Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp23 na. 1 uku. 8-9
  • 2 | “Faraja Kutoka Katika Maandiko”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 2 | “Faraja Kutoka Katika Maandiko”
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ile Iko na Maana Gani?
  • Namna Gani ile Inaweza Kusaidia?
  • Vijana Wanashuka Moyo—Sababu Gani? Ni Nini Inaweza Kuwasaidia?
    Amuka!—2017
  • 3 | Mifano ya Biblia Inaweza Kukusaidia
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
  • Kushuka Moyo Kushuka Moyo
    Amuka!—2013
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
wp23 na. 1 uku. 8-9
Mwanaume mwenye kuzeeka iko nafikiri juu ya mambo yenye iko nasoma mu Biblia.

2 | “Faraja Kutoka Katika Maandiko”

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mambo yote yenye yaliandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutoka katika Maandiko tukuwe na tumaini.” —WAROMA 15:4.

Ile Iko na Maana Gani?

Mu Biblia muko mawazo yenye kufariji yenye inaweza kutupatia nguvu na kutusaidia tuvumilie wakati tuko napiganisha mawazo yenye kuvunja moyo. Ujumbe wenye uko mu Biblia unatusaidia tutumainie pia kama hivi karibuni mawazo yenye kuvunja moyo haitakuwa tena.

Namna Gani ile Inaweza Kusaidia?

Siye wote tunajisikiaka mubaya wakati fulani, lakini wale wenye wameshuka moyo ao wenye wako na mahangaiko ya nguvu sana wanaweza kuwa najisikia mubaya sana kila wakati. Namna gani Biblia inaweza kusaidia?

  • Mu Biblia muko mawazo mingi yenye kufaa yenye tunaweza kufikiria pa nafasi ya mawazo yenye haifae. (Wafilipi 4:8) Biblia inaweza kuyaza akili yetu na mawazo yenye kufariji na yenye kutuliza yenye inaweza kutusaidia tujisikie muzuri.—Zaburi 94:18, 19.

  • Biblia inaweza kutusaidia tuepuke kuwaza kama hatuko wa maana.—Luka 12:6, 7.

  • Mu Biblia muko maandiko ya mingi yenye inatuhakikishia kama hatuko peke yetu na kama Mungu, Muumbaji wetu, anaelewa kabisa namna tunajisikiaka.—Zaburi 34:18; 1 Yohana 3:19, 20.

  • Biblia inaahidi kama Mungu atamaliza mawazo yenye kuvunja moyo. (Isaya 65:17; Ufunuo 21:4) Wakati tuko nateseka juu ya mawazo yenye kutuhuzunisha, ile tumaini inaweza kutusaidia tukuwe na nguvu ya kuvumilia.

Namna Biblia Iko Nasaidia Jessica

Namna Ugonjwa wa Kushuka Moyo Unanihangaishaka

Jessica analala na Biblia yenye kuwa wazi mu mukono.

“Wakati nilikuwa na miaka 25, nilikuwa na mahangaiko mingi na wanganga walisema kama nilikuwa na ugonjwa wa kushuka moyo sana. Nilikuwa nateseka sana juu ya mawazo yenye sikuweza kuzuia ya mambo yenye kuhuzunisha yenye ilishakapita. Wanganga walinisaidia kujua kama juu nilikuwa na mawazo yenye haifae kuhusu mambo fulani ya mubaya yenye ilitokeaka mu maisha yangu, njo maana nilifikia kuwa mwenye kushuka moyo. Nilikunywa madawa na pia wanganga walinisaidia nijue mawazo ya mubaya yenye nilikuwa nayo na niiepuke.”

Namna Biblia Inanisaidiaka

“Mu kipindi yenye nilikuwa najisikia mubaya sana juu ya ugonjwa wangu wa kushuka moyo, nilikuwa na wasiwasi sana, nilikuwa na mahangaiko ya mingi, na nilikuwa nakosa usingizi. Mara mingi usiku nilikuwa nalemewa na mawazo yenye kuhangaisha. Vile Zaburi 94:19 inafasiria, Mungu anaweza kutufariji na kututuliza wakati mahangaiko inatulemea. Kwa hiyo nilikuwa naweka Biblia na buku yenye iko na maandiko yenye kutia moyo pembeni ya kitanda yangu. Wakati nilikuwa nashindwa kulala, nilikuwa nasoma maandiko fulani ya Biblia. Na ni mu ile njia njo nilikuwa naacha mawazo ya Mungu inifariji.

“Biblia inatutia moyo tutupilie mbali mawazo yoyote yenye iko tofauti na mambo yenye tunajua juu ya Mungu. Zamani nilikuwa hakika kama siko wa maana, hakuna mutu mwenye anaweza kunipenda, na niko tu wa bure. Lakini nilijifunza kama ile mawazo haipatane hata kidogo na mafundisho ya Biblia. Juu Biblia inaonyesha kama Mungu ni Baba mwenye upendo na mwenye huruma mwenye anahangaikiaka kila mumoya wetu kipekee. Pole kwa pole nilifikia kuanza kutawala mawazo yangu kuliko kuacha mawazo yangu initawale.

“Nilijifunza kujiona vile Mungu ananionaka. Ile ilikuwa hatua ya maana yenye ilinisaidia niache kujiona kuwa wa bure. Ninangoya kwa hamu wakati wenye mawazo yote yenye kuleta huzuni itaisha. Kujua kama matatizo ya akili itaishaka kunanipatia nguvu ya kuvumilia na kunanisaidia nitumainie kama sitakuwaka tena mwenye kushuka moyo.”

Juu ya Kupata Musaada Ingine:

Soma habari “Msaada Kutoka kwa ‘Mungu wa Faraja,’” mu gazeti Amuka! ya Mwezi wa 7, 2009 ku jw.org.

Sikiliza usomaji wa kitabu ya Zaburi ku jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine