linapatana na kanuni hii: “Kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe.” (Wagalatia 6:5) Hata hivyo, inapohusu urafiki wa kimapenzi, kwa hekima wengi hutafuta ushauri wa Shahidi mkomavu anayewatakia mema.—Methali 1:5.
Mambo mengi ambayo hufanywa na wale walio katika urafiki wa kimapenzi ni dhambi nzito. Kwa mfano, Biblia inatuamuru tuepuke uasherati. Uasherati unatia ndani matendo machafu kati ya watu ambao si wenzi wa ndoa, kama vile kupapasana sehemu za siri au kufanya ngono ya mdomo au ngono ya mkundu. (1 Wakorintho 6:9-11) Hata vitendo vinavyoamsha hamu ya ngono hadi kufika karibu sana kufanya ngono ni “uchafu” usiompendeza Mungu. (Wagalatia 5:19-21) Pia, mazungumzo yasiyofaa yenye “maneno machafu” yanashutumiwa katika Biblia.—Wakolosai 3:8.
Moyo (yule mtu wa ndani) ni wenye hila. (Yeremia 17:9) Unaweza kumwongoza mtu kufanya mambo anayojua ni makosa. Ili mioyo yao isiwapotoshe, watu walio na urafiki wa kimapenzi huepuka kuwa peke yao katika hali zenye kushawishi. Wanaweza kuamua kujiunga na kikundi cha marafiki au kuchagua mtu wa kuandamana nao. (Methali 28:26) Wakristo waseja wanaotafuta mwenzi wa ndoa wanatambua hatari ya kutafuta marafiki wa kimapenzi kupitia vituo vya Intaneti, na hasa hatari ya kuanzisha uhusiano na watu wasiowafahamu vizuri.—Zaburi 26:4.
Urafiki wa kimapenzi ni nini?
Urafiki wa kimapenzi unatia ndani jambo lolote linalofanywa na watu wawili linaloonyesha kwamba kuna upendezi wa kimahaba kati yao. Wanaweza kuwa kati ya watu au peke yao, maeneo ya wazi au faraghani, ana kwa ana, ama yanaweza kuwa ni mazungumzo ya simu au ujumbe wa simu. Mashahidi wa Yehova hawauoni urafiki huo kuwa ni kujifurahisha tu, bali ni aina ya uchumba, hatua muhimu inayoongoza kwenye ndoa.
TAREHE 24-30/11
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ISAYA 1-2
Musaada Kwa Bale Benye “Kulemewa na Kosa”
ip-1-SW uku. 14 fu. 8
Baba Mwenye Wana Waasi
Isaya aendelea na ujumbe wake wenye maneno makali kwa taifa la Yuda: “Ole wake, taifa lenye dhambi, watu wanaochukua mzigo wa uovu, wazao wa watenda mabaya, watoto wanaoharibu; wamemwacha BWANA, wamemdharau yeye aliye Mtakatifu wa Israeli, wamefarakana naye na kurudi nyuma.” (Isaya 1:4) Matendo maovu yaweza kuongezeka na kuwa mzigo wenye kulemea sana. Katika siku ya Abrahamu Yehova alizifafanua dhambi za Sodoma na Gomora kuwa “nzito sana.” (Mwanzo 18:20, Zaire Swahili Bible) Hali kama hiyo sasa ni dhahiri kwa watu wa Yuda, kwa maana Isaya asema kwamba ‘wanauchukua mzigo wa uovu.’ Kwa kuongezea, awaita “wazao wa watenda mabaya, watoto wanaoharibu.” Naam, Wayudea ni kama watoto wahalifu. “Wamefarakana [na Baba yao] na kurudi nyuma.”
Yehova Anapenda Batu Yote Batubu
Mara kwa mara Yehova alitumia manabii wake juu waonye na kurekebisha batu yake. Kwa mufano, Mungu alisema hivi kupitia nabii Yeremia: “Rudia, Ee Israeli mwenye kuasi . . . Sitakuangalia kwa kasirani, kwa maana mimi ni mushikamanifu . . . Sitaendelea kuwa na kinyongo milele. Isipokuwa tu ukubali hatia yako, kwa maana umemuasi Yehova.” (Yer. 3:12, 13) Kupitia Yoeli Yehova alisema hivi: “Murudie kwangu kwa mioyo yenu yote.” (Yoe. 2:12, 13) Alimuomba Isaya aseme hivi: “Mujinawishe, mujisafishe; muondoe matendo yenu maovu mbele ya macho yangu; muache kutenda mabaya.” (Isa. 1:16-19) Kupitia Ezekieli Yehova aliuliza hivi: “Je, ninafurahia kabisa kifo cha mutu muovu? . . . Je, mimi sifurahie kwamba aache njia zake naye aendelee kuishi? Sifurahie hata kidogo kifo cha mutu yeyote, . . . kwa hiyo mugeuke na kuishi.” (Eze. 18:23, 32) Yehova anafurahia kuona batu banatubu juu anapenda baishi milele. Kwa hiyo, Yehova hangoyake tu watenda-zambi wabadilike mbele akamate hatua ya kuwasaidia. Tuone mifano ingine yenye inaonyesha vile.
Mali ya Kiroho
ip-1 uku. 39 fu. 9
Kuinuliwa Kwa Nyumba ya Yehova
Leo, batumishi ya Mungu habakusanyikake tena ku mulima wenye kuwa na hekalu yenye kujengwa na majiwe, juu kwanza, Baroma baliharibu hekalu ya Yehova yenye ilikuwa Yerusalemu mu mwaka wa 70 K.K.Y. Tena, mutume Paulo alisemaka wazi kama tabenakulo na hekalu yenye ilikuwaka Yerusalemu bilikuwa tu nafananisha mambo yenye ingetokea. Bilikuwa nafananisha njo “hema ya kweli, yenye imesimamishwa na Yehova, hapana na mwanadamu.” (Waebrania 8:2) Ile hema ya kiroho ni mupango yenye Yehova alikamata juu tumukaribie mu ibada kupitia zabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo. (Waebrania 9:2-10, 23) Ile inafanya tuelewe kama “mulima wa nyumba ya Yehova” yenye Isaya 2:2 inazungumuzia, inafananisha ibada safi yenye tuko namutolea Yehova leo. Bale benye biko namutolea Yehova ibada safi habakutanake tena bote fasi fulani ya pekee mu dunia, lakini banaungana kupitia umoja wenye kuwa mu ibada yabo.
Hotuba: Zambi Ni Nini?
ijwbq habari ya 96
Zambi Ni Nini?
Jibu ya Biblia
Zambi ni tendo, hisia, ao wazo yenye inapingana na kanuni za Mungu. Mutu anafanya zambi wakati anavunja sheria ya Mungu, kwa kufanya mambo ya mubaya yenye Mungu hakubali. (1 Yohana 3:4; 5:17) Biblia inasema pia kama ni zambi kukosa kufanya mambo yenye tunajua kama ni ya muzuri.—Yakobo 4:17.
Mu luga zenye zilitumiwa juu ya kuandika Biblia, maneno yenye kutafsiriwa zambi inamaanisha “kutokufikia kusudi,” ao kutokufikia kitu yenye mutu alikuwa navizia. Kwa mufano, mu Israeli ya zamani mulikuwa kikundi ya maaskari wenye walikuwa najua sana kurusha majiwe, na walikuwa wanalenga kitu fulani “bila kukosea.” Kama maneno “bila kukosea” inatafsiriwa neno kwa neno, inaweza kuwa hivi: “Bila kufanya zambi.” (Waamuzi 20:16) Kwa hiyo, kufanya zambi ni kukosa kufikia kusudi ya kanuni kamilifu za Mungu, ao kushindwa kuzifuata.
Juu Mungu njo alituumba, iko na haki ya kututilia kanuni zenye tunapaswa kufuata. (Ufunuo 4:11) Tutatoa hesabu mbele yake juu ya matendo yetu.—Waroma 14:12.
Inawezekana kabisa kuepuka kufanya zambi?
Hapana. Biblia inasema kama “wote wamefanya zambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.” (Waroma 3:23; 1 Wafalme 8:46; Muhubiri 7:20; 1 Yohana 1:8) Juu ya nini?
Ku mwanzo, wanadamu wa kwanza, Adamu na Eva, hawakukuwa na zambi, juu wakati waliumbwa, walikuwa wakamilifu na waliumbwa kwa mufano wa Mungu. (Mwanzo 1:27) Lakini walipoteza ukamilifu wakati walikosa kumutii Mungu. (Mwanzo3:5, 6, 17-19) Wakati walizala watoto, waliwapitishia zambi na hali ya kutokamilika. (Waroma 5:12) Njo maana Mufalme Daudi wa Israeli alisema hivi: “Nilizaliwa nikiwa na hatia ya kosa.”—Zaburi 51:5.
Zambi fulani ni kubwa kuliko zingine?
Ndiyo. Kwa mufano, Biblia inasema kama watu wa Sodoma ya zamani walikuwa “waovu, na walikuwa wanatenda zambi nzito” na zambi zao zilikuwa “nzito sana.” (Mwanzo 13:13; 18:20) Tuone mambo tatu yenye inatusaidia kujua ukubwa wa zambi.
Uzito. Biblia inatuambia tuepuke zambi nzito sawa vile kufanya uasherati, kuabudu sanamu, kuiba, kulewa, kunyanganya, kuua, na kupashana habari na pepo wachafu. (1 Wakorinto 6:9-11; Ufunuo 21:8) Biblia inaonyesha kama zile zambi ziko tofauti na zambi zenye mutu anafanyaka bila kufikiri ao bila kukusudia, kwa mufano, maneno ao matendo yenye kuumiza wengine. (Mezali 12:18; Waefeso 4:31, 32) Lakini Biblia inatutia moyo tusizarau zile zambi zenye tunafanyaka bila kufikiri ao bila kukusudia juu zinaweza kutufikisha ku zambi nzito.—Matayo 5:27, 28.
Nia. Watu fulani wanafanyaka zambi juu hawajue sheria za Mungu. (Matendo 17:30; 1 Timoteo 1:13) Biblia haiseme kama, ikiwa mutu anafanya zambi na hajue, ni kusema hana kosa. Lakini inaonyesha kama mutu mwenye anafanya zambi bila kujua iko tofauti na ule mwenye anavunja sheria ya Mungu kimakusudi. (Hesabu 15:30, 31) Watu wenye kufanya zambi kimakusudi wanachochewa na “moyo muovu.”—Yeremia 16:12.
Ni mara ngapi zambi imefanywa. Tena Biblia inaonyesha kama kuko tofauti kati ya mutu mwenye anafanya zambi mara moya na mutu mwenye anafanya zambi kwa wakati murefu. (1 Yohana 3:4-8) Mungu atahukumu wale wenye ‘wanazoea kutenda zambi kimakusudi,’ hata kisha kujua mambo yenye kuwa sawa.—Waebrania 10:26, 27.
Wale wenye wamefanya zambi nzito wanaweza kusumbuliwa sana na zamiri kwa sababu ya zambi zenye walifanya. Kwa mufano, Mufalme Daudi aliandika hivi: “Kwa maana makosa yangu yamekuwa mengi sana juu ya kichwa changu; kama muzigo muzito, ni mengi sana siwezi kuyabeba.” (Zaburi 38:4) Lakini Biblia iko na hii maneno yenye kufariji: “Mutu muovu aache njia yake na mutu mubaya mawazo yake; na amurudilie Yehova, mwenye atamuonyesha rehema, kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.”—Isaya 55:7.
TAREHE 1-7/12
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ISAYA 3-5
Yehova Anastahili Utii Wetu
ip-1-SW uku. 73-74 fu. 3-5
Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!
Iwapo Isaya awaimbia kihalisi wasikilizaji wake mfano huo au la, huo kwa hakika wavuta fikira zao. Labda wengi wao wanafahamu kazi ya kupanda shamba la mizabibu, na ufafanuzi wa Isaya ni dhahiri na halisi. Sawa na wakuzao mizabibu leo, mmilikaji wa shamba la mizabibu apanda, si mbegu za zabibu, bali mzabibu “ulio mzuri [‘uliochaguliwa,’ BHN],” au “mzabibu mwekundu,” (NW) ulio bora—kitawi au mche kutoka kwa mzabibu mwingine. Kwa kufaa, yeye apanda mizabibu “kilimani penye kuzaa sana,” mahali ambapo shamba la mizabibu litasitawi.
Kazi ngumu yahitajika ili shamba la mizabibu lizae. Isaya aeleza kuwa mmilikaji ‘afanya handaki [“alililima vizuri,” BHN] shamba na kutoa mawe yake’—kazi ngumu, yenye kuchosha sana! Yaelekea atumia mawe yaliyo makubwa ‘kujenga mnara.’ Nyakati za kale, minara hiyo ilikuwa vituo vya walinzi walioilinda mimea dhidi ya wezi na wanyama. Pia, ajenga ukuta wa mawe ili kuyazunguka matuta ya shamba hilo la mizabibu. (Isaya 5:5) Mara nyingi hilo lilifanywa ili kuzuia mmomonyoko wa udongo wa juu ulio muhimu.
Baada ya kufanya kazi kwa bidii ili kulilinda shamba lake la mizabibu, mmilikaji ana haki ya kulitazamia lizae matunda. Kwa kutazamia hilo, yeye achimba shinikizo la divai. Lakini je, mavuno yanayotarajiwa yatokea? La, shamba hilo la mizabibu lazaa zabibu-mwitu.
ip-1-SW uku. 76 fu. 8-9
Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!
Isaya amwita Yehova, aliye mmilikaji wa shamba la mizabibu, “mpenzi wangu.” (Isaya 5:1) Isaya aweza tu kumtaja Mungu kwa njia hiyo yenye urafiki kwa sababu ana uhusiano wa karibu pamoja Naye. (Linganisha Ayubu 29:4; Zaburi 25:14.) Hata hivyo, upendo wa nabii huyo kwa Mungu hauwezi kulingana na upendo ambao Mungu ameonyesha “shamba lake la mizabibu”—taifa ‘alilolipanda.’—Linganisha Kutoka 15:17; Zaburi 80:8, 9.
Yehova ‘alilipanda’ taifa lake katika nchi ya Kanaani na kuwapa sheria na kanuni zake, zilizokuwa kama ukuta wa kuwalinda ili mataifa mengine yasiwafisidi. (Kutoka 19:5, 6; Zaburi 147:19, 20; Waefeso 2:14) Pamoja na hayo, Yehova aliwapa waamuzi, makuhani, na manabii wa kuwafundisha. (2 Wafalme 17:13; Malaki 2:7; Matendo 13:20) Israeli ilipotishwa kwa uvamizi wa kijeshi, Yehova aliinua wakombozi. (Waebrania 11:32, 33) Kwa kufaa, Yehova auliza: “Je! ni kazi gani iliyoweza kutendeka ndani ya shamba langu la mizabibu nisiyoitenda?”
w06-SW 15/6 uku. 18 fu. 1
‘Utunze Mzabibu Huu’!
Isaya aliifananisha “nyumba ya Israeli” na shamba la mzabibu ambalo hatua kwa hatua lilizaa “zabibu-mwitu” au zabibu zilizooza. (Isaya 5:2, 7) Zabibu-mwitu ni ndogo kuliko zabibu za shambani na hazina nyama nyingi, nazo mbegu zake huchukua nafasi kubwa ya tunda. Zabibu-mwitu haziwezi kutumiwa kutengeneza divai wala kuliwa. Huo ni mfano mzuri unaowakilisha taifa lililoasi imani ambalo matunda yake yalikuwa ni uvunjaji wa sheria badala ya uadilifu. Si Mkulima wa mizabibu aliyetokeza matunda hayo yasiyofaa. Yehova alifanya yote awezayo ili kufanya taifa hilo lizae matunda. Aliuliza hivi: “Kuna kitu gani ambacho bado sijalifanyia shamba langu la mizabibu, ambacho bado sijafanya ndani yake?”—Isaya 5:4.
w06-SW 15/6 uku. 18 fu. 2
‘Utunze Mzabibu Huu’!
Kwa kuwa mzabibu wa Israeli haukuwa unazaa, Yehova alionya kwamba angevunja ukuta wa ulinzi aliokuwa amejenga kuzunguka watu wake. Kamwe hangepunguza tena matawi ya mzabibu huo wa mfano wala kuulimia. Mvua ya majira ya kuchipua ambayo mmea huo ulitegemea haingenyesha, na miiba na magugu yangejaa katika shamba hilo la mizabibu.—Isaya 5:5, 6.
Mali ya Kiroho
ip-1 uku. 80 fu. 18-19
Ole Kwa Shamba ya Mizabibu Yenye Kukosa Uaminifu!
Mu Israeli ya zamani, inchi muzima ilikuwa ya Yehova. Alipatiaka kila familia ya Baisraeli uriti wa sehemu ya inchi, na alibaambiaka kama bangeweza kupangisha ao kuipatia mutu mwingine kwa wakati fulani tu, lakini alibakatazaka kuiuzisha “kwa muda wa kudumu.” (Walawi 25:23) Ile sheria ilikuwa nasaidia mutu aepuke kukamata ao kunyanganya sehemu ya inchi yenye haikukuwa ya familia yake. Tena, ilikuwa nasaidia sana batu ya mafamilia juu basiangukie mu bumaskini ya nguvu. Lakini mu Yuda, Baisraeli fulani balikuwa na tamaa na balikuwa navunja ile sheria. Balikuwa nafanya nini? Mika aliandika hivi: “Wanatamani mashamba na kuyanyanganya; pia nyumba, na kuzikamata; na wanamunyanganya mutu nyumba yake kwa udanganyifu, na uriti wake.” (Mika 2:2) Lakini Mezali 20:21 inatuonya hivi: “Uriti wenye unapatikana kwanza kwa pupa mwishowe hautakuwa baraka.”
Yehova aliahidi kunyanganya bale batu benye tamaa ile masehemu ya inchi yenye haikukuwa yabo. Alisema pia kama manyumba yenye balinyanganya ‘ingeachwa na kubakia kama jangwa’. Tena, masehemu ya inchi yenye balinyanganya haingekuwa tena na mboleo. Maandiko haiseme wazi namna gani na wakati gani njo ile laana ilipaswa kutimia. Lakini inawezekana ilitimia kwa sehemu fulani wakati Baisraeli balipelekwa mu uhamisho Babiloni.—Isaya 27:10.
TAREHE 8-14/12
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ISAYA 6-8
“Mimi Huyu! Unitume Mimi!”
ip-1-SW uku. 94-95 fu. 13-14
Yehova Mungu Yumo Katika Hekalu Lake Takatifu
Basi na tusikilize pamoja na Isaya. “Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.” (Isaya 6:8) Kwa wazi, swali la Yehova limekusudiwa kujibiwa na Isaya, kwa sababu hakuna nabii mwingine wa kibinadamu aonekanaye katika ono hilo. Pasipo shaka hilo ni ombi kwa Isaya awe mjumbe wa Yehova. Lakini kwa nini Yehova auliza, “Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?” (Italiki ni zetu.) Kwa kubadili neno la umoja “nimtume” hadi neno la wingi “yetu,” Yehova sasa ajihusisha na angalau mtu mmoja mwingine. Nani huyo? Je, huyo siye Mwana wake mzaliwa-pekee, ambaye baadaye alikuja kuwa mwanamume Yesu Kristo? Kwa kweli, huyo ndiye Mwana yuleyule ambaye Mungu alimwambia, “Na tumfanye mtu kwa mfano wetu.” (Mwanzo 1:26; Mithali 8:30, 31) Naam, Mwana wake mzaliwa-pekee ndiye aliye katika makao ya mbinguni pamoja na Yehova.—Yohana 1:14.
Isaya hasiti kuitikia! Haidhuru ni ujumbe wa aina gani, yeye ajibu kwa haraka: “Mimi hapa, nitume mimi.” Wala haulizi faida ambayo labda atapata kwa kukubali mgawo huo. Roho yake ya utayari ni kielelezo chema kwa watumishi wote wa Mungu leo, walio na utume wa kuhubiri ‘habari njema hii ya ufalme katika dunia yote inayokaliwa.’ (Mathayo 24:14) Kama vile Isaya, wao washikamana na mgawo wao kwa uaminifu nao watimiza “ushahidi kwa mataifa yote,” licha ya kutoitikia kulikoenea kotekote. Nao wasonga mbele katika tumaini, kama vile Isaya, kwa sababu wanajua kuwa utume wao umeidhinishwa na mamlaka kuu kupita zote.
ip-1-SW uku. 95-96 fu. 15-16
Yehova Mungu Yumo Katika Hekalu Lake Takatifu
Yehova sasa atoa muhtasari wa mambo ambayo Isaya apaswa kusema na vile yatakavyopokewa: “Enenda, ukawaambie watu hawa, Fulizeni kusikia, lakini msifahamu; fulizeni kutazama, lakini msione. Uunoneshe moyo wa watu hawa, ukayatie uzito masikio yao, ukayafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa.” (Isaya 6:9, 10) Je, hayo yamaanisha kuwa Isaya apaswa kusema kwa kutojali na kukosa busara na kuwavunja moyo Wayahudi, hivyo awatenganishe na Yehova? Hata kidogo! Hao ni watu wa Isaya mwenyewe naye ana huruma ya kidugu kwao. Lakini maneno ya Yehova yaonyesha namna watu watakavyoupokea ujumbe wake, haidhuru ni kwa uaminifu jinsi gani Isaya atimiza kazi yake.
Watu ndio wenye lawama. Isaya ‘atafuliza’ kusema nao, bali hawataukubali ujumbe huo wala kupata ufahamu. Wengi wao watakuwa wakaidi na wasioitikia, kama vipofu na viziwi kabisa. Kwa kufuliza kuwaendea, Isaya atawaruhusu “watu hawa” waonyeshe kuwa hawataki kufahamu. Watathibitisha kuwa wanafunga akili na mioyo yao zisisikie ujumbe wa Isaya—ujumbe wa Mungu—kwao. Jinsi watu leo walivyo vivyo hivyo! Wengi sana kati yao hukataa kuwasikiliza Mashahidi wa Yehova wahubiripo habari njema ya Ufalme wa Mungu unaokuja.
ip-1-SW uku. 99 fu. 23
Yehova Mungu Yumo Katika Hekalu Lake Takatifu
Kwa kunukuu kitabu cha Isaya, Yesu alikuwa akionyesha kuwa unabii huo una utimizo fulani katika siku yake. Mtazamo wa moyo wa watu kwa jumla ulikuwa kama wa Wayahudi katika siku ya Isaya. Walijifanya vipofu na viziwi wasipate ujumbe wake nao vivyo hivyo wakaharibiwa. (Mathayo 23:35-38; 24:1, 2) Hilo lilitukia wakati ambapo majeshi ya Roma yakiongozwa na Jenerali Tito yalishambulia Yerusalemu mwaka wa 70 W.K. na kulibomoa jiji hilo na hekalu lake. Ingawa hivyo, baadhi ya watu walikuwa wamemsikiliza Yesu na kuwa wanafunzi wake. Yesu aliwatangaza hao kuwa ‘wenye furaha.’ (Mathayo 13:16-23, 51) Alikuwa amewajulisha kuwa waonapo “Yerusalemu limezingirwa na majeshi yaliyopiga kambi,” yawapasa “[kuanza] kukimbia hadi kwenye milima.” (Luka 21:20-22) Kwa hiyo, “mbegu takatifu” iliyokuwa imedhihirisha imani na iliyokuwa imefanywa kuwa taifa la kiroho, “Israeli wa Mungu,” iliokolewa.—Wagalatia 6:16.
Mali ya Kiroho
w06 1/12 uku. 9 fu. 4
Mambo Makubwa Katika Kitabu ya Isaya—I
7:3, 4—Juu ya nini Yehova alimuokoaka Mufalme Ahazi hata kama alikuwaka Mufalme mubaya? Bafalme ya Siria na Israeli balikuwa napanga kutosha Mufalme Ahazi ku kiti ya ufalme juu ya kumuweka mutoto wa Tabeeli pa nafasi yake. Lakini, ule Tabeeli hakukuwa wa mu kizazi ya Daudi. Sasa kama ule mutoto yake angefikia kuwa mufalme, ile ingefanya agano yenye Yehova alifanyaka na Daudi isitimie. Njo maana Yehova alimuokoa Ahazi juu ya kulinda kizazi kya Daudi mwenye mungepaswa kutoka “Mukubwa wa Amani”.—Isaya 9:6.
TAREHE 15-21/12
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ISAYA 9-10
“Mwangaza Mukubwa” Ulitabiriwa
ip-1-SW uku. 126 fu. 16-17
Ahadi ya Mkuu wa Amani
Naam, “zamani za mwisho” alizotabiri Isaya ni wakati wa huduma ya Kristo duniani. Yesu alitumia wakati mwingi wa maisha yake duniani akiwa Galilaya. Alianza huduma yake katika wilaya ya Galilaya na kutangaza: “Ufalme wa mbingu umekaribia.” (Mathayo 4:17) Huko Galilaya, alitoa Mahubiri ya Mlimani yaliyo maarufu sana, akawachagua mitume wake, akafanya mwujiza wake wa kwanza, na kuonekana kwa wafuasi wapatao 500 baada ya ufufuo wake. (Mathayo 5:1–7:27; 28:16-20; Marko 3:13, 14; Yohana 2:8-11; 1 Wakorintho 15:6) Hivyo, Yesu alitimiza unabii wa Isaya kwa kuitukuza “nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali.” Bila shaka, Yesu hakuhudumia watu wa Galilaya peke yao. Kwa kuhubiri habari njema nchini kote, Yesu ‘alilifanya kuwa tukufu’ taifa lote la Israeli, kutia ndani Yuda.
Hata hivyo, namna gani kuhusu mtajo wa Mathayo juu ya “nuru kubwa” katika Galilaya? Huo pia ulinukuliwa katika unabii wa Isaya. Isaya aliandika: “Watu wale waliokwenda katika giza wameona nuru kuu; wale waliokaa katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewaangaza.” (Isaya 9:2) Kufikia karne ya kwanza W.K., nuru ya ile kweli ilikuwa imefichwa na mambo ya kipagani yasiyo ya kweli. Wayahudi waliokuwa viongozi wa kidini walikuwa wamelizidisha tatizo hilo kwa kushikilia mapokeo yao ya kidini ‘yaliyolibatilisha neno la Mungu.’ (Mathayo 15:6) Wanyenyekevu walionewa na kutatanishwa, huku wakifuata “viongozi vipofu.” (Mathayo 23:2-4, 16) Yesu Mesiya alipokuja, macho ya watu wengi wanyenyekevu yalifunguliwa kiajabu. (Yohana 1:9, 12) Kazi ya Yesu akiwa duniani na baraka zilizotokana na dhabihu yake zafananishwa ipasavyo na “nuru kuu” katika unabii wa Isaya.—Yohana 8:12.
ip-1-SW uku. 128 fu. 18-19
Ahadi ya Mkuu wa Amani
Wale walioitikia nuru hiyo walikuwa na sababu nyingi za kufurahi. Isaya aliendelea: “Umeliongeza taifa, umezidisha furaha yao; Wanafurahi mbele zako, kama furaha ya wakati wa mavuno, kama watu wafurahivyo wagawanyapo nyara.” (Isaya 9:3) Kuhubiri kwa Yesu na kule kwa wafuasi wake kulitokeza wenye moyo wa haki, walioonyesha hamu ya kumwabudu Yehova kwa roho na kweli. (Yohana 4:24) Katika muda unaopungua miaka minne, umati ulikubali Ukristo. Elfu tatu walibatizwa katika siku ya Pentekoste mwaka wa 33 W.K. Muda mfupi baadaye, “idadi ya wanaume ikawa karibu elfu tano.” (Matendo 2:41; 4:4) Wanafunzi walipozidi kudhihirisha nuru kwa bidii, “idadi ya wanafunzi ikafuliza kuzidi sana katika Yerusalemu; na umati mkubwa wa makuhani ukaanza kuwa mtiifu kwa imani.”—Matendo 6:7.
Sawa na wale wanaoshangilia kupata mavuno mengi au wanaofurahia kugawanya nyara yenye thamani baada ya ushindi mkubwa wa kijeshi, wafuasi wa Yesu walishangilia kwa sababu ya ongezeko. (Matendo 2:46, 47) Baadaye, Yehova aliifanya nuru ing’ae katika mataifa. (Matendo 14:27) Kwa hiyo watu wa jamii mbalimbali wakashangilia kwa sababu njia ya kumkaribia Yehova ilikuwa imefunguliwa kwao.—Matendo 13:48.
ip-1-SW uku. 128-129 fu. 20-21
Ahadi ya Mkuu wa Amani
Matokeo ya utendaji wa Mesiya ni ya kudumu, kama tuonavyo katika maneno yafuatayo ya Isaya: “Umeivunja nira ya mzigo wake, na gongo la bega lake, na fimbo yake yeye aliyemwonea, kama katika siku ya Midiani.” (Isaya 9:4) Karne kadhaa kabla ya siku ya Isaya, Wamidiani walipanga njama na Wamoabi ili kushawishi Israeli watende dhambi. (Hesabu 25:1-9, 14-18; 31:15, 16) Baadaye, Wamidiani waliwatisha Waisraeli kwa kuvamia na kupora vijiji na mashamba yao kwa miaka saba. (Waamuzi 6:1-6) Ndipo Yehova, kupitia Gideoni mtumishi wake, akayashinda kabisa majeshi ya Midiani. Baada ya “siku [hiyo] ya Midiani,” hakuna uthibitisho uonyeshao kuwa watu wa Yehova waliteseka tena mikononi mwa Wamidiani. (Waamuzi 6:7-16; 8:28) Katika wakati ujao ulio karibu, Yesu Kristo, Gideoni mkuu, atawatwanga na kuwaua adui za watu wa Yehova leo. (Ufunuo 17:14; 19:11-21) Kisha, “kama katika siku ya Midiani,” ushindi kamili na udumuo milele utapatikana kwa nguvu za Yehova, wala si kwa uwezo wa binadamu. (Waamuzi 7:2-22) Watu wa Mungu hawatateseka tena kamwe chini ya nira ya uonevu!
Wonyesho wa nguvu za Mungu si utukuzaji wa vita. Yesu aliyefufuliwa ndiye Mkuu wa Amani, naye ataleta amani ya milele kwa kuwaharibu adui zake. Isaya sasa asema juu ya zana za kijeshi kuharibiwa kabisa kwa moto: “Silaha zote za mtu mwenye silaha wakati wa mshindo [“kila buti ya akanyagaye kwa mtetemo,” “NW”], na mavazi yaliyofingirishwa katika damu, yatakuwa tayari kuteketezwa, yatakuwa kuni za kutiwa motoni.” (Isaya 9:5) Mitetemo inayosababishwa na kukanyaga kwa buti za wanajeshi walio mwendoni haitasikika tena kamwe. Yunifomu zenye damu za askari waliozoea vita hazitaonekana tena. Vita havitakuwapo tena kamwe!—Zaburi 46:9.
Mali ya Kiroho
w25.07 uku. 10, kisanduku
Namna ya Kutoa Mashauri
Ona mambo fulani yenye inafanya Yesu akuwe “Mushauri wa Ajabu,” na namna tunaweza kuiga mufano wake.
Yesu alijua mambo ya kusema. Kila siku, Yesu alijua jambo ya muzuri ya kusema juu mashauri yake ilitegemea hekima ya Yehova hapana hekima yake mwenyewe. Aliambia banafunzi yake hivi: “Mambo yenye ninawaambia ninyi, siyaseme kwa kujitungia mimi mwenyewe.”—Yoh. 14:10.
Jambo yenye tunajifunza: Hata kama tulishakomala na tunajua mambo ya mingi, tunapaswa kuhakikisha kama mashauri yetu inategemea Neno ya Mungu, hapana mawazo yetu.
Yesu alijua wakati wa kupana shauri. Hakuambia banafunzi mu siku moya mambo yote yenye balikuwa na lazima ya kujua. Lakini Yesu alikuwa nachunga wakati ya muzuri ya kushauria banafunzi yake. Na alikuwa nabaambia tu mambo yenye banaweza kuelewa.—Yoh. 16:12.
Jambo yenye tunajifunza: Kama tunapenda kushauria mutu, ni muzuri tuchunge mupaka tupate “wakati [wa muzuri] wa kusema.” (Muh. 3:7) Kama tunaambia mutu mambo ya mingi sana, anaweza kukosa afanye nini na anaweza kuvunjika moyo. Tumuambie tu mambo yenye iko na lazima ya kujua kupatana na hali yake.
Yesu alijua namna ya kusema. Alishauria mitume wake mara mingi juu waonyeshe unyenyekevu. Kila mara alifanya vile kwa upole na kwa heshima.—Mt. 18:1-5.
Jambo yenye tunajifunza: Hata kama inaomba tushaurie mutu tena na tena juu ya jambo fulani, ni muzuri kila mara tuseme kwa upole na kwa heshima.
Onyesho: Mashahidi wa Yehova Balibadilishaka Biblia Juu Ipatane na Byenye Banaamini?
ijwfq-SW habari ya 35
Je, Mashahidi wa Yehova Wameibadili Biblia Ili Ifaane na Mambo Wanayoamini?
La, hatujafanya hivyo. Kinyume na hilo, mara tu tunapogundua kwamba jambo fulani tunaloamini halipatani na yale ambayo Biblia inasema, tunaacha kuamini jambo hilo.
Tulichunguza Neno la Mungu kwa makini miaka mingi hata kabla ya kuchapisha Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika mwaka wa 1950. Tulitumia tafsiri za Biblia zilizokuwepo ili kutegemeza mafundisho yetu. Hebu tufikirie baadhi ya mambo ambayo Mashahidi wa Yehova wameamini kwa miaka mingi, na ujaribu kuona ikiwa mambo hayo yanapatana kabisa na mambo ambayo Biblia inafundisha hasa.
Jambo tunaloamini: Mungu si utatu. Gazeti la Zion’s Watch Tower la Julai 1882 lilisema hivi: “Wasomaji wetu wanajua kwamba, ingawa tunamwamini Yehova na Yesu, na pia Roho takatifu, tunakataa kabisa fundisho la kuwa kuna Miungu watatu ndani ya mtu mmoja, au kama wanavyosema wengine, Mungu mmoja ndani ya watu watatu kwa sababu hilo si fundisho la Biblia.”
Biblia inasema nini? “Jehova Mwenyiezi Mngu wetu, Jehova ni mmoja.” (Kumbukumbu la Torati 6:4, The Old Testament in Swahili, [Mombasa]) “Kwetu sisi Mungu ni mmoja tu, aliye Baba, ambaye vitu vyote vimetoka kwake, nasi tunaishi kwake; yuko na Bwana mmoja Yesu Kristo, ambaye kwake vitu vyote vimekuwapo, na sisi kwa yeye huyo.” (1 Wakorintho 8:6, Union Version) Yesu mwenyewe alisema: “Baba ni mkuu kuliko mimi.”—Yohana 14:28, Douay-Rheims Version.
Jambo tunaloamini: Wanadamu hawateseki milele katika moto wa mateso. Likinukuu andiko la Waroma 6:23 kutoka kwenye tafsiri ya King James Version, gazeti la Zion’s Watch Tower la Juni 1882 lilikuwa na kichwa “Mshahara wa Dhambi Ni Kifo,” na lilisema: “Maneno hayo ni mepesi kuelewa na yako wazi kabisa. Inashangaza kwamba wengi wanaokiri kuipokea Biblia kama Neno la Mungu huendelea kupingana na maneno hayo ya kweli huku wakisisitiza kwamba Biblia inafundisha kuwa mshahara wa dhambi ni uzima wa milele katika mateso.”
Biblia inasema nini? “Nafsi itendayo dhambi, itakufa.” (Ezekieli 18:4, 20, King James Version) Adhabu ya mwisho ambayo wale wanaompinga Mungu watapata si kuteswa milele, bali “maangamizi ya milele.”—2 Wathesalonike 1:9, Bible in Swahili.
Jambo tunaloamini: Ufalme wa Mungu ni serikali halisi, si hali fulani iliyo moyoni mwa mtu. Gazeti la Zion’s Watch Tower la Desemba 1881 lilisema: “Bila shaka kusimamishwa kwa ufalme huu, kutahusisha kupinduliwa kwa falme zote za dunia.”
Biblia inasema nini? “Katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele: bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.”—Danieli 2:44, Union Version.
Je, Mashahidi wa Yehova wanategemea Biblia ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ili kutetea mambo wanayoamini?
Hapana, kwa sababu tunapowahubiria watu sisi hutumia tafsiri nyinginezo za Biblia. Isitoshe, ingawa sisi huwapa watu Biblia ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya bila malipo ikiwa sehemu ya kazi yetu ya elimu ya bure ya Biblia, tunafurahia kujifunza na wale ambao wangependa kutumia tafsiri nyinginezo za Biblia pia.
TAREHE 22-28/12
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ISAYA 11-13
Biblia Ilisema Nini Juu ya Mwenye Angefikia Kuwa Masiya?
ip-1-SW uku. 159 fu. 4-5
Wokovu na Kushangilia Chini ya Utawala wa Mesiya
Karne kadhaa kabla ya wakati wa Isaya, Waebrania wengine walioandika Biblia walitaja kuja kwa Mesiya, Kiongozi wa kweli, ambaye Yehova angemtuma kwa Israeli. (Mwanzo 49:10; Kumbukumbu la Torati 18:18; Zaburi 118:22, 26) Sasa kupitia Isaya, Yehova aongeza mambo ya ziada. Isaya aandika: “Litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.” (Isaya 11:1; linganisha Zaburi 132:11.) Maneno “chipukizi” na “tawi” yaonyesha kuwa Mesiya atakuwa mzao wa Yese kupitia Daudi mwana wake, aliyetiwa mafuta awe mfalme wa Israeli. (1 Samweli 16:13; Yeremia 23:5; Ufunuo 22:16) Mesiya wa kweli awasilipo, “tawi” hilo, la nyumba ya Daudi, litazaa matunda mema.
Yesu ndiye Mesiya aliyeahidiwa. Mathayo, mwandikaji wa gospeli, alirejezea maneno ya Isaya 11:1 aliposema kwamba Yesu alipoitwa “Mnazareti,” jina hilo lilitimiza maneno ya manabii. Kwa kuwa Yesu alilelewa mjini Nazareti, aliitwa Mnazareti, jina ambalo labda lahusiana na neno la Kiebrania lililotumiwa katika Isaya 11:1, yaani, “tawi.”b—Mathayo 2:23, NW, kielezi-chini; Luka 2:39, 40.
ip-1-SW uku. 159 fu. 6
Wokovu na Kushangilia Chini ya Utawala wa Mesiya
Mesiya atakuwa mtawala wa aina gani? Je, atakuwa kama Mwashuri mkatili, mshupavu, anayeharibu ufalme wa kaskazini wa Israeli wenye makabila kumi? Sivyo hata kidogo. Isaya asema hivi kumhusu Mesiya: “Roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA; na furaha yake itakuwa katika kumcha BWANA.” (Isaya 11:2, 3a) Mesiya ateuliwa na roho takatifu ya Mungu, wala si kwa kutiwa mafuta. Jambo hilo latukia kwenye ubatizo wa Yesu, Yohana Mbatizaji aonapo roho takatifu ya Mungu iliyo kama njiwa ikiteremka juu ya Yesu. (Luka 3:22) Roho ya Yehova ‘yakaa juu ya’ Yesu, naye atoa uthibitisho wa jambo hilo atendapo kwa hekima, ufahamu, shauri, uweza, na ujuzi. Ni sifa bora kama nini anazostahili mtawala kuwa nazo!
Juu ya Nini Tunapaswa Kumuogopa Yehova?
Mutu mwenye anamuogopa Mungu mu njia yenye kufaa anamupendaka na hafanyake jambo yoyote yenye inaweza kuharibisha urafiki wake pamoya naye. Yesu “alimuogopa Mungu” mu ile njia. (Ebr. 5:7) Hakumuogopa mu njia yenye haifae. (Isa. 11: 2, 3) Lakini, alimupenda sana na alipenda kumutii. (Yoh. 14:21, 31) Sawa vile Yesu, tunamuheshimiaka sana Yehova ao kumutii juu iko na upendo, hekima, haki, na nguvu. Tunajua pia kama Yehova anatupendaka sana na kama anahangaikiaka namna tunatenda wakati anatupatia muongozo. Tunaweza kuhuzunisha ao kufurahisha moyo wake.—Zb. 78:41; Mez. 27:11.
Usihukumu Mutu Kulingana na Namna Anaonekana kwa Inje
UNABII wa Isaya juu ya Yesu Kristo unatutia moyo na kutupatia tumaini. Isaya alitabiri kama Yesu “hatahukumu kulingana na mambo yenye anaona kwa macho yake, wala kukaripia kulingana tu na mambo yenye anasikia kwa masikio yake” na kama “atawahukumu kwa haki watu wa hali ya chini.” (Isa. 11:3, 4) Sababu gani jambo hilo linatutia moyo? Kwa sababu tunaishi katika ulimwengu wenye kujaa ubaguzi, na watu wanahukumu wengine kulingana na mambo yenye wanaweza kuona. Tuko kabisa na lazima ya Yesu, Muamuzi mukamilifu, mwenye hatatuhukumu kulingana na namna tunaonekana kwa inje!
ip-1-SW uku. 161 fu. 11
Wokovu na Kushangilia Chini ya Utawala wa Mesiya
Wafuasi wake wanapohitaji kurekebishwa, Yesu huwarekebisha kwa njia inayowanufaisha zaidi—kielelezo bora kwa wazee Wakristo. Kwa upande mwingine, wale wanaozoea uovu wanatarajia hukumu kali. Mungu atakapouhukumu mfumo huu wa mambo, Mesiya “ataipiga dunia” kwa sauti yake yenye mamlaka, huku akitoa hukumu ya kuharibu waovu wote. (Zaburi 2:9; linganisha Ufunuo 19:15.) Hatimaye, hakutabaki watu wowote waovu wanaoharibu amani ya wanadamu. (Zaburi 37:10, 11) Yesu, ambaye viuno vyake vimefungwa kwa haki na uaminifu, ana uwezo wa kutekeleza hayo.—Zaburi 45:3-7.
Mali ya Kiroho
‘Kuleta Watu Wengi Kwenye Haki’
Wale wote wenye watafufuliwa watakuwa na lazima ya kufundishwa. (Isa. 26:9; 61:11) Njo maana, Ufalme wa Mungu utaanzisha kazi kubwa ya kufundisha watu yenye haiyafanyikaka. (Soma Isaya 11:9, 10.) Juu ya nini? Juu wenye hawako wenye haki wenye watafufuliwa watakuwa na lazima ya kujifunza juu ya Yesu Kristo, Ufalme, bei ya ukombozi, jina ya Yehova, na juu ya nini yeye tu njo iko na haki ya kutawala. Hata wenye haki watakuwa na lazima ya kujifunza juu ya mambo yenye Yehova amefundisha pole kwa pole watu wake kuhusu mipango yenye iko nayo juu ya dunia. Wamoja kati ya wale waaminifu walikufaka zamani sana mbele kazi ya kuandika Biblia imalizike. Wenye hawako wenye haki na wenye haki, wote watakuwa na mambo mingi ya kujifunza.
TAREHE 29/12–4/1
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU ISAYA 14-16
Baadui ya Mungu Batapata Malipizi
Ukuwe Hakika Kama ‘Neno la Mungu Ni Kweli’
Mu Biblia muko maunabii mingi yenye ilitimia. Maunabii fulani iliandikwa na ikatimia kisha miaka mingi kupita. Historia inahakikisha kama ile maunabii ilitimia kabisa. Ile haitushangaze juu tunajua kama ile maunabii yote yenye kuwa mu Biblia inatoka kwa Yehova. (Soma 2 Petro 1:21.) Fikiria unabii kuhusu kuanguka kwa muji wa zamani wa Babiloni. Mu karne ya munane M.K.Y., Yehova aliongoza nabii Isaya atabiri kama muji wenye nguvu wa Babiloni utakamatwa. Alitaya na mutu wa kukamata ule muji, ni kusema, Koreshi, na alionyesha waziwazi namna ule muji ungekamatwa. (Isa. 44:27–45:2) Alitabiri pia kama Babiloni itaharibiwa na haitaikaliwa tena. (Isa. 13:19, 20) Ni vile mambo ilikuwa kabisa. Wamedi na Waajemi walikamata muji wa Babiloni mu mwaka wa 539 M.K.Y. Leo, fasi kwenye kulikuwa ule muji kuko tu mabomoko.—Ona video Biblia Ilisemaka Kama Babiloni Itaharibiwa mu kitabu Furahia Maisha Milele! ya kielektroniki, somo ya 03, nukta ya 5.
ip-1-SW uku. 189 fu. 1
Shauri la Yehova Dhidi ya Mataifa
YEHOVA aweza kutumia mataifa kuwatia nidhamu watu wake kwa sababu ya uovu wao. Ijapokuwa hivyo, hayapi msamaha mataifa hayo kwa ajili ya ukatili wao usiostahili, kiburi, na kuchukia kwao ibada ya kweli. Basi, muda mrefu mapema, yeye ampulizia Isaya kurekodi “ufunuo juu ya Babiloni.” (Isaya 13:1) Hata hivyo, Babiloni ni tisho la wakati ujao. Katika siku ya Isaya, Ashuru yawakandamiza watu wa agano wa Mungu. Ashuru yaharibu ufalme wa kaskazini wa Israeli na kuangamiza sehemu nyingi za Yuda. Lakini ushindi wa Ashuru ni wa muda tu. Isaya aandika: “BWANA wa majeshi ameapa, akisema, Hakika yangu kama vile vilivyoazimia, ndivyo itakavyokuwa . . . kwamba nitamvunja huyo Mwashuri vipande vipande katika nchi yangu, na juu ya mlima wangu nitamkanyaga chini ya miguu yangu; ndipo nira yake iliyo juu yao itakapoondoka, na mzigo wake utatoka mabegani mwao.” (Isaya 14:24, 25) Muda mfupi baada ya Isaya kutangaza unabii huo, tisho la Ashuru laondolewa nchini Yuda.
ip-1-SW uku. 194 fu. 12
Shauri la Yehova Dhidi ya Mataifa
Unabii huo utatimizwa lini? Hivi karibuni. “Hilo ndilo neno lile alilolisema BWANA juu ya Moabu zamani. Lakini sasa BWANA asema hivi, Katika muda wa miaka mitatu, kama miaka ya mtu wa mshahara, utukufu wa Moabu utadharauliwa, pamoja na wingi wake wote; mabaki yake yatakuwa machache sana, kama si kitu kabisa.” (Isaya 16:13, 14) Kwa kupatana na hayo, kuna uthibitisho wa kiakiolojia kwamba, mnamo karne ya nane K.W.K., Moabu iliteseka sana na sehemu nyingi nchini mwake zikaachwa ukiwa. Tiglath-pilesa wa Tatu alimtaja Salamanu wa Moabu miongoni mwa watawala waliomlipa ushuru. Senakeribu alipokea ushuru kutoka kwa Kamusunadbi, mfalme wa Moabu. Watawala wa Ashuru, Esar-hadoni na Ashurbanipali walisema kuwa waliwatawala Wafalme Musuri na Kamashaltu wa Moabu. Karne kadhaa zilizopita, Wamoabi walikoma kuwa kikundi cha watu. Magofu ya majiji yanayodhaniwa kuwa ya Wamoabi yamevumbuliwa, ingawa hadi sasa kuna uthibitisho mchache ambao umefukuliwa unaohusu adui huyo wa Israeli ambaye hapo awali alikuwa mwenye nguvu sana.
Mali ya Kiroho
w06 1/12 uku. 10 fu. 11
Mambo Makubwa Katika Kitabu ya Isaya—I
14:1, 2—Namna gani batu ya Yehova balikamata ‘mateka bale benye balikuwa banabashika bakiwa bametekwa’? Ile ilionekanaka wazi mu maisha ya batumishi fulani sawa vile Danieli, mwenye alifikiaka kuwa ofisa mukubwa wa Babiloni wakati wa Wamedi na Waajemi; pia Esta, mwenye alifikia kuwa malkia wa Waajemi; na Mordekai, mwenye alifikia kuwa mukubwa wa bakubwa bote mu Uajemi.
Hotuba: Unabii Ni Nini?
ijwbq-SW habari ya 108
Unabii Ni Nini?
Jibu la Biblia
Unabii ni ujumbe ulioongozwa na roho ya Mungu, ufunuo kutoka kwa Mungu. Biblia inasema kwamba manabii “walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.” (2 Petro 1:20, 21) Kwa hiyo, nabii ni mtu anayepokea ujumbe kutoka kwa Mungu na kuwapitishia wengine ujumbe huo.—Matendo 3:18.
Manabii walipataje ujumbe kutoka kwa Mungu?
Mungu alitumia njia kadhaa kuwapitishia manabii wake mawazo yake:
Maandishi. Mungu alitumia njia hii angalau pindi moja alipompa Musa zile Amri Kumi zikiwa zimeandikwa.—Kutoka 31:18.
Kupitia malaika. Kwa mfano, Mungu alitumia malaika kumletea Musa ujumbe ambao alipaswa kumpelekea Farao wa Misri. (Kutoka 3:2-4, 10) Wakati ambapo maneno hususa yalikuwa muhimu, Mungu aliwaongoza malaika wamwambie mtu maneno hususa ya kuandika, kama alivyofanya alipomwambia Musa hivi: “Jiandikie maneno haya, kwa sababu ninafanya agano pamoja nawe na Israeli kupatana na maneno haya.”—Kutoka 34:27.
Maono. Nyakati nyingine nabii alipokea maono alipokuwa macho na akiwa anafahamu kabisa kinachoendelea. (Isaya 1:1; Habakuki 1:1) Maono mengine yalikuwa halisi kabisa hivi kwamba wahusika waliyashiriki. (Luka 9:28-36; Ufunuo 1:10-17) Pindi nyingine, maono yalipitishwa mhusika akiwa katika njozi. (Matendo 10:10, 11; 22:17-21) Pia Mungu aliwasilisha ujumbe wake katika ndoto wakati ambapo nabii alikuwa amelala.—Danieli 7:1; Matendo 16:9, 10.
Kuongoza akili. Mungu aliongoza mawazo ya manabii wake ili kupitisha ujumbe wake. Hiyo ndiyo maana inayotolewa na maneno haya ya Biblia: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” Maneno hayo yanayosema “limeongozwa na roho ya Mungu” yanaweza pia kutafsiriwa “lenye pumzi ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16; Union Version) Mungu alitumia roho yake takatifu, au kani ya utendaji, kuingiza mawazo yake katika akili za watumishi wake. Ujumbe ulikuwa wa Mungu, lakini manabii ndio waliochagua namna ya kuyapanga maneno.—2 Samweli 23:1, 2.
Je, nyakati zote unabii unahusisha kutabiri wakati ujao?
Hapana, unabii wa Biblia hautabiri tu kuhusu mambo ya wakati ujao. Hata hivyo, ujumbe mwingi kutoka kwa Mungu unahusiana na wakati ujao, hata ikiwa si moja kwa moja. Kwa mfano, manabii wa Mungu waliwaonya Waisraeli wa kale kuhusu njia zao mbaya. Maonyo hayo yalifafanua baraka za wakati ujao ikiwa watu wangetii, na pia yalitaja madhara ambayo wangepata kwa kutotii. (Yeremia 25:4-6) Matokeo yalitegemea njia ambayo Waisraeli waliamua kufuata.—Kumbukumbu la Torati 30:19, 20.
Mifano ya unabii wa Biblia usiohusisha utabiri
Pindi moja Waisraeli walipomwomba Mungu msaada, alituma nabii kueleza kwamba kwa kuwa walikataa kutii amri za Mungu, basi Mungu alikataa kuwasaidia.—Waamuzi 6:6-10.
Wakati ambapo Yesu alizungumza na mwanamke Msamaria, alifunua mambo kuhusu maisha yake ya zamani ambayo hangeweza kuyajua bila kufunuliwa na Mungu. Mwanamke huyo alitambua kwamba Yesu alikuwa nabii hata ingawa hakuwa ametabiri kuhusu wakati ujao.—Yohana 4:17-19.
Wakati wa kesi ya Yesu, maadui wake walimfunika uso, wakampiga, kisha wakamwambia: “Toa unabii. Ni nani aliyekupiga?” Hawakuwa wakimwambia Yesu atabiri wakati ujao bali kwa msaada wa Mungu aseme ni nani aliyempiga.—Luka 22:63, 64.